Mbongo Orijino
New Member
- Aug 4, 2009
- 3
- 0
Kuna habari nimezipata toka kwa mmoja ya wadau juu ya utendaji usioridhisha wa Uongozi wa TSN au wachapishaji wa gazeti kongwe kuliko yote Daily News na Habari Leo, Japo si wazi lakini yasemekana kuna kama kamgomo baridi fulani hivi kutokana na wafanyakazi kutoridhishwa na utendaji huo na yasemekana ni miaka karibia sita sasa hakuna nyongeza ya aina yoyote ya mshahara tofauti na enzi za boss wa zamani ambaye baadaye alipelekwa Ikulu, zaidi kinachofanyika ni kama usanii hivi na uongozi ambao nao kwa sasa upo kama haupo vile kwa kuwapiga kalenda wafanyakazi kila mwaka kama watoto wa kuku vile kuwa watanyonya kesho.
Zipo tuhuma nyingi na nyingine ziliwahi hata kuandikwa na gazeti fulani juu ya ukabila, upendeleo na zaidi viongozi wake kuwa Ma Vasco Dagama fulani kwa kupishana angani au juu kwa juu tu, na yasemekana wengi wa wafanyakazi ambao wameendelea kuwapo pale wapo kwa ajili ya kontact tu kwa wengi wana makampuni yao ambayo ndo yanawashughulisha zaidi kuliko TSN.
Wenye data kamili naomba mtupatie na hasa wana JF waliopo hapo TSN (naamini wapo) kwani hili ni shirika la umma na si mali ya mtu binafsi na Watanzania wana haki ya kujua kile kinachojiri hapo kwa faida ya wote.
Zipo tuhuma nyingi na nyingine ziliwahi hata kuandikwa na gazeti fulani juu ya ukabila, upendeleo na zaidi viongozi wake kuwa Ma Vasco Dagama fulani kwa kupishana angani au juu kwa juu tu, na yasemekana wengi wa wafanyakazi ambao wameendelea kuwapo pale wapo kwa ajili ya kontact tu kwa wengi wana makampuni yao ambayo ndo yanawashughulisha zaidi kuliko TSN.
Wenye data kamili naomba mtupatie na hasa wana JF waliopo hapo TSN (naamini wapo) kwani hili ni shirika la umma na si mali ya mtu binafsi na Watanzania wana haki ya kujua kile kinachojiri hapo kwa faida ya wote.