Kweli inasikitisha. sasa hivi Wapemba wanayimwa kujiandikisha kupiga kura ili CCM wayachukue majimbo yao 2010 viongozi wao wako huku Bara wanatumikia agenda za RA dhidi ya maadui zake.
Profesa, tulikuamini sana, achana na hao akina Jussa na Maalim, pigania haki ya wazalendo hapa wanaoibiwa fedha zao kila siku na majambazi ya CCM. Achana kuikandia Chadema kwa agizo la RA, ungana na Chadema katika kuutokomeza ufisadi ndani ya CCM kwa lengo la kuleta utawala bora. Achana na tamaa ya pesa za wizi, pigania haki ya wazalendo hata bila malipo, kwani siasa za kweli ni kujitolea.
Kama kweli una uchungu wa nchi hii, adui yako inapasa awe CCM, na siyo Chadema. Unapotea sana. Utakimbiwa na wengi.
Mwiba,TATIZO HATA PICHA ZA UFUNGUZI WA ZINDUKA MNASHINDWA KUTULETEA ,poleni sana.
Kivipi mbona unataka kukwepa hoja nakuingiza udini?? labda wewe ndiyo umeanza udini??
Lipumba anaongelea mafisadi wote either wako chadema, wako CCM it doesn't matter?? ,Masikio yangu yako huru nasubiria kusikia chadema wakijibu hizo tuhuma kwa faida ya nchi!!
Lipumba kesha katiwa , anaonyesha yale madai ya watanzania kwamba CUF kuna udini mie naongezea anasimama kumtetea Rostam kwa mshiko na kwa kuwa wote wanatoka Tabora .Mtu mwenye heshima na akili timamu hata ndani ya CCM they will never stand for Rostam trust me and at least not in the open like this .Lipumba kweli pumba .Kesha jua CIF imekufa visiwani sasa anaisaidia CCM bara .
Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema).
Ataka TAKUKURU nyingine iundwe kuchunguza iliyopo
Habel Chidawali,Dodoma
MBUNGE wa Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema), ambaye ni maarufu kwa kuanika uovu, jana aliulipua mradi mkubwa wa kusambaza maji kwa wananchi wanaoishi kwenye miji ya Shinyanga na Kahama uliogharimu takriban Sh252 bilioni za walipakodi, akidai kuwa una harufu ya ufisadi.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana akiwa mchangiaji wa tatu katika hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa mwaka wa fedha 2009/10.
Alidai kigogo mmoja wa Mamlaka ya Maji safi na Majitaka wa Shinyanga kuwa alifanya ufisadi mkubwa, akishinikiza wenzake wakubali kupitisha fedha ambazo haziko katika utaratibu mzuri huku akionekana kuwekewa ulinzi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Dk Slaa alisema katika mradi, ambao unatoka ndani ya mradi mkubwa wa Ziwa Victoria, ameingia mdudu anayeonekana wazi, lakini wahusika hawaonyeshi kasi katika namna ya kumshughulikia.
"Ni lazima iundwe Takukuru nyingine kwa ajili ya kuichunguza Takukuru iliyopo hivi sasa, kwani inaonekana kuwa imeshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake na inaingilia kazi ambazo zinaonekana wazi kuwa ni sehemu ya rushwa," alisema.
Aliitaka serikali iunde taasisi nyingine ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kwa ajili ya kuichunguza Takukuru iliyoko hivi sasa.
Alisema sababu za kutaka kuundwa kwa taasisi hiyo mpya ni kutokana na kile alichokieleza kuwa, Takukuru imeshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake.
Akiongea kwa hisia kali, siku moja baada ya Spika Samuel Sitta kuruhusu watu kuonyesha hisia zao, mbunge huyo ambaye ni katibu mkuu wa Chadema, alizungumza huku akionyesha baadhi ya vielelezo vyake.
Alisema: "Tarehe 13 Machi mwaka huu, kigogo huyo alikwenda katika Hoteli ya Karena na kuongea na mkurugenzi wa Trans Ocean Supply Ltd na kukubaliana mambo ambayo ni wazi yanaonyesha kuwa kuna mianya ya kifisadi.
"Kama haitoshi siku iliyofuata alikwenda tena mkurugenzi huyo na kumchukua mgeni wake bila ya kujua walikuwa wanazungumza kitu gani, lakini kwa kutumia gari la serikali aina ya (Toyota)Prado namba STJ 6463 alimbeba na kumpeleka kwenye Uwanja wa Ndege wa Shinyanga."
Dk Slaa alifafanua kuwa siku chache baada ya kuondoka kwa mkurugenzi wa Trans Ocean Supply Ltd, Gulam aliwaita wenzake na kuwaeleza kuwa alikuwa na maagizo kutoka kwa wakubwa ili aweze kununua vifaa vya kufunga mitambo ya maji katika miji ya Shinyanga na Kahama.
Kwa mujibu wa Dk Slaa, mkurugenzi huyo alikataliwa na mkurugenzi wa fedha wa Shinyanga kwamba asingeweza kutoa fedha zozote kwa ajili ya manunuzi ambayo yalikuwa nje ya utaratibu, lakini alilazimishwa na kutishwa ili akubali kuidhinisha kiasi cha Sh 2.1 bilioni ambazo tayari zilikuwa zikidaiwa.
Mbunge huyo alifafanua zaidi kuwa, baadhi ya viongozi waliendelea kumtishia mkurugenzi wa fedha na hata kiasi cha kumwandikia barua ya kumsimamisha kazi huku Takukuru ikiingilia kati kwa kuwasaidia baadhi ya watu ili wambane mkurugenzi huyo wa fedha ambaye aliendelea kuweka msimamo na kugoma.
Aliongeza kuwa, mkurugenzi wa maji aliamua kutembeza karatasi kwa ajili ya kuwasainisha wajumbe wa bodi kwenye nyumba zao ili waidhinishe fedha hizo bila ya kufuata maoni ya mkurugenzi wa fedha.
Alisema wakati huo tayari mita 4,000 za maji zilishafika katika eneo hilo bila ya kujua tenda hiyo ilikuwa imepitishwa na nani na kwa muda gani.
Maelezo ya Dk Slaa yalisema kuwa, kutokana na msimamo wa mkurugenzi huyo, alipelekewa fedha katika bahasha na alipokana, aliitiwa watu wa Takukuru ambao walimchunguza na bila kupata kitu chochote, lakini waliendelea kumfuatilia bila ya kujua sababu zipi ziliwafanya wamfuatilie.
Pamoja na kuihusisha Takukuru katika masuala ya rushwa, Dk Slaa aliijia juu Wizara ya Maji na Umwagiliaji ambayo alisema imeonyesha udhaifu katika mradi huo baada ya kutumia fedha nyingi huku ikitambua kuwa bado kuna matatizo makubwa katika eneo hilo.
Alisema kuwa, taasisi hiyo haikutenda haki katika jambo hili kutokana na kuhusika moja kwa moja katika masuala mazima ya kushughulikia jambo hilo kwa kuwa iliwaacha wahusika kamili na kumfuata mtu mwingine tena kwa vitisho.
Alisema tayari ameshamfikishia Waziri wa Maji na Umwagiliaji taarifa zote na orodha ndefu ya majina ili aweze kushughulikia, vinginevyo hakuna haki inayotendeka kwa watumishi wenye misimamo ya kweli ndani ya wizara hiyo.
Kwa upande wa Maji, Dk Slaa aliibebesha lawama kwa kusema ilitumia kiasi cha Sh 700 milioni katika mradi huo huku itambua kuwa kuna tatizo kubwa katika mgogoro wa uendeshaji shughuli zake na kwamba, fedha hizo hazikutumika ipasavyo.
Dk Slaa alisema Sh700 milioni zingeweza kutosha kugharamia mradi mzima wa kusambaza maji katika miji ya Shinyanga na Kahama na kwamba kuidhinisha Sh2 bilioni ni sehemu ya ufisadi mkubwa usio na huruma kwa wananchi wa Tanzania. Katika hotuba ya makadirio ya matumizi, wizara hiyo iliomba Bunge lipitishe jumla ya Sh 264,933,617,000 ili ziweze kutumiwa katika miradi mbalimbali.
http://www.mwananchi.co.tz
LUNYUNGU.
Maneno ya Mkandara unayakumbuka?kuwa wapinzani wasigombee ukoko.
Edwin Mtei hakuacha kazi 1974 ni mbele ya mwaka huo cheki details zako.Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.
Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.
Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?
Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?
Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.
Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.
Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors
Yaani jamaa u-Profesa wake anaudhalilisha si kidogo. Maana hii ni wazi kabisa kuwa katumwa na RA kubomoa upinzani. Na hajui kuwa watu sasa wamechoka ni hizi porojo tu za kurushiana maneno bali wanataka mikakati hasa ya kulinusuru taifa kutoka kwenye lindi la umaskini ikiwemo kudhibiti wizi wa rasilimali za taifa na si hizo porojo za maneno. Arudi akajipange upya maana bara hakuendeshwi kwa jazba za chuki dhiki ya mtu fulani tu.
Maproffesa wengi wa Tanzania wengi wao walisoma sana kwa kukalili na kupasi mitihani yao na kupata A+ lakini kwenye practical ni F+. Enzi zile za ujamaa Mtu kama Proffesa alieshimika sana kwamba anajua mambo kumbe ni kwa sababu hapakuwa na utandawazi wa kuwagundua ubovu wao, leo hii mtu akisema kitu kama ni pumba unajua tu huyu mtu kachemsha, ni kama huyu anayejiita Prof Lipumba. Huyu jamaa atakufa kabla ya umri wake, maana alijua akiwa prof maisha yakuwa mazuri, kumbe yamekuwa kinyume chake, angalia sasa anavyopewa visenti kidogo tu na kuanza kupayuka utafiri mtu ambaye hata darasa la kwanza hakupita. Rostamu alisema Mengi ni Nyangumi, leo prof kasema tena Mengi ni nyangumi, jee hii imekaaje!!. Prof katetea turbine za Dowan/Rostamu zinunuliwe huku akijua wazi ni hiyo fraud. Jee watu kama hawa kweli hata akikufundisha utabaki kukalilishwa vitabu vya mwaka 47, mwisho wa yote kwenye practical life unakuwa kama ujaenda shule.
Ndo maana wasomi wengi Tanzania akisoma mpaka apate ajira, maana wanafundishwa kuajiiwa wakati huo, India, US, UK, JAPAN etc wanafundishwa kujiajili. Utakuta mtu na masters Degree au degree mojae anaajiliwa na mhindi wa darasa la saba hapo Dar. hiyo yote ni kwa sababu ya kufundishwa na hawa Maprof uchwara.
Edwin Mtei hakuacha kazi 1974 ni mbele ya mwaka huo cheki details zako.
Maproffesa wengi wa Tanzania wengi wao walisoma sana kwa kukalili na kupasi mitihani yao na kupata A+ lakini kwenye practical ni F+. Enzi zile za ujamaa Mtu kama Proffesa alieshimika sana kwamba anajua mambo kumbe ni kwa sababu hapakuwa na utandawazi wa kuwagundua ubovu wao, leo hii mtu akisema kitu kama ni pumba unajua tu huyu mtu kachemsha, ni kama huyu anayejiita Prof Lipumba. Huyu jamaa atakufa kabla ