CUF waishambulia CHADEMA

Uko sahihi, CUF sio chama cha upinzani tena hivyo hakiwezi kuungana na Chadema, ukiangalia Ndugu Mrema wa TLP kwenye kampeni alikuwa anampigia kampeni JK, hivyo binafsi simwamini hata kidogo kuingia kambi ya upinzani kwani anaweza kuwa chanzo cha migogoro na kuturudisha nyuma zaidi. Ukiangalia pia NCCR Mageuzi pia hawaaminiki ukianzia na kukuru kakara za mwenyekiti wake wakati wa kampeni hata sasa juu ya Chadema na wabunge wake, hivyo ni bora Chadema kusimama kama wao ili kuepuka migororo ambayo ingetokana na wao kuungana na vyama vingine.

Naafikiri baadae tutawaelewa viongozi wa Chadema nini wanachokifanya sasa hivi.
 

Mkuu,
Nilikuwa nimeanza kupata wasiwasi kama kweli ni wewe ndio umeandika hii maneno manake inaonekana kiwango chake kiko chini sana kwa mtu kama wewe lakini nilipofika hapo kwenye red bold nikaamini kwamba ni wewe mwenyewe Bob.
Nadhani ukirudia hali yako ya kawaida utakuja na mawazo mazuri zaidi kuliko haya mkuu. CUF wana muafaka na CCM na hakuna anayejua nini kilichomo kwenye makubaliano yao. Kwahiyo sio suala la kuamka tu na kuunda umoja usioeleweka kwa kuwa tu chadema iwafurahishe CUF(CCM). NCCR, TLP na UDP wanajulikana wako upande gani sasa mkuu bado tu hulioni hilo? unataka tu chadema iungane nao ili ufurahi? hapana bana, hebu itendee haki chadema kwa hili japo kidogo.
 
Mkuu Mkandara...nakubaliana na ulichosema kwa 110% lakini validity yake nadhani imekuwa overtaken na time (or rather events).
Bond iliyopo kati ya CUF na CCM is just too strong to reverse. NCCR/TLP ndio hao, nao ni kama mouthpiece ya CCM.
Beats common sense how can Chadema fit into such chemistry without compromising their opposition stature.
 
Nadhani CUF inatumiwa na CCM ili kui-keep Busy CHADEMA huku CCM wakiwalaghai watanzania kua upinzani hauna lolote ila kulumbana tu kila siku. Huu ndio Mchezo unaochezwa sasa hivi. Ni Muhimu Chadema kuwa makini na CUF sana kwa sababu wako kwenye payrol ya CCM ili kuidhoofisha CHADEMA ambacho kimekua tishio kwa CCM.

Ni muhimu CHADEMA kutoa Msimamo wao wa Mwisho kuhusu hili swala na kuendelea mbele na shughuli yao ya kuwatumikia wananchi, Wasijisahau na kuingia katika Malumbano na CUF kwa sababu hawa wanafiki wako Kazini.

Kuhusu Kumkataa/Kumkubali JK, sijui kwanini CUF wanajiingiza katika hili wakati haliwahusu. inatakiwa awepo mtu wa kuwaambia CUF usoni kwamba hayawahusu na waache kuingilia mambo ambayo si ya kwao.

CUF should not interfere with how CHADEMA runs its affairs.Its none of their business, they should keep their comments and advices to themselves
:A S angry:
 
MBONA MNAVURUGA AKILI KAMA PUNGUWANI JAPO NAJUA ITS CONTRARY? KWANI CUF YA ZANZIBAR NA CUF YA BARA NI TOFAUTI? IWEKE IVI: kwani wajumbe (wabunge) wa Baraza la Uwakilishi visiwani, na wabunge wa hili la jamhuri ya muungano (bara & visiwani) wanaowakilisha CUF, ni CUF hiyo hiyo au kuna ya bara na visiwani? NI CHAMA KIMOJA CHENYE MRENGO/MWELEKEO MMOJA. SASA KAMA WAO VISIWANI NI WAMOJA NA CCM, itakuaje bara wawe tofauti....... KAMA HUIELEWI IYO KUMBUKA KUELIMIKA NI KULE KUBAKI MUELEWA BAADA YA KUSAHAU ULIYOFUNDISHWA SHULENI... Yule injinia (kingereza mbofu mbofu) aliegombea unaibu spika alijitoa amwachie CCM, ili akija kugombea uwakilishi SADEC CCM wampe kimahaba!!!! Sasa huo ni mwanzo tu... CUF si wapinzani tena, hamwelewi nini sasa? Sema wao ndo hawajielewi.... hau wanaelewa lakini wanataka watufanye hatwelewi... na sisi tunakaa tunawaskiliza....nafikiri ni ujinga mtupu huu....
 

hapo umenena mkuu
 

Sio Kwa ajili ya Zanzibar... Kwa ajili ya Pemba...
 
NITARUDIA KUSEMA TENA NA TENA CUF NI WANAFIKI WAKUBWA NA NI WAFITINI.
Nasema hivyo kwa sababu CUF wameunda serikali ya ummoja wa kitaifa na CCM Zanzibar bila kuwashirikisha TADEA, UPDP, JAHAZI ASILI, NRA na vyama vingine. Kama wao wanaona CHADEMA ni wabaguzi kwa kuto kuwashilikisha NCCR MAGEUZI, UDP, na TLP kuunda serikali ya upinzani Bungeni kwanini wao wasinge kataa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kushirikisha vyama vyote vya upinzani Zanzibar. Kuunda serikali ya ukweli wanashirikiana na chama kimoja (CCM) na kubagua wapinzani wengine, lakini kuunda serikali kivuli wanataka uwepo ushirikiano wa wapinzani wote si kuwa na chama kimoja (CHADEMA) mbona msimamo wao ni kwa serikali kivuli lakini kwa serikali halisi msimamo huo haupo?

Wanasema wapinzani wengine hawana wabunge au wajumbe wa baraza la wawakilishi ndio maana hawamo ktk serikali, si wangewateua hata wawili au mmoja kuwapa nafasi ya ujumbe wa baraza la wawakilishi na kumuingiza ktk serikali ya mapinduzi ili kuonyesha huo umoja wa kitaifa?

Ubaguzi wao umeanza toka ktk kujadili muafaka kwa kutoshirikisha vyama vingine, kama kweli wao si wabaguzi kwa nini ktk majadilianao ya muafaka walikuwa na CCM pekee na hawakuwashinikiza CCM kuwa na vyama vingine ili uwe muafaka wa Taifa la Zanzibar na si muafaka wa CCM na CUF. Inapofika sehemu kuna maslahi CUF wanataka kuwa peke yao na kuwatenga wenzao (mf serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar) hila linapofika swala hambalo halina maslahi ya kifedha (serikali kivuli ya muungano) CUF wanataka ushirikiano wa pamoja. Waache unafiki na ubaguzi wa ubara na upemba. kwanza wao ndio wabaguzi wakubwa kuliko CCM huko Zanzibar. KTK chaguzi wa mwaka huu wameibiwa ushindi wao lakini kwa kuwa wameahidiwa kuwemo serikalini wanacheka tu na kujifanya hawaoni wizi uliofanyika. waache CHADEMA waendeshe mapambano yao kwa kutumia mikakati yao na wao waendelee na uswahiba na CCM.

Mwaka 1995 walipokuwa wengi bungeni waligoma kuunda serikali kuvuli ya pamoja na NCCR leo wanajifanya wamesahau na kuwakumbatia NCCR ili wajue ni wanzao. kupoteza nafasi ya kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania kinawauma sana na wataumia sana hadi ifike 2015 watateseka kweli mioyoni mwao
 
Wakuu zangu,
yawezekana kweli bado sijaamka lakini yanitisha sana kuona huu muafaka baina ya CUF na CCM umekuwa kidonda kikubwa cha Upinzani hasa tukizingatia kwamba CUF wameyafanya yote haya kwa faida ya Wazanzibar. Labda tunachoshindwa kuelewa ni kwamba bado tupo ktk mfumo wa chama kimoja na CCM ndiye anaamua kila kitu kulingana na mustakabali wa Taifa letu kama wanavyoliangalia wao.

Ikumbukwe tu kwamba Muafaka baina ya CUF na CCM umefanyika wakati bunge letu lipo na hakuna chama wala kiongozi yeyote wa Upinzani aliyesimama na kupinga Muafaka huo kulingana na sheria. Kama kweli Upinzani upo nadhani la muhimu ilikuwa kupinga muafaka huo kwanza kisheria kwani binafsi ingawa sii mwanasheria lakini nadhani CCM na CUF walipindisha sheria kuunda muundo mpya wa serikali ya Zanzibar kinyume cha katiba hivyo kuwanyima fursa hiyo vyama vingine kushiriki kikamilifu, kiasi kwamba vyama vingine havitakuwa na nafasi ya kuunda serikali isipokuwa CCM na CUF au kutakuwepo na aina mbili ya serikali ile ya kikatiba na hiyo ya CCM na CUF..

Kwa hiyo, nachozungumzia mimi ni Upinzani ktk serikali ya Muungano na laukama CUF wameungana na CCM na mnaamini kwamba wameungana kutokana na muafaka ulofanyika Zanzibar basi nadhani ipo kila sababu kupinga muafaka huu kisheria kwanza kuliko kuweka madai haya na kuyapa uhalali. Kama kweli hii ndio sababu iliyotangulia kwa nini Chadema waliwafuata CUF na kutaka kuunda Upinzani nao hali wakijua kwamba CUF ameungana na CCM? kwa nini Chadema wasiwafuate vyama vingine badala ya CUF na kama wote hawa hawaaminiki Chadema anapungukiwa kipi ikiwa ushirikiano wenyewe ni wa bungeni tu...

Sasa labda nizungumzie Political strategic hateful attitudes...
Kwanza niwape mfano wa kimaisha ili mpate kunifahamu vizuri where do I come from..na mifano yangu ni ile ile asoipenda Mwanakijiji..

CCM na CUF wameklubaliana Unyumba pasipo ndoa na CUF kama mwanamke malaya ametaka unyumba na Chadema lakini Chadema hawataki kwa sababu CUF kawekwa kinyumba na CCM ili apate kujengewa nyumba yake huko Unguja. Lakini kuwepo sababu hizo Chadema hawataki tena mahusiano na CUF pamoja na kwamba Chadema wanajua sababu ya CUF kukaa na CCM hivyo kuhofia matokeo ya relation baina yao.

Sasa mimi nasema hivi huu ni wivu wa kijinga ikiwa Chadema anafahamu fika kwamba CUF anafanya umalaya wa kisiasa ili afanikishe sera zake ndani ya utawala wa CCM. Na maadam mbaya wa Chadema ni CCM strategically Chadema anatakiwa kumuumiza CCM kwa kila nafasi anayopata na moja wapo ni hii ya kushirikiana na CUF na vimada wake wote ktk baadhi ya maswala. Nikirudi ktk mfano wangu pale juu, mtu yeyote mwenye mahusiano na ametumia fedha na muda wake kumjenga, akisikia kuna mhuni anapiga kwa pembeni pasipo gharama itamuuma zaidi na pengine kuwa na wasiwasi zaidi na mahusiano baina yao.

Kwa maana hiyo Chadema kama chama wanatakiwa kuwa na mbinu za kuwaangusha CCM na mojawapo ni kuendelea ushirikiano na CUF pale inapohitajika kukidhi haja za Chadema kama ilivyokuwa toka mwanzo. CCM wanajulikana ni mafisadi tena ktk hili ndio kabisa wamemchukua mke wa mtu na kumweka kinyumba..Chadema wasifanye hasira kama kweli mufaka huo ndio unawauma zaidi basi wafikishe mashataka yao mahakamani ili kupata sheria. Lakini tunapoendelea kudai kwamba CUF nbdio walikuwa hawataki ushirikiano hali Chadema ndio tumewapa nafasi hiyo kwa masharti nadhani ni bora tuwe wakweli. Tukubali kwamba Chadema imekataa ushirikiano na CUF kwa sababu CUF imetaka vyama vingine vishirikishwe lakini hili halikubaliki na Chadema na kwa sababu zifuatazo.

Again, nashindwa kuelewa kwa nini tuwakaribishe CUF ktk ushirikiano na tuwaache wengine hali CUF amekaa vibaya zaidi ya NCCR -Mageuzi au TLP ukichukulia muafaka uliopo baina ya CUF na CCM. Wakuu zangu sintapenda kuendelea na ubishi huu lakini utetezi wa wana Chadema hauna mantiki hata kidogo ikiwa Chadema waliwafuata CUF kisha leo tunasema hatuwataki CUF kwa sababu ya ushirika wake na CCM...Je, Chadema hawakuona ubaya wa mahusiano hayo toka mwanzo kabla hawajawafuata CUF?

Nazidi kuwaumiza vichwa!
 
Hivi tuongeze ukweli upi zaidi ya huu? Thanks William. Be Blessed a million times.
 
Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post
Have you seen post number 3 Mh. Acid? It is so clear that Chadema will never surrender to CUF.
Kama wanadhani bado wao wanaweza kuunda kambi yao waendelee tu lakini wajue haina nguvu kwa namna yoyote ile. Wataishia kuwa wanahama viti siku Chadema waki boycott hotuba za Kikwete! No way!
 
Nilikuwa nalisoma mtandaoni lakini nimeliondoa hata kwenye cookies zangu! Silitaki kabisa kama nisivyotaka Uhuru na magazeti yote ya Rostam.
 
Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post

I secondyou mkuu!! Ni wakati wa kuwa careful na kila move!! Thanks mkuu!!:smile-big:
 
Kikwete na sera ya udini
Hivi leo nimesikia kikwete anasema kuna udini mkubwa sana hapa Tanzania na akaongea kwa msisitizo kabisa,guys is it true?
 
Acid, Hivi kweli unafikiri kwa hali ya kawaida, CHADEMA wanaweza kuungana na CUF ambao wameungana na CCM? Japo CHADEMA waliextend hiyo invitation, do you realy think it can work. Kwamba CHADEMA wa team up na Mapandikizi ya CCM na washirika wakuu CCM (CUF)? How do you real expect CHADEMA to share political secrets and strategies without feeling vulnerable. Well they are aloneand have kept their doors open. Ndo wameanza let's wait and see what will become of the opposition in the paliament.
 
Hapo ndo inajulikana kuna upinzania au kuna kutafuta sifa na vyeo thanks kwa wachangiaji kama @Nikupateje. Hawa cuf ndo Bure bureshi hamna kitu kabisaa wacha wabwabwaje maana hawana jipya kwishinei hoja zao zimemezwa sasa wanakimbilia kushabulia upande wao!!!
 
Eti CHADEMA WAMEWAKWAZA MBATIA NA LIMBUKA HIVYO INABIDI WAENDE WAKAONGEE NAO NY.................O!! KWA LIPI HASA LA KUWABEMBELEZA NYIE WAPINZANI FAKE? KWANZA YA NINI KUPOTEZA MUDA WA BURE WAKATI CUF NI CCM NA IKO SERIKALINI TAYARI TENA SERIKALI HARAMU NA BANDIA ISIYOCHAGULIWA NA WANANCHI SASA WATAKUWAJE WAPINZANI WA KWELI? MBOWE ALICHOFANYA NI KUONDOA LAWAMA NDIO AKAMWITA HUYO ASIYEJUA KUTUNZA SIRI CHEMBA NA SIYO KAMA HAMAD ANAVYOTAFSIRI KUWA CHADEMA HAWANA UWEZO WA KUJIONGOZA BILA WAPINZANI WENGIE, HAHAHAHAHAHAHAH LOOOOOOOOO HUYO MPINZANI NANIIIIII...MREMAAA, MBATIAAAA, CUF WANAOKULA KUKU SAIVI NA MAFISADIII.. TUACHE UNAFIKI JAMANI CHADEMA NDIO CHAMA CHA WANANCHI NA NDIO WAPINZANI WA KWELI BUNGENI..CHADEMA MMOJA NI KAMA ELFU MOJA HAHAHAHAHAHA
 

Hivi ni Malecela kweli kaandika haya? Nashangaa. Congrats!!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…