CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

Wazenji wana Tabia za Uchoyo sana yaani chao ni chao Ardhi ya Wazenji ni ya wazenji tu lakini Ardhi ya watanganyika ni Ardhi ya wote Tambueni Kuwa wapemba wengi sana wanamiliki Ardhi huku Tanganyika na hawapati Vikwazo wakati wa kununua viwanja mashamba nk Lakini Mtu wa Bara akitaka kumiliki Ardhi Zenji inakuwa issue ! Watu wa Bara wanabaguliwa Zenji eti wamewabatiza majina wanawaita Vichogo au Chogo yaani Utazani wao wamesahau Kuwa pale walipelekwa Enzi ya Utumwa asili Yao ni huku huku Bara kwa kweli Wazenji wana Vituko sana Siku muungano Ukiwa marehemu watawakumbuka sana watanganyika Maana Mkoloni Mwarabu wanayetaka kumrejesha hataki vuvuzela atawanyoosha hadi wanyooke

Mie ni mbaara kabisaa, lakini nina miliki nyumba huko Zanzibar, hayo maneno mangine nani kakunywesha..?

Na hakuna Mzanzibar wala Mpemba ang'ang'aniaye ati Tanganyikwa, bali Wazanzibar wana madai yao ya muhimu na tatizo kubwa kabisa laanzia pale katika ule ati Muungano.


Ina maana jambo hilo hulifahamu ama watumia uburu wa jirani yako kutafakari mambo..?


Wakati mwangine jaribu kuketi pekeako na utafakari kwamba, hivi wanachodai Wazanzibar kina maana au ni wameamua tu..? Kisha picha hiyo ijenge upande wako kuwa weye ndo Mzanzibar na viongozi wako wamekutenda kiasi hicho, je, utapata muda wa kuleta maropoko kama hayo...?!!

Choyo wanacho wahodhio madaraka na wenye tamaa kama waliopo SIASANI.

Hapo namaanisha wale waililiao ati kukamata madaraka ilhaali uadilifu waishaanza uvunja hata kabla hawajapewa nchi.


Na weye jigeiye muda ili kutafakari mambo kwa faida ya kuonesha uendeaji wa mambo na si kufuata fuata kiushabiki.
 
Naunga mkono cuf.
Haya maneno ya huyu bini ni kujikomba.mungejua hawa ccm walivo wanafiki msinge isema cuf.
Hakuna watu walio kua hawana mwelekeo kama ccm znz.
Hivi mnajua kuwa wazanzibar walioko bara hawaruhusiwi kumuliki ardhi huko kwao znz?
Basi kwanza wangebadili katiba kuwaruhusu wa znz waishio bara kuwa na haki hio.
Ni ujinga tu kujipendekeza kwa bara ili walindwe kukaa madarakani na kupokezana na watoto wao hata kwa gharama ya kuuza nchi yao.
Hilo ajue halipiti anajifurahisha. Katiba ya zanzibar ishapigwa seal. Kuibadilisha inahitajika 2/3 ya kura hilo halipo. Si analipwa mshahara wake na tanganyika lazima atajikomba
 
Kimsingi ndugu zetu Watanganyika hapo hamupaswi kuwalaumu Wazanzibar, hili ni zao la msingi wa Muungano wetu, Zanzibar ipo, katiba take ipo na Wazanzibar wana hakki ya kuilinda na kuitetea popote walipo! Lakin pia Ardhi sio suala la Muungno kiuhalisia, ndio maana bado Zanzibar katiba yao huwapa fursa Wazanzibar kumiliki ardhi na katiba hiyo husimamiwa na SMZ, hovyi hapo Wazanzibar bado wapo kweny mstari sawiya!
Kwa upande wa Tanganyika kwa vile wamejivisha vazi la Muungano, ardhi ni mali ya Watanzania wote kwa vile katiba inamtambua raia kama Mtanzania, hivyo ndugu zetu musilalame wala musiwe na gere Al muhimu itafuteni Tanganyika yenu ije iwasimamie ardhi yenu sio kuleta maneno ya chuki na fitina kwa Wazanzibar walio Tanganyika, lolote mufanyalo kwao sio suluhisho la kudumu!

Hakuna anayewaonea Gere kwani 98% ya pato la Taifa lote linapatikana Tanganyika Ndio Maana hata wapemba wengi wamehamia bara kuisaka shilingi wabara wanataka Ardhi Zenji ili waje waamushe Mzunguko wa pesa wawape changamoto za maendeleo muache ulalamishi na kuchapa kazi
 
Kisiwa kidogo wabunge mawaziri utitiri yaani ni wengi sana huku wengine wakipata posho huku na huku Dodoma wapo na zenji wapo pesa ya kubembeleza muungano ni nyingi inatumika pasipo kero kumalizika Wabunge wa bara hawanusi baraza la wakilishi lakini wabunge wa zenji Dodoma kama kawa Watu million 1.5 wanawapelejesha watu million 45 kama nyumbu kwa kweli huu Muungano Tanganyika amechunwa sana hadi ngozi inakaribia Nyama ya utumbo

nakuhisi siasa yako, umejifunzia JF maana hata hujui muungano wetu unavyoendeshwa,
Serikali mbili maana yake, mambo ya Zanzibar ni kwa Wazanzibar ila mambo ya Tanganyika au hujiita Wabara ni ya Watanzania wote...!! sasa Mzanzibar sio Mtanzania...?
 
Bara hakuna cuf wala chadema wote wamekula maji ya kijani.....

basi inakuwaje mara kadhaa tumeona wabunge wa cuf wakiwakejeli cdm na wakati mwingine kujiunga na wa ccm? nao wanakuwa wamekula maji ya kijani? Utakuwa umekubali kuwa cuf ni cha wazanzibari kwa observation yako?
 
Bimani mwenyewe aliyetoa press conference huyo hapo kwenye picha. Mwangalie kwa makini halafu tuambie umegundua nini. Kazi kwako.

View attachment 143741
hapo mimi naona gaidi au mmwagia watu tindikali, au mwana uamsho.

inakuwaje zanzibar wamiliki ardhi bara na bara tusimiliki ardhi zanzibar? kwahiyo wazanzibari wawe na ardhi pande zote mbili na wabara tuwe na ardhi upande mmoja tu. tu nachojikomba kwao hasa nini hata kukubali kuendeshwa na na wazenji kiasi hiki? huu muungano una faida gani? nyie mnaokula posho dodoma tunaomba mjadiliane haya na mfikie muafaka, ama sivyo , serikali tatu ziwepo na muungano futilia mbali kule. na muungano ukivunjika, wazenji walioko hapa warudishwe kwao ndani ya mwezi mmmoja na wanyang'anywe haki ya kumiliki ardhi ili iliyopo hapa wanayomiliki waiuze au wanyang'anywe.
 
CUF ni sawa na jamvi la wageni, si chama tena bali ni genge la wahuni wachache waliolewa kahawa.
 
Hakuna anayewaonea Gere kwani 98% ya pato la Taifa lote linapatikana Tanganyika Ndio Maana hata wapemba wengi wamehamia bara kuisaka shilingi wabara wanataka Ardhi Zenji ili waje waamushe Mzunguko wa pesa wawape changamoto za maendeleo muache ulalamishi na kuchapa kazi

Sawa mkuu, ila kwa idadi ya Wazanzibar huwatendei hakki kulinganisha kiwango cha kodi na Watanganyika, ni kuishiwa kwa hoja!!
hapa nataka useme kwamba wapi Wazanzibar hawatendi hakki kulinda ardhi yao hali ya kuwa sio mali ya Muungano...? na hao Wapemba unaosema ww hawakujenga kwa magendo ispokua sheria imezingatiwa, sasa huo ni udhaifu wenu ama ndio ile janja yenu ya kutaka kuimeza Zanzibar inawatafuna, maana Wazanzibar kwa sasa hawatweza kuuza tena nchi yao
 
basi inakuwaje mara kadhaa tumeona wabunge wa cuf wakiwakejeli cdm na wakati mwingine kujiunga na wa ccm? nao wanakuwa wamekula maji ya kijani? Utakuwa umekubali kuwa cuf ni cha wazanzibari kwa observation yako?

