Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Wana jamvi kuna hili jambo limenifika, nikaona bora nililete hapa nipate busara zenu.Juzi nilimpeleka mke wangu hospital, wakati yuko ndani na daktari(male) alikaa muda mrefu sana. Sasa wakati tuko njiani nikamuuliza kwa nini kachelewa sana, akanijibu kuwa daktari ana tabia mbaya, nikamuuliza kafanya nini? Akaniambia ni kawaida daktari wa uzazi kumshika mgonjwa viungo vya uzazi kwa ajili ya checking. Lakini jinsi huyu daktari alivyokuwa anamshika alikuwa ana lake jambo. Kwa sababu alimshika matiti kwa namna ya kumtomasa tomasa, akawa anamuingiza vidole ukeni,baada ya muda anarudia rudia kisha anajifanya kama anaandika details.Sasa wana JF nilikuwa nauliza hivi ni kawaida kwa daktari wa uzazi kufanya hivi vitendo?? Naombeni mnipe jibu na ushauri kabla sijaenda kumchukulia RB na hatua zaidi