CUF yataka serikali tatu

Moja tu. Muungano utakuwepo milele, ili tuishi kwa kujenga nchi bila porojo mikwara na matusi bora serikali 1 tu.
 
mm naona bora kila nchi ijikate kivyake tutakutana katika Umoja wa Afrika mashariki The East African Community (EAC) kuliko kutafuta matatizo mengine ya kuja kuanza kupigana kati ya WaTanganyika na WaZanzibari.....Nchi zote za Africa zinaishi bila ya muungano kama wetu na ziko poa wanaendelea na maisha bora kuliko sisi tuliokuwa na Muungano ni lawama tupu sitaki hata kusikia kitu kinaitwa muungano tena:ban:
 
kumbuka Muungano lazima/muhimu/nashauri uwepo ila sababu zipi unafikiri za muhimu katika kutetea hoja ya serikali moja au tatu. mbili ndo hizi zilizozaa sintofahamu mpaka leo kwa hiyo haifai.

Hoja ya Muungano na Jawapu la Muungano liko kwa Wananchi wa Pande mpili za Muungano yani Tanganyika na Zanzibar pindipo MMoja akisema hautaki Muungano au ni Muungano gani basi hapo ndipo utapata jawabu lako.
 
Serekali ya zanzibar na serekali ya tanganyika basi kila nchi na mambo yake tusitiane jasho .kama ushirika EAC,AU.UN zipo na kuna nafasi ya nchi na nchi kuingia mikataba ya maslahi . Muungano wa tz ni wizi mtupuu
 
union-label.jpg




Unguja na Pemba ziwe mojawapo katika wilaya za nchi iitwayo Tanzania, aina yoyote nyingine ya Muungano ni ujinga, upuuzi na upotezaji wa muda, full stop.
 
Yaani si kuamini pale niliposikia katika moja ya mikutano ya CHADEMA, wakitonya kuwa wao wanamsimamo wa serikali tatu,wakiwa na maana ya Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.

Kwa kweli kama watazidi kuitajataja karata hii basi litakuwa ni dume la kusafiria na bila ya shaka yeyote ile litawafikisha kileleni zaidi ni kuwa wasimamizi wa maneno yao. Tatizo imekuwa kama wana uwoga fulani fulani katika kutamka hadharani na kwa uwazi na ufafanuzi zaidi.

WaTanganyika wanaihitaji kauli hii iwe ni kauli mbiu kuelekea uchaguzi mkuu ujao kuwa ni zamu ya Tanganyika kuwa na serikali yao.
 
Kwani kutakuwa na Faida gani kukiwepo Serikali 3? Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar... Mwiba? Ninavyoelea mimi Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena, hata kukiwa na hizo Serikali 3 Chadema inazozitaka hakutokuwa na Faida yoyote ni kujizidishia Matatizo mengine. Hizo Serikali 2 za Muungano hakuna faida yoyote ile je itakuwa Tanzania kuwa na Serikali3? Tuwasikilize hawa Wa Zanzibar wanachokitaka kwanza ndio halafu tutazungumza kuwepo na Serikali 3 mkuu
 
Kwani kutakuwa na Faida gani kukiwepo Serikali 3? Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar... Mwiba? Ninavyoelea mimi Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena, hata kukiwa na hizo Serikali 3 Chadema inazozitaka hakutokuwa na Faida yoyote ni kujizidishia Matatizo mengine. Hizo Serikali 2 za Muungano hakuna faida yoyote ile je itakuwa Tanzania kuwa na Serikali3? Tuwasikilize hawa Wa Zanzibar wanachokitaka kwanza ndio halafu tutazungumza kuwepo na Serikali 3 mkuu

Mmmmmh
 
Yaani si kuamini pale niliposikia katika moja ya mikutano ya CHADEMA, wakitonya kuwa wao wanamsimamo wa serikali tatu,wakiwa na maana ya Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.

Kwa kweli kama watazidi kuitajataja karata hii basi litakuwa ni dume la kusafiria na bila ya shaka yeyote ile litawafikisha kileleni zaidi ni kuwa wasimamizi wa maneno yao. Tatizo imekuwa kama wana uwoga fulani fulani katika kutamka hadharani na kwa uwazi na ufafanuzi zaidi.

WaTanganyika wanaihitaji kauli hii iwe ni kauli mbiu kuelekea uchaguzi mkuu ujao kuwa ni zamu ya Tanganyika kuwa na serikali yao.
Mwiba, swala la serikali tatu ni swala la Bara zaidi maana kuwepo serikali tatu kunaifanya bara pia kuwa na serikali yake hivyo hakuna chochote kinachoongezeka Visiwani maana tayari wao wanayo serikali yao.

Hivyo, madai ya Wazanzibar kujitenga hayahusiani na kuwepo kwa serikali tatu japokuwa wapo wasioelewa maana ila wanasema tu ziwezo serikali tatu wakidhani kutakuwa na tofauti yoyote kwa Zanzibar. Maadam Zanzibar nia yao ni kujitenga baada ya kutoridhika na muungano kutokana na uroho wa madaraka, kuwepo kwa serikali tatu kuna manufaa zaidi maana hapo ndipo wataijua picha halisi...

Ni wazo zuri sana lakini sii dawa wala kinga, serikali tatu haiwezi kuondoa kero za Wazanzibar maana wanachokidai ni 'sovereign' mamlaka kamili ya kitaifa hasa ktk wizara ya mambo ya nje, Ulinzi na wizara zote zilizomo ndani ya muungano jambo ambalo linapingana na tafsiri yoyote ya muungano.
 
Yaani si kuamini pale niliposikia katika moja ya mikutano ya CHADEMA, wakitonya kuwa wao wanamsimamo wa serikali tatu,wakiwa na maana ya Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.

Kwa kweli kama watazidi kuitajataja karata hii basi litakuwa ni dume la kusafiria na bila ya shaka yeyote ile litawafikisha kileleni zaidi ni kuwa wasimamizi wa maneno yao. Tatizo imekuwa kama wana uwoga fulani fulani katika kutamka hadharani na kwa uwazi na ufafanuzi zaidi.

WaTanganyika wanaihitaji kauli hii iwe ni kauli mbiu kuelekea uchaguzi mkuu ujao kuwa ni zamu ya Tanganyika kuwa na serikali yao.
Mim nakubali kabisa
 
Kwani kutakuwa na Faida gani kukiwepo Serikali 3? Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar... Mwiba? Ninavyoelea mimi Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena, hata kukiwa na hizo Serikali 3 Chadema inazozitaka hakutokuwa na Faida yoyote ni kujizidishia Matatizo mengine. Hizo Serikali 2 za Muungano hakuna faida yoyote ile je itakuwa Tanzania kuwa na Serikali3? Tuwasikilize hawa Wa Zanzibar wanachokitaka kwanza ndio halafu tutazungumza kuwepo na Serikali 3 mkuu

MziziMkavu
nimekupata vema,
tafadhali mkuu kama una
takwimu za kuonyesha wazanzibar wote hawataki muungano naomba uzitupie hapa., ntashukuru sana mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Kwani dawa siku zote hupatikana vipi? sii hutanyika uchunguzi kwanza mgonjwa kufanyiwa vipimo, ukachukuliwa damu ikafahamika ugonjwa kisha unapewa dawa inayohusiana na Ugonjwa. Kinachofanyika leo ni kelele za mgonjwa wa wasiwasi tu ambaye hana maradhi hayo kama yangekuwepo asingekwenda kazini kama tunavyowaona kina Jussa, Maaalim Seif, Karume wote wanaitumikia serikali ya Jamhuri ya muungano. hakuna mgonjwa hapa ila wanatumia ugonjwa wa kitoto kililia mafua ili upikiwe chapati na chai ya hiriki..

Nchi zenye matatizo tuliwaona viongozi wao kina Ojukwu wa Biafra, John Garang wa South Sudan, Hami Awate wa Eritria ambao walikataa hata kuzitumikia serikali zao kwa sababu walitaka kujitenga na kero zilikuwa halali..Lakini ya Zanzibar ni wadudu tu walioko ktk kokwa la embe ambao kazi yao ni kutula taratibu hadi embe lifubae na kuanguka toka mtini.

Serikali tatu, sii dawa bali kutuliza maumivu na presha...Chadema wanaitetea hopja hii kwa maslahi ya bara na ndio maana CUF na Wazanzibar walipiga mahesabu wakagundua kwamba serikali tatu ingekula kwao wakajitoa na kuunda serikali ya mseto ndani ya mfumo uliopo wa muungano kinachobadilika ni kuvikana vyeo kama lilivyokuwa Azimio la Zanzibar.

Hawa wanaofanya chokochoko za muungano wangetakiwa kuwajibishwa lakini kutokana na serikali yetu kuwa dhaifu kiasi kwamba wanashindwa hata kuwawajibisha Mafisadi ndio maana tunaona swala hili ni zito sana na linatuelemea. Wapo watu wanaamini kabisa Ufisadi hauwezi kudhibitiwa, ati Ufidasi hauwezi kwisha upo hata Marekani?... hii mifano ya mwendawazimu wakati tumejaza magereza zetu vibaka ambao pia wezi hawa hawawezi kwisha.

Swala la kero za muungano ni swala la kisiasa na ulaji na linatumiwa ili baadhi ya viongozi wapate kuchaguliwa ktk uchaguzi mkuu wa Zanzibar maana ndivyo wananchi wanaaminishwa kwamba kuna tatizo ktk muungano wakati tatizo ni viongozi wenyewe. Dawa ya kero za muungano ni KATIBA MPYA. Katiba itakayo wabana viongozi wote na kuacha mamlaka hayo kwa wananchi wenyewe kiasi kwamba wakitaka kura za maoni lazima zifanyike, wakitaka kumwondoa kiongozi madarakani wanaweza wakati wowote. Kuondoa au kupunguza madaraka kwa viongozi wa juu, kurudisha miiko na maadili kwa viongozi ambao wameshindwa kutatua matatizo ya Watanzania ndio dawa ya kwanza.

Kuunda serikali tatu itakuja kuunda majimbo na mengine ambayo yote kwa ujumla wake ni ULAJI tu, maana Tanzania kwa eneo ni sawa na state moja ya Marekani au Province moja ya canada lakini budget yake ni chini ya hata mji mmoja wa Marekani ambao una watu wasiozidi millioni 10.

Chukua mfano wa Zanzibar kama jimbo au Nchi, na wameshindwa kama jimbo na wameshindwa pia kama nchi..unaweza kunambia wanashindwa vipi kujiendeleza.. viongozi wake hawna tofauti na wa bara hivyo tunachukua mfano gani ikiwa huu ndogo uliopo machooni mwetu hauna mafao..
- TATIZO ni mambo mawili ambayo ni UONGOZI BORA na Mfumo Mbaya wa Kiutawala (KATIBA) haya ndio dawa na kinga ya kero zote za muungano na umaskini ni kuwabana mbavu tu makupe, mirija na makabaila..
 
Hawa wanaofanya chokochoko za muungano wangetakiwa kuwajibishwa ..

Una maana gani? kwa muda gani unaweza kuwatawala watu uwalazimishe lile unalolitaka wewe? na utawawajibisha vizazi vyote? maana watu wenye manung'uniko na mfumo mzima wa muungano waliaza muda tu baada ya muungano!
 
Una maana gani? kwa muda gani unaweza kuwatawala watu uwalazimishe lile unalolitaka wewe? na utawawajibisha vizazi vyote? maana watu wenye manung'uniko na mfumo mzima wa muungano waliaza muda tu baada ya muungano!
Hawa watu ni kina nani?..maana nijuavyo kila hatua ya Muungano wetu wamefanya mabadilisha Kikatiba kukidhi malalamishi mengi ya Wazanzibar, hadi imefikia leo kuna watu tena Wazanzibar wanauliza kwa nini yaliongezwa maswala ambayo hayakuwepo ktk Artical of Union!...Tutaweza vipi kuridhisha kila mtu wakati ilifanyika kwa ajili ya hawa hawa wanaolalamika. Mkuu wangu hakuna mwenye manung'uniko isipokuwa wachawi ambao hawakushiriki hata ktk Mapinduzi ya Zanzibar, ni kundi la watu wasiopenda hata kuunga Mapinduzi isipokuwa kwa kutambua uhuru wa Sultan..Na kama wangekuwa na uwezo basi wangeweza hata kuindoa hata serikali ya Mapinduzi na kurudisha Zanzibar ile waitakayo. Hata kina Smioth na Botha wanalalamika vile vile kuhusu Zimbabwe na South Africa lakini tunachoweza kuwaambia ni kwamba wakue (grow up) Dunia ile kukoloniwa na uhuru wa bandia imeshapita na haitarudi tena.

Kama yapo madai na manung'uniko ya Wazanzibar basi madai hayo yanahusiana na demokrasia ambayo CCM - Zanzibar kupitia baraza la Mapinduzi imehakikisha hawapati ushindani toka watu wasiokuwa na asili ya Mapinduzi yale. Hivyo hili ni swala la ndani kama mke na mume chumbani, kero zote za Wazanzibar zinatokana na mdudu alokaa ndani ya kokwa nao ni viongozi wenu wenyewe... Tazama ni jana tu waziri wa Fedha wa Zanzibar alitangaza Bajeti ya Visiwani, huyu waziri aliweza vipi kuitanga bajeti ikiwa mnatawaliwa? Na pengine nambie wewe ni Mbara gani alihusika ama kushiriki ktk kuandaa bajeti hiyo? Wamelazimishwa wapi na fedha walizikusanya vipi hadi kuwa na bajeti..
 
Back
Top Bottom