Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Mh!Lizzy ujue ni kazi sana kuishi kwa style ya kutochangia kwenye jamii hii ya dotcomu,unaweza tengwa flan hivi.All an all namkubali sana mtu anaeishi kinyume na mazoea,big up kama ni kweli. . . .
Ahh wapi! Kuoa/kuolewa wewe afu wengine tukuchangie! Nani kasema bana! Ukichangiwa kumtunza mwenzako usilalamike! Imefika wakti sasa kujigharimikia nyie wenyewe! Kama unahitaji harusi ama send off basi jua kuwa hilo jukumu lako! Sisi ukitualika twaja na zawadi zetu tu! We fikiria kila mwaka marafiki wangapi wanaoa/olewa! Ukisema umchangie kila mtu watoto wataenda shule kweli? Mtu unakuta hata ajui atakula nini eti naye anajitutumua na harusi/send off! Lazima? Si mwende kwa mchungaji/padre/shehe mkamalizane mrudu kwenye ujenzi wa taifa! Acheni kuiga vitu zingine bana. Tena kwa kuiga waTZ ndo tunaongoza! Juzi eti napita mtaani nakuta maandamano ya mazishi na tarumbeta juu! Dah! Kaaaaaaaaaazi kwelikweli