Basil Lema
Member
- Jan 20, 2013
- 86
- 277
Waheshimiwa wanajamvi kwa sasa ninaweka habari hii hapa kama tetesi kwa malengo mawili:
1. Kuwafanya wahusika wajue kuwa hila zao zimeshajulikana.
2. Kufuatilia zaidi nyendo za wahusika na hatimaye tulete updates hapa hapa jukwaani.
Jana nilipata habari kutoka kwa chanzo muhimu cha ndani kabisa kwa,ba maofisa wa tume ya uchaguzi wameelekea jijini Arusha kwa lengo la kwenda kurekebisha daftari la kudumu la wapiga kura kwa kata nne zenye uchaguzi.
Maofisa hao ni pamoja na makarani wa kupiga picha na wajuzi wa IT. Imepangwa wafanye kazi hiyo hadi Jumanne tarehe 2/7/2013. Kama mpango wao huo ukifanikiwa Tume inaamini kwamba kwa kila kata kutakuwa na rekebisho la walau 38%. Hili rekebisho litakuwa kura za msingi za kuipa CCM ushindi kwa kata zote nne.
Nikiwa bado natafuta habari zaidi naomba nitoe kwa muhtasari maeneo yatakayorekebishwa.
1. Watu wote walioondoka Arusha ama kwa kufariki, kusafiri au kuhama mapengo yao yatazibwa na wapiga kura maalum watakaopewa shahada kwa ajili yao.
2. Wapiga kura wanaojulikana wazi kuwa wa CDM watafuatwa kwa malengo ya kuombwa wauze shahada zao, wengine zitaibiwa na wale wagumu kabisa watawekwa rumande siku za kuelekea uchaguzi mdogo.
Wakubwa serikalini na ndani ya CCM wanahitaji ushindi Arusha mjini kwa udi na uvumba hivyo kama wakigundua mbinu zao za ushindi zimegundulika ama kwamba zitagonga mwamba wataahirisha tena uchaguzi kwa kisingizio cha usalama.
Hadi sasa jeshi la polisi linapangwa kwa ajili ya kupelekwa Arusha kwa lengo la kusaidia utekelezaji wa mbinu hizi za kihuni za CCM kwa kisingizio cha kuimarisha usalama.
Stay tuned!!
1. Kuwafanya wahusika wajue kuwa hila zao zimeshajulikana.
2. Kufuatilia zaidi nyendo za wahusika na hatimaye tulete updates hapa hapa jukwaani.
Jana nilipata habari kutoka kwa chanzo muhimu cha ndani kabisa kwa,ba maofisa wa tume ya uchaguzi wameelekea jijini Arusha kwa lengo la kwenda kurekebisha daftari la kudumu la wapiga kura kwa kata nne zenye uchaguzi.
Maofisa hao ni pamoja na makarani wa kupiga picha na wajuzi wa IT. Imepangwa wafanye kazi hiyo hadi Jumanne tarehe 2/7/2013. Kama mpango wao huo ukifanikiwa Tume inaamini kwamba kwa kila kata kutakuwa na rekebisho la walau 38%. Hili rekebisho litakuwa kura za msingi za kuipa CCM ushindi kwa kata zote nne.
Nikiwa bado natafuta habari zaidi naomba nitoe kwa muhtasari maeneo yatakayorekebishwa.
1. Watu wote walioondoka Arusha ama kwa kufariki, kusafiri au kuhama mapengo yao yatazibwa na wapiga kura maalum watakaopewa shahada kwa ajili yao.
2. Wapiga kura wanaojulikana wazi kuwa wa CDM watafuatwa kwa malengo ya kuombwa wauze shahada zao, wengine zitaibiwa na wale wagumu kabisa watawekwa rumande siku za kuelekea uchaguzi mdogo.
Wakubwa serikalini na ndani ya CCM wanahitaji ushindi Arusha mjini kwa udi na uvumba hivyo kama wakigundua mbinu zao za ushindi zimegundulika ama kwamba zitagonga mwamba wataahirisha tena uchaguzi kwa kisingizio cha usalama.
Hadi sasa jeshi la polisi linapangwa kwa ajili ya kupelekwa Arusha kwa lengo la kusaidia utekelezaji wa mbinu hizi za kihuni za CCM kwa kisingizio cha kuimarisha usalama.
Stay tuned!!