CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

Wanzanzibar acheni unafiki, Acheni ubinafsi na mtawafanya wanzanzibar walioko Bara wavamiwe na kunyanganywa mali zao. Kwanza mnatutesa sana ondokeni mtuachie nchi yetu. Na mkiingia Bara mnaingia na passport. Tumewalea sana. Mara tuwasomeshe bure, mara tuwaleteee maharagwe bure. kilakitu bure.:target:

Watanganyika tuache utoto na kujadili issues za msingi kwa jazba na mihemko! Zanzibar kuna ardhi gani ya kuwagawia hata wasiokua Wazanzibari?? Hizi ni deal za kitoto za watawala wanaohangaika kuhakikisha tunabakizs mfumo wa serikali mbili. Watanganyika tunadanganywa kwamba sasa tutaweza miliki ardhi Zanzibar!!

Nawaunga mkono CUF kwa kustukia na kuukataa huo utapeli wa siasa za CCM! Kwamba Watanganyika wenzangu hata kama huo utapeli utaingizwa ktk Katiba ni lazima Baraza la Wawakilishi Zanzibar walidhie sheria hiyo kutumika Zanzibar. Mzanzibari gani ataruhusu ujinga kama huo? Wanataka kusababisha vita ya ardhi huko Zanzibar?
 
unajua huu ni upuuzi viongozi kufikiri.changu tule wote,chako ufiche.muungano gani huu.Mungu ibariki Tanganyika!

Kwani lini Wazanzibari walidai ardhi ya Tanganyika? Kama mmewaachia basi ni nyinyi wenyewe. Si nyie mliotaka kuondolewa suala la kusafiria paspoti kutoka sehemu moja kwenda nyengine?
 
Mnataka kutugeuza kama Palestina ,yaani Waisrael walinunua ardhi za palestine baada ya muda wakawageukia na kuwafukuza wakisema ardhi yote ni ya WaTanganyika Wazanzibari hamna chenu ,kwa ufupi waTanzania wanauwezo kabisa wa kuinunua Zanzibar yote:yuck:
 
kwani lazima wapewe? Cha msingi katiba ya zanzibar imekosea kuendekeza huo ubaguzi wa wazi!

Kwani kuna kipengele chochote kinachosema Mtanganyika hana haki ya kumiliki ardhi? Natowa challenge aje mtu kuthibitisha hili kuwaq Mtanganyika katajwa kwenye katiba kuwa asimiliki ardhi Zanzibar.
 
wapemba wajiandae kuja kumiliki ardhi huko pemba na unguja! Tumechoka na huo unyanyasaji wenu kwa wabara walioko zanzibar!

Nguo ya kuazima haisitiri ma ta ko! Wazee walitwambia hayo na kwa kujua hilo nimekuwa nakataa kila siku kununua kiwanja Tanganyika ingawa nilishawishiwa sana!
Watanganyika wanawanyanyasa kwa maneno wahindi na Waarabu ambao wazee wao walizaliwa Tanganyika na hawana pengine pa kwenda.
 
Bimani mwenyewe aliyetoa press conference huyo hapo kwenye picha. Mwangalie kwa makini halafu tuambie umegundua nini. Kazi kwako.

View attachment 143741

Nilitanguliza kusema posti ya juu! Huu ndio mtindo wa Watanganyika iwapo huna ngozi nyeusi katu huitakuwa Mtanganyika, iko siko asili yako itakuponza. Yaoneni kama uongo!
 
Hizo ndio siasa za vibaraka wa ccm, ukiwa kibaraka ccm inakubidi ujitoe ufahamu kwanza, cuf hawajui kuwa wanaumiza ndugu zao wanaoishi bara.
Ukiwa na maana watutowe muhanga Wazanzibari tulio wengi kwa faida ya hao wachache? Wazanzibari tutamuunga mkono yeyote kwa hili la kumiliki ardhi.
 
Hapa nilipo kuna jirani yangu ambaye ni mzanzibar pure na anamiliki ardhi ya kutosha. Sasa huu uzi umenifungua macho kuwa kumbe ile ardhi inaweza kuwa yangu muda wowote,ni suala la muda tuuuu. Huyu jirani yangu alishawahi kumkatalia mtoto wangu wa mwanaume alipoenda kuchumbia kwake kwa kigezo cha kwamba suala la kuoleana si la muungano!!!!, kumbe hata ardhi nayo cyo suala la muungano!! Huyu jamaa atanikoma kwenye hili suala la ardhi lazima alikimbie jiji la sivyo akubali kijana wangu amuoe binti yake.

Endeleeni kuelewa kuwa "mtu kwao". Malizana nae kwani hayo ni yenu nani alimwambia kuwa mtu huacha asili yake!
 
Mkuu hapa swala ni utanzania,kama sheria ni kwamba ardhi siyo mali ya muungano mbona wazanzibar wanamiliki ardhi huku bara?
kama issue ni ukubwa wa ardhi kwa nini wanyarwanda wamarudishwa kwao kama waamihaji haramu?

Mtanganyika anaweza kumiliki ardhi Zanzibar mradi afuate taratibu. Unataka kuelewa taratibu?
 
muungano hauna maana kamwe na siku ipo wapemba na waunguja watakaa hapa bara kwa passport na mashamba yote watanyanganywa.
 
Ikija kwenye masuala ya kibaguzi kama haya wanasema "waasisi wa muungano" na yakija mambo serious "wanasema ulikuwa muungano wa Karume na Nyerere"

Tunapotumia hayom ya kibaguzi kama unavyoyaita tunawatumia waasisi kwa kukusudia Karume kwani hayo yote uyaitayo ya kibaguzi yaliwekwa na Karume na Nyerere akanyamaza kimya. Unahitajika kutafakari hilo!
 
Chama Cha Wananchi(CUF) kimepinga wazo na rai ya kupunguza masharti ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ili kulegeza nguvu zake kisheria na kuwapa fursa Watanzania Bara kumiliki ardhi Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo umetolewa na Mkurugenzi wa Habari na Mwasiliano ya Umma wa CUF Salum Bimani katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana visiwani humo, siku chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Muungano) Samia Suluhu Hassan, kushauri Katiba ya Zanzibar kuangaliwa upya na kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar.

Bimani alisema kuwa suala la ardhi siyo la Muungano tangu mkataba wa awali wenye orodha ya mambo ya Muungano na siyo sahihi kufanyika marekebisho ili kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar kwani ni ndogo na ndiyo sababu hata waasisi wa Muumgano waliamua ardhi hiyo imilikiwe na wazanzibari pekee. Chanzo mwananchi

Wazenji wana Tabia za Uchoyo sana yaani chao ni chao Ardhi ya Wazenji ni ya wazenji tu lakini Ardhi ya watanganyika ni Ardhi ya wote Tambueni Kuwa wapemba wengi sana wanamiliki Ardhi huku Tanganyika na hawapati Vikwazo wakati wa kununua viwanja mashamba nk Lakini Mtu wa Bara akitaka kumiliki Ardhi Zenji inakuwa issue ! Watu wa Bara wanabaguliwa Zenji eti wamewabatiza majina wanawaita Vichogo au Chogo yaani Utazani wao wamesahau Kuwa pale walipelekwa Enzi ya Utumwa asili Yao ni huku huku Bara kwa kweli Wazenji wana Vituko sana Siku muungano Ukiwa marehemu watawakumbuka sana watanganyika Maana Mkoloni Mwarabu wanayetaka kumrejesha hataki vuvuzela atawanyoosha hadi wanyooke
 
Chama Cha Wananchi(CUF) kimepinga wazo na rai ya kupunguza masharti ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ili kulegeza nguvu zake kisheria na kuwapa fursa Watanzania Bara kumiliki ardhi Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo umetolewa na Mkurugenzi wa Habari na Mwasiliano ya Umma wa CUF Salum Bimani katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana visiwani humo, siku chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Muungano) Samia Suluhu Hassan, kushauri Katiba ya Zanzibar kuangaliwa upya na kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar.

Bimani alisema kuwa suala la ardhi siyo la Muungano tangu mkataba wa awali wenye orodha ya mambo ya Muungano na siyo sahihi kufanyika marekebisho ili kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar kwani ni ndogo na ndiyo sababu hata waasisi wa Muumgano waliamua ardhi hiyo imilikiwe na wazanzibari pekee. Chanzo mwananchi

Kimsingi ndugu zetu Watanganyika hapo hamupaswi kuwalaumu Wazanzibar, hili ni zao la msingi wa Muungano wetu, Zanzibar ipo, katiba take ipo na Wazanzibar wana hakki ya kuilinda na kuitetea popote walipo! Lakin pia Ardhi sio suala la Muungno kiuhalisia, ndio maana bado Zanzibar katiba yao huwapa fursa Wazanzibar kumiliki ardhi na katiba hiyo husimamiwa na SMZ, hovyi hapo Wazanzibar bado wapo kweny mstari sawiya!
Kwa upande wa Tanganyika kwa vile wamejivisha vazi la Muungano, ardhi ni mali ya Watanzania wote kwa vile katiba inamtambua raia kama Mtanzania, hivyo ndugu zetu musilalame wala musiwe na gere Al muhimu itafuteni Tanganyika yenu ije iwasimamie ardhi yenu sio kuleta maneno ya chuki na fitina kwa Wazanzibar walio Tanganyika, lolote mufanyalo kwao sio suluhisho la kudumu!
 
Kwani kuna kipengele chochote kinachosema Mtanganyika hana haki ya kumiliki ardhi? Natowa challenge aje mtu kuthibitisha hili kuwaq Mtanganyika katajwa kwenye katiba kuwa asimiliki ardhi Zanzibar.
pole sana mkuu, naomba uhangaike na uitafute katiba ya zanzibar utaiona inasemaje kuhusu haki ya kumiliki ardhi ipo kwa nani! Huu ubaguzi hauvumiliki hata kidogo mkuu!
 
Kisiwa kidogo wabunge mawaziri utitiri yaani ni wengi sana huku wengine wakipata posho huku na huku Dodoma wapo na zenji wapo pesa ya kubembeleza muungano ni nyingi inatumika pasipo kero kumalizika Wabunge wa bara hawanusi baraza la wakilishi lakini wabunge wa zenji Dodoma kama kawa Watu million 1.5 wanawapelejesha watu million 45 kama nyumbu kwa kweli huu Muungano Tanganyika amechunwa sana hadi ngozi inakaribia Nyama ya utumbo
 
Mtanganyika anaweza kumiliki ardhi Zanzibar mradi afuate taratibu. Unataka kuelewa taratibu?
Mkuu hilo ni jema sana na ndivyo inavyotakiwa kuwa.kuna aliyeandika kwamba wabara milioni 2 wakija huko watapata wapi ardhi nilikuwa napingana na hilo,kama inaruhusiwa kumiliki ardhi ni vyema.
 
Mkuu hapa swala ni utanzania,kama sheria ni kwamba ardhi siyo mali ya muungano mbona wazanzibar wanamiliki ardhi huku bara?
kama issue ni ukubwa wa ardhi kwa nini wanyarwanda wamarudishwa kwao kama waamihaji haramu?

Bwana wee kwani nani anataka muungano?
Tuwe wakweli nyinyi watangsnyika ndio mmeshikilia
Wazanzibar wame resist zamani tangu enzi za karume jumbe salmin karume na hata sasa shein.
Wamepaza sauti zao. Mbara mtanganyika gani amefungwa kwa kuukataa muungano? Hakuna.
Lakini wapo wazanzibari wengi wamefungwa kuuliwa na kupoteza kazi zao kwa kukataa minyororo ya muungano.
Maadam nyie ndio mnao utaka basi tuyakuoeni na tutamiliki ardhi yenu na ya kwetu ngooo..na mabinti wetu ngoo.
Hatujawalazimisha
 
Back
Top Bottom