Nimewatazama wale wajumbe wa bodi kupitia ITV, nimewasikiliza pia. Nilichojifunza ni kwamba hivi vyama vya siasa, kwa baadhi ya watu vimegeuka kuwa "vyombo vya kuendeshea" maisha yao. Wale wajumbe, pengine kwa kuelekezwa, wanaugeuza mgogoro uliopo CUF sasa kuwa baina ya CUF bara na CUF Zanzibar. Na ili kunogesha wanamwonyesha Seif kuwa ndiye tatizo. Taasisi zinazoua vyama vya upinzani vinavyosumbua chama tawala huelekeza mashambulizi kwa viongozi BOLD kama ilivyo kwa Seif. Wale wazee kudhihirisha kuwa wanatumika sasa kukimaliza chama, wametumia jukwaa lile kumshambulia Seif tena kwa kutumia hoja zisizoendana na mgogoro uliopo CUF sasa. Kwa hali ilivyo, hawa wazee kama akina Lugeye ndio watatumika kuimaliza kabisa CUF iwe sawa na TLP ya Mrema, UDP ya Cheyo, kile cha Dovutwa; na the like. Sioni kama kuna namna CUF itajinasua katika mbinu hizi za kutumia watu waliochoka!