Kwani wewe huoni huna masikio huku bara si kila suku ushindi wa kishindo? Na watatawala miaka mingi bafo. Watanganyika wamelazwa ndani ya muungano.
Chadema cuf nccr wote kwa bara hamna kitu.
Walipoulizwa mnataka vyama vingi znz walisema ndio na tanganyika walisema hapana.
Kwa hio ccm iko bara na cuf iko znz
 
CUF ni sawa na jamvi la wageni, si chama tena bali ni genge la wahuni wachache waliolewa kahawa.

Bora hawa walewao kahawa maana sasa imewachangamsha AKILI na wamejitambua na hawataki tena kurejea UPUUZINI kama ule wema waliofanza Baba zetu za kumkubali yule Nyerere na baadaye ttwataabika sie vizazi vyao.


Ila shida ni kwa wale walevi wa "MBEGE" na wanaowatumikia kama akina @ Yericko kijana cha msambila.


Dhihaka zenyu si muda matokeo mtajayapata, maana mlowadhaniya kuwa bado wangali usingizini sasa weshaamka.
 
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi

Mkuu, ukweli wenyewe ni kwamba hata kama Watanganyika wataruhususiwa naamini itakuwa kinadharia zaidi kuliko vitendo. Hivi kweli kwa udogo wa Zanzibar, Watanganyika wakatafute ardhi huko.
Lakini pia viongozi wenu waliotwa ardhi kubwa wathibitiwe.
Je jamaa zetu wa Zanzibar wenye ardhi bara tuwafanyeje? Chetu ni chetu na chao ni chetu lazima ifike mwisho.
 
Kiboko na kidume cha wanafiki wote vibaraka wa kuuza nchi yao.. Zanzibar kwanza muungano baadae

Kweli hii imesema mengi. Bila shaka ni mmoja wa wanaotaka Sultani arudi Zanzibar. Hajali maslahi ta wapemba wenye ardhi na vitega uchumi/biashara Tanganyika
 
Kweli hii imesema mengi. Bila shaka ni mmoja wa wanaotaka Sultani arudi Zanzibar. Hajali maslahi ta wapemba wenye ardhi na vitega uchumi/biashara Tanganyika

Sultani gsni? Huyu tulio naye wa tanganyika ametosha.
Zanzibaaaaaaaaaar
 
Nakumbuka kiwanja changu fuoni...yaani mpaka halmashauri nililipa na hati nikapewa na nikageukwa....
 
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi
Kwani kila anayetaka ardhi anapewa?? Si kuna taratibu?!, sisi tunataka kama mtanzania ambaye ni mtanganyika ameamua kuishi visiwani basi awe na uwezo wa kujenga kama vile mzanzibari anayeishi tanganyika anaweza kujenga na kuishi bila tabu. Au kama kwenye ardhi Zanzibar inajiona ni ndogo basi ifike mahali na kwenye mambo mengine ikubali udogo wake.

Sio kwenye ardhi Zanzibar ijione ndogo lakini tukija kwenye suala la serikali ya Muungano inataka nusu kwa nusu hiyo haiwezekani!! Mizani inayotumika ni lazima iwe sawa katika kila jambo sio huku sisi wadogo kule na sisi pia ni nchi tunataka usawa na Tanganyika, huu utakuwa ni uhuni!!!
 
Hivi watanganyika mna matatizo ya ardhi mpaka mupewe na ardhi ya zanzibar?sie wenyewe haitutoshi kaeni huko kwenu tanganyika mulime,zanzbr kwanza.
Suala sio matatizo suala ni kujenga umoja, ili watanganyika waone huu muungano kweli ni wa dhati basi wapewe haki ya kikatiba kumiliki ardhi zanzibar. Kumbuka hata ikitolewa hiyo haki, usidhani watanganyika ndiyo watakimbilia huko Zanzibar. Suala ni haki na usawa.
 
Back
Top Bottom