kumbuka Muungano lazima/muhimu/nashauri uwepo ila sababu zipi unafikiri za muhimu katika kutetea hoja ya serikali moja au tatu. mbili ndo hizi zilizozaa sintofahamu mpaka leo kwa hiyo haifai.
Kwani kutakuwa na Faida gani kukiwepo Serikali 3? Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar... Mwiba? Ninavyoelea mimi Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena, hata kukiwa na hizo Serikali 3 Chadema inazozitaka hakutokuwa na Faida yoyote ni kujizidishia Matatizo mengine. Hizo Serikali 2 za Muungano hakuna faida yoyote ile je itakuwa Tanzania kuwa na Serikali3? Tuwasikilize hawa Wa Zanzibar wanachokitaka kwanza ndio halafu tutazungumza kuwepo na Serikali 3 mkuu
Mwiba, swala la serikali tatu ni swala la Bara zaidi maana kuwepo serikali tatu kunaifanya bara pia kuwa na serikali yake hivyo hakuna chochote kinachoongezeka Visiwani maana tayari wao wanayo serikali yao.Yaani si kuamini pale niliposikia katika moja ya mikutano ya CHADEMA, wakitonya kuwa wao wanamsimamo wa serikali tatu,wakiwa na maana ya Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.
Kwa kweli kama watazidi kuitajataja karata hii basi litakuwa ni dume la kusafiria na bila ya shaka yeyote ile litawafikisha kileleni zaidi ni kuwa wasimamizi wa maneno yao. Tatizo imekuwa kama wana uwoga fulani fulani katika kutamka hadharani na kwa uwazi na ufafanuzi zaidi.
WaTanganyika wanaihitaji kauli hii iwe ni kauli mbiu kuelekea uchaguzi mkuu ujao kuwa ni zamu ya Tanganyika kuwa na serikali yao.
Mim nakubali kabisaYaani si kuamini pale niliposikia katika moja ya mikutano ya CHADEMA, wakitonya kuwa wao wanamsimamo wa serikali tatu,wakiwa na maana ya Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.
Kwa kweli kama watazidi kuitajataja karata hii basi litakuwa ni dume la kusafiria na bila ya shaka yeyote ile litawafikisha kileleni zaidi ni kuwa wasimamizi wa maneno yao. Tatizo imekuwa kama wana uwoga fulani fulani katika kutamka hadharani na kwa uwazi na ufafanuzi zaidi.
WaTanganyika wanaihitaji kauli hii iwe ni kauli mbiu kuelekea uchaguzi mkuu ujao kuwa ni zamu ya Tanganyika kuwa na serikali yao.
dawa na kinga ni nini?Ni wazo zuri sana lakini sii dawa wala kinga
Kwani kutakuwa na Faida gani kukiwepo Serikali 3? Serikali ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar... Mwiba? Ninavyoelea mimi Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena, hata kukiwa na hizo Serikali 3 Chadema inazozitaka hakutokuwa na Faida yoyote ni kujizidishia Matatizo mengine. Hizo Serikali 2 za Muungano hakuna faida yoyote ile je itakuwa Tanzania kuwa na Serikali3? Tuwasikilize hawa Wa Zanzibar wanachokitaka kwanza ndio halafu tutazungumza kuwepo na Serikali 3 mkuu
Hawa wanaofanya chokochoko za muungano wangetakiwa kuwajibishwa ..
Hawa watu ni kina nani?..maana nijuavyo kila hatua ya Muungano wetu wamefanya mabadilisha Kikatiba kukidhi malalamishi mengi ya Wazanzibar, hadi imefikia leo kuna watu tena Wazanzibar wanauliza kwa nini yaliongezwa maswala ambayo hayakuwepo ktk Artical of Union!...Tutaweza vipi kuridhisha kila mtu wakati ilifanyika kwa ajili ya hawa hawa wanaolalamika. Mkuu wangu hakuna mwenye manung'uniko isipokuwa wachawi ambao hawakushiriki hata ktk Mapinduzi ya Zanzibar, ni kundi la watu wasiopenda hata kuunga Mapinduzi isipokuwa kwa kutambua uhuru wa Sultan..Na kama wangekuwa na uwezo basi wangeweza hata kuindoa hata serikali ya Mapinduzi na kurudisha Zanzibar ile waitakayo. Hata kina Smioth na Botha wanalalamika vile vile kuhusu Zimbabwe na South Africa lakini tunachoweza kuwaambia ni kwamba wakue (grow up) Dunia ile kukoloniwa na uhuru wa bandia imeshapita na haitarudi tena.Una maana gani? kwa muda gani unaweza kuwatawala watu uwalazimishe lile unalolitaka wewe? na utawawajibisha vizazi vyote? maana watu wenye manung'uniko na mfumo mzima wa muungano waliaza muda tu baada ya muungano!