CUF sasa dhahiri mambo ni magumu

CUF sasa dhahiri mambo ni magumu

Uliwekwa uzi hapa kuhusu hili mkadai ni uzishi, haya sasa!! Watano kati ya tisa wamekataa kikao hicho cha zanzibar na hawamtaki Seif.

Si kweli, kati ya wale watano, ni wawili tu ndio wajumbe halali wengine ni feki...unless unatulazimisha tuamini unavyotaka!!
 
Ningeshangaa profesa kung'olewa kirahisi namna hiyo kwenye chama alichokipigania kwa muda mrefu.
 
Hapa naona magoli yanazidi kuhamishwa na tunasahau key subject yetu ni utenguzi wa barua ya kujiuzulu kwa prof. Mengine haya tunajadili mbwembwe tu.
 
Ningeshangaa profesa kung'olewa kirahisi namna hiyo kwenye chama alichokipigania kwa muda mrefu.
Mbona alikimbia kipindi cha kampeni? Lipumba hana Uchungu na CUF bali pesa za ccm ndizo zinamtoa fahamu na siku ccm wakisitisha kumpatia pesa lazima atasepa na kuwa kimya.
 
Kaf ina hali mbaya sana, ndugu wa upande wa pili hawatapona kwani hakuna Ukawa nje ya Kafu.
Nakama Ukawa ukifa itakuwa mbaya sana kwani tumeshuudia Ukuta ukuanguka wenyewe.
 
Ili use mdhamini inatakiwa iweje? Nilidhani unatakiwa kuwa na akunti iliyonona
 
Mimi namshabikia lipumba kwa sababu anatoka bara tu, huyo maalim itachukua muda sana kumkubali
 
Pesa ya serikali kuhamia Dodoma imekuwa shida, pesa za misaada kwa waathirika bukoba walichangisha watu lakini pesa za kumpatia lipumba avuruge ukawa ipo ya kutosha
Una evidence yoyote inayoonyesha serikali ilimpatia fedha lipumba ili avuruge Ukawa? Nahisi ubongo wako umejaa Ushuzi, acha kufikiri kwa kutumia Ushuzi
 
Mbona alikimbia kipindi cha kampeni? Lipumba hana Uchungu na CUF bali pesa za ccm ndizo zinamtoa fahamu na siku ccm wakisitisha kumpatia pesa lazima atasepa na kuwa kimya.
Alikimbia sababu Maalim alimzunguka akalamba pesa ndefu kwa lowasa, kwani hulijui hilo Mnyoo?
 
Wajumbe wa bodi ya wadhamini toka Bara wameonyesha kutokubaliana kabisa na msimamo wa upande wa pili unaopingana na Mwenyekiti wa CUF, Prof Lipumba.

Kulingana na habari za ITV saa mbili, mtanange unaoonyesha kuwa Bodi ya wadhamini imegawanyika kabisa, huku wajumbe toka bara wakisema mambo kutoka kwa Maalim, enough is enough.

Upande unaolalamikiwa kwa ukiukwaji wa taratibu ndani ya chama cha CUF, ni ule unaoongozwa na Maalim Seif. Mjumbe mmoja ameenda mbali zaidi na kudai tatizo ni usultani wa Katibu wa chama Maalim Seif.

Mjumbe huyo amedai Maalim amekuwa akijilimbikizia madaraka na hatimae kuwafukuza wanachama waanzilishi kama James Mapalala, Mzee Mloo na hata Hamad Rashid.

Mjumbe huyo akimfananisha Maalim na Napoleon aliyeshinda vita nyingi na hatimaye kuzidiwa nguvu katika mji wa Waterloo huko Ulaya, mjumbe huyo kasema Maalim sasa kafika Waterloo yake. Hapa ndo kafika.

Mjumbe mwingine amesema vikao vilivyoitishwa kinyemela huko Zanzibar bila kushirikisha wajumbe toka Bara ni ukiukaji mkubwa wa taratibu za chama.

Sinema inaendelea.
Hivi tuseme haya yote walikuwa hawayafahamu??? na walichukua hatua gani. Wazee wetu wametuachia methali nyingi tu na moja wapo ni MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO 'SPARE THE ROD AND SPOIL THE CHILD
 
Njaa na unafiki unakiangamiza chama cha CUF.

Kama una mtu mmoja, angalau mwanasiasa yeyote wa nchi hii ambaye hana njaa na pia si mnafiki naomba umtaje, mmoja tu halafu tuone kama vyama vingine vitapona!
 
Mimi namshabikia lipumba kwa sababu anatoka bara tu, huyo maalim itachukua muda sana kumkubali
Mwalimu alisema mtu akianza ubaguzi tu, itammaliza na hataishia kubagua mtu mmoja.
Rekodi ya Maalim inajieleza, na inammaliza
 
Mwalimu alisema mtu akianza ubaguzi tu, itammaliza na hataishia kubagua mtu mmoja.
Rekodi ya Maalim inajieleza, na inammaliza
Wewe ubaguzi umekumaliza? CCM damudamu mna shida sana. CCM katika nchi hii ndio wabaguzi. Wanaiba chaguzi na kupindua matokeo ya uchaguzi. Au huo sio ubaguzi? Kwa nini CCM inajihisi na kujiona ina hati miliki ya kuitawala nchi hii? Au huo sio ubaguzi?
 
Mm sijaelewa kwamba maalim ndio tatizo lakini tuambieni kama lipumba alijihudhuru au alienda likizo, mm hapo tatizo la maalim kwani hawezi kumfukuza mwenyekiti, kweli bara huku hakuna upinzani wa kweli na msimamo hakuna!
 
Uliwekwa uzi hapa kuhusu hili mkadai ni uzishi, haya sasa!! Watano kati ya tisa wamekataa kikao hicho cha zanzibar na hawamtaki Seif.
mkuu hata kama wote wange mpinga seif, bado inge halalisha marejeo ya lipumba!!!!!,.....hili linaeleweka kwa tu kwa mzee Ibra na baadhi ya wana ccm tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom