Ndg wana JF. Wasalamu.
Hivi karibuni nimejaribu kupitia michango/thread zilizoletwa na mtajwa hapo juu.
Mkuu
guzman_ , kwanza asante kunianzishia thread.
Kwa namna ya uandishi wake na mawazo yake imenilazimu kutaka kujua Pascal Mayala ni nani hasa?
Pascal Mayalla ni mwana JF mwenzenu mtu wa kawaida sana.
Kiwango changu rasmi cha elimu ni darasa la 7, ila baada ya hapo nikaanza kuungaunga mara usome hiki mara kile, nikaungaunga hadi nikawa mwandishi wa habari na mtangazaji, nikaendelea kujisomea kwa kujisomesha kwa elimu ya kuunga unga hadi kuhitimu shahada ya sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM, ambapo ilinichukua miaka 15 kukabidhiwa LL.B yangu na ikanichukua miaka 5 mingine kukubaliwa kuwa wakili.
professional yake ni nini?
Professional yangu ni Mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea na sasa ni Wakili wa kujitegemea kwa kujitolea kutetea haki kwa watu na uwezo wa kuajiri wakili.
Historia yake ya kiafya ikoje (Hasa ya kiakili)
Niliwahi pata ajali mbaya ya Piki Piki nikadhaniwa nimekufa kumbe nilizimia tuu nikafufukia baridi la mortuary, kwa muda niliozimia madaktari wakasema nitakuwa confined to a wheelchair!, nilikuja kusimama and here I'm.
?Na kama mtanzania au la! n.k
Sio tuu ni Mtanzania, bali ni Mtanzania original halisi na Mzalendo wa kweli wa taifa hili.
NB: Naamini hamna mtu anaweza kuwa na fikra kubwa kama huyu jamaa.
Asante
Kitendo cha kuleta mada ya mkuu wetu wa mkoa kuwa Raisi wa JMT baada ya JPM binafsi nimeona ni suala zuri ila nani kaleta mawazo hayo ndo nataka kujua profile yake.
Mimi naandikia watu watatu humu
- Kuna mada nawaandikia wananchi wa kawaida simple minds, ambao hawahitaji kufikiri chochote, wao interest zao ni kusikia tuu chochote, hizi ni mada kuwahusu watu, naziandika kwa ajili ya simple minds ambao wao interest zao ni habari za watu.
- Mimi kama Mwandishi wa habari, kuna mada naripoti kuhusu matukio mbalimbali, Kwa ajili ya ordinary minds ambao hu discuss events, kumetokea nini wapi na ikawaje.
- Na kuna mada naziandika kwa ajili ya great minds, hizi ni mada kuhusu ideas na wasomaji they need to think. Mada hizi huziandika kwa coded ili kuelewa nazungumzia nini ni lazima kwanza uwe na uwezo to read in between the lines, pili uwe na uwezo wa kuzibaini hizo codes na uncode the codes to connect the dots.
Ikitokea wewe ni simple mind ukakutana na mada ya great minds, utaishia chaka!. Hiki ndicho kilichokukuta wewe uliposoma bandiko hili
Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze..., ukikutana na mada iliyokuzidi kimo, lazima utaishia kuingia chaka. Pole.
Ila pia kiukweli nimeisaidia sana jf kuwa transforms simple minds wengi kuwa great minds. Na wewe uliposoma mwanzo bandiko hilo ulikuwa simple mind, sasa lisome tena huku unatafakari utapata kitu kingine, akisoma ikashindwa kabisa kujua nazungumzia nini, then bandiko hilo sio saizi yako.
Karibu ujaribu, ukishidwa kabisa nitakufungulia baadhi ya codes.
P.