Dah, Bolingo zilizowahi nibamba

Dah, Bolingo zilizowahi nibamba

Namsikiliza Alain Kounkou "Andolo" bonge moja la Soukous.
 
Ndugu zangu naomba msaada nani alitunga wimbo wenye maneno haya

Mume wangu nimulevi ...ananuka pombe

mume wangu nimulevi... analewa pombe

kambelembele maama...kambelembele maama....

kambelembele mama, kambelembele mama
 
Kuna ile ilikuwa Ku........ma ina uma Ku.........ma ina uma Oooh aliimba Cjui Koffi ilikiwa ni mwendo wa kushika Yale maeneo hata km n ME kwa motion flan hv km unaumwa kweli
 
mayamaya maya mayango shetusi mokei mayamayango doke moke mayawayango mayamayanga nalingio maya eeh. ivi huu wimbo unaitwaje na ni wa nani? msaada tafadhali.
 


_ Ndya by Mpongo Love

Maria Tabola by Sam Mangwana

-Yondo Sister-Sexy yondo

From my childhood n`till now, sichoki kuzikililiza
 
Je, Kuna ukweli wowote kuwa Aurlus Mabele amekuwa Teja?
Siyo teja bana labda kama kaanza siku hizi lakini alikuwa kafulia na anaumwa miguu hawezi hata kutembea kwa muda mrefu sana.

Mimi ni miongoni mwa mashabiki wake wakubwa japo nasikitika hana taarifa kwenye social media.

Huyu jamaa mkosi ulianza kwa kudhulumiwa mgao wa faida ya bendi ya Loketo na mwanzilishi mwenzie wa bendi ya Loketo ambaye ni Dally Kimoko.

Mbaya zaidi akakimbiwa na mkewe huko Ufaransa hasa baada ya kudhulumiwa na kuanza kuumwa miguu na akakosa fedha za matibabu na huduma mbali mbali.

Kwa sasa amepona miguu na inasemekana ameanza harakati za kutaka kurudi kwenye game.

N.B: Chanzo changu ni watu na social networks naweza kurekebishwa pia.
 
bolingo zilikuwa zamani hakika...
na binafsi yangu ukinitajia Mtindo wa Bolingo ninaoukubali basi sisiti kuutaja mtindo uliitwa Soukous...

Na kama utazungumzia Soukous basi Sokous Stars ndo bendi.
Na miongoni mwa nyimbo za Soukous ninazozikubali basi...
1. Rose
2. Robin pretty
3. Sophia
4. Rhoda.
5. Aba goimo
Kisha ktk kundi la sokous alikuwepo shangazi mmoja alieitwa Yondo Kusala maarufu kama Yondo Sister ambae nae alitamba na vibao kama...
1. Cayina
2. Bazzo
3. Mwana kento
4. Wapi yoo
Na nyingine nyiingi sana.

Halafu pakawepo na mtu alieitwa Luciana Bokilo.
Bokilo yeye alitamba na...
1. Aziza
2. Missete
3. One way.

Kisha akaja kamanda mwingine alieitwa Lokasa ya Mbongo ambae nae akapiga ngoma kali kama...
1. Adiza
2. Marijose
3. Monica.
4. Nairobi night amabao kwa pamoja alishirikiana na makamanda wenzie waliounda Soukous Stars.

Machi/5/1989 katika hotel ya New Morning mjini Paris Mpiga gitaa la Bass Ngouma Lokito akiwa na nguli mwenzie ambae ni mcharaza Gitaa la Rythim Lokasa ya Mbongo walianzisha Band ambayo waliibatiza jina la Soukous Stars.

Miongoni mwa members wengine walikuwemo Paris Shimita,
Yondo Sister, Balu kanta na Zitani Nell.. nyota wengi ktk bara hili kama Manu Dibango, Jacob Desvarieux, Jocelyn Kiambukuta na Sam
Mangwana, walikuwapo siku hiyo.

Kituo kikubwa cha matangazo nchini Ufaransa RFI (Radio France International) walirusha LIVE tukio hilo la kumbukumbu.

Mara moja bendi ikawa na ikaanza kufanya maonesho ya LIVE karibu Duniani kote huku wakishirikiana na nyota wengine Barani Efrica.
Baada ya miaka kadhaa kupita Soukous Stars wakajinyakulia umaarufu wa hali ya juu.
miongoni mwa nyota waliokuwepo ktk kundi hilo ambao walitoka nchi mbali mbali barani Africa ni Yondo Sister, Shimita, Nyomba,
Luciana de Mingongo toka Kinshasa, Democratic
Republic of Congo;.

Kisha wakawepo Ballu Canta, Zitani Nell, Pierre
Belcos, Lucien Bokilo toka Congo Brazzaville;

Saladin Saladin wa Central Africa Republic;

Arsene Kounde toka Benin na Joseph Koujojo toka
Cameroon.

Balantanda njoo uwazungumzie Wenge BCBG walipotoka mpaka walipo sasa.
Tafuta wimbo mwingine unaitwa Napika. Sikiliza uje unipe ripoti. Wa Mbilia
Mbilia pia ana Boyaye, phenomeno na yambanga nazikubali sana.
 
ahaaaa ulikuwa upo juu kama ulikuwa umemiliki radio ile ilikuwa inaitwa radio cassete sijui?ile radio kule kwetu moshi kijana alokuwa anaimiliki alikuwa anaonekana lulu kama kijana anaemiliki range now! alikuwa anawindwa balaa...
Teh! Tulikuwa na zile ziliitwa Lasonic zilikuja nadhani ni copy ya Panasonic ila hizi zikawa ni modern kidooogo na ilikuwa inapiga zaidi!!

Kanda za redio zaidi ya elfu mbili!! Mh! Ilitufanya tukawajua wanawake mapema aisee
 
Wakuu msaada tafadhali,

Nani alitunga wimbo wenye maneno haya

Mume wangu nimulevi ...ananuka pombe

mume wangu nimulevi... analewa pombe

kambelembele maama...kambelembele maama....

kambelembele mama, kambelembele mama
 
Asante kwa kunikumbusha enzi hizo haswa Soukoss star, Bokilo na Salmon Rama niliwapenda sana alipokuwa kundi la Loketo
Remy Sahlomon alimtegemea sana Dally Kimoko katika nyimbo zake..hakuwa mtu wa mashairi mengi sana ila Guitar 🎸 lilitawala.
 
Back
Top Bottom