Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Rafiki yangu Yericko Nyerere ameandika kwenye kitabu chake cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, umuhimu wa kupeana taarifa (za maana) baina ya mahakama, wizara ya mambo ya ndani na idara zake... Hapa ni katika kuboresha tasnia ya usalama wa taifa.
Mimi naamini kama taasisi ya Urais (ikulu), wizara ya mambo ya ndani na idara zake pamoja na mahakama wangeshirikana kwa kupeana taarifa- (bila kuathiri haki za kiraia) ndege yetu isingekamatwa na Mkulima Hermanus huko J'burg - SA.
Kumbe, kesi iliyotolewa hukumu na mahakama kuu ya nchi moja mwanachama wa SADC inaweza kusajiliwa na hukumu hiyo ikatekelezwa na mahakama kuu ya nchi nyingine mwanachama wa jumuia ya SADC. Ndio maana mkulima Hermanus aliamua kusajili hukumu ya kesi ya mahakama kuu ya Tanzania iliyoamuru alipwe fidia ya pesa zake, akaisajili huko J'burg Afrika kusini - kwa kufuata kanuni za jumuia ya SADC.
Swali?
Waliomfutia uraia na kumzuia Hermanus asiingie nchini - (bila shaka walilenga kumdhulumu madai yake) Je! Hawakujua kama angeweza kusajili hukumu ya mahakama kuu ya Tanzania katika mahakama kuu ya Gauteng - Afrika Kusini?
Je! Hakuna mtu miongoni mwa watoa maamuzi aliyejua kanuni hii ya SADC?
Kuna mtu anaitwa Profesa Kabudi Paramaganda, waziri wa mambo ya nje na mwenyekiti baraza la mawaziri wa nchi za SADC. Mapema mwezi Agosti alitawala vyombo vya habari akionekana kuhubiri kwenye mimbari za mkutano wa SADC, na zaidi ya hapo ni mbobezi wa sheria. Huyu ameshiriki kikamilifu kumfutia uraia Bwana Hermanus.
Je! Profesa Kabudi, kwa nafasi hizo alizokuwa nazo hakujua kanuni hii ya SADC?
Hakuna namna ya Profesa Kabudi kuepuka lawama kwenye jambo hili. Uzalendo uchwara wa kukurupukia mambo unatugharimu sasa - tunakwenda kulipa gharama kubwa kwa mkupuo. Mkulima amekuwa akidai deni kwa miaka 37, hiyo subira ni ya kimalaika - lakini awamu ya tano ikamuona msumbufu, ikamfutia uraia wake wa kuasili na kumzuia kuingia nchini. Lengo ni nini kama sio kumdhulumu? Au kama ana makosa mengine kwanini asishitakiwe?
Imekula kwetu. Taarifa kutoka J'burg zinadai kuna namna mbili tu ya kuipata ndege yetu Aribus 220-300 yenye thamani ya dola 90 milioni; Moja ni kumlipa Hermanus fedha zake zote kwa mkupuo, Pili ni kuweka dhamana ya mali yenye thamani sawa au zaidi ya deni analodai Hermanus. Hakuna kitu watafanya wanasheria wa serikali ya Tanzania waliokwenda South Afrika zaidi ya kupiga selfie. Hivyo yani.
Next time, jambo linalogusa mahakama, mambo ya nje, mambo ya ndani na idara zake, liamuliwe baada ya majadiliano na kupeana taarifa kutoka pande zote husika.
Wapo watu walijua kinachoweza kutokea lakini wakisema tu! wanaitwa wasaliti, maadui...ooh sio wazalendo! Sasa tukome kukurupuka.
Mimi naamini kama taasisi ya Urais (ikulu), wizara ya mambo ya ndani na idara zake pamoja na mahakama wangeshirikana kwa kupeana taarifa- (bila kuathiri haki za kiraia) ndege yetu isingekamatwa na Mkulima Hermanus huko J'burg - SA.
Kumbe, kesi iliyotolewa hukumu na mahakama kuu ya nchi moja mwanachama wa SADC inaweza kusajiliwa na hukumu hiyo ikatekelezwa na mahakama kuu ya nchi nyingine mwanachama wa jumuia ya SADC. Ndio maana mkulima Hermanus aliamua kusajili hukumu ya kesi ya mahakama kuu ya Tanzania iliyoamuru alipwe fidia ya pesa zake, akaisajili huko J'burg Afrika kusini - kwa kufuata kanuni za jumuia ya SADC.
Swali?
Waliomfutia uraia na kumzuia Hermanus asiingie nchini - (bila shaka walilenga kumdhulumu madai yake) Je! Hawakujua kama angeweza kusajili hukumu ya mahakama kuu ya Tanzania katika mahakama kuu ya Gauteng - Afrika Kusini?
Je! Hakuna mtu miongoni mwa watoa maamuzi aliyejua kanuni hii ya SADC?
Kuna mtu anaitwa Profesa Kabudi Paramaganda, waziri wa mambo ya nje na mwenyekiti baraza la mawaziri wa nchi za SADC. Mapema mwezi Agosti alitawala vyombo vya habari akionekana kuhubiri kwenye mimbari za mkutano wa SADC, na zaidi ya hapo ni mbobezi wa sheria. Huyu ameshiriki kikamilifu kumfutia uraia Bwana Hermanus.
Je! Profesa Kabudi, kwa nafasi hizo alizokuwa nazo hakujua kanuni hii ya SADC?
Hakuna namna ya Profesa Kabudi kuepuka lawama kwenye jambo hili. Uzalendo uchwara wa kukurupukia mambo unatugharimu sasa - tunakwenda kulipa gharama kubwa kwa mkupuo. Mkulima amekuwa akidai deni kwa miaka 37, hiyo subira ni ya kimalaika - lakini awamu ya tano ikamuona msumbufu, ikamfutia uraia wake wa kuasili na kumzuia kuingia nchini. Lengo ni nini kama sio kumdhulumu? Au kama ana makosa mengine kwanini asishitakiwe?
Imekula kwetu. Taarifa kutoka J'burg zinadai kuna namna mbili tu ya kuipata ndege yetu Aribus 220-300 yenye thamani ya dola 90 milioni; Moja ni kumlipa Hermanus fedha zake zote kwa mkupuo, Pili ni kuweka dhamana ya mali yenye thamani sawa au zaidi ya deni analodai Hermanus. Hakuna kitu watafanya wanasheria wa serikali ya Tanzania waliokwenda South Afrika zaidi ya kupiga selfie. Hivyo yani.
Next time, jambo linalogusa mahakama, mambo ya nje, mambo ya ndani na idara zake, liamuliwe baada ya majadiliano na kupeana taarifa kutoka pande zote husika.
Wapo watu walijua kinachoweza kutokea lakini wakisema tu! wanaitwa wasaliti, maadui...ooh sio wazalendo! Sasa tukome kukurupuka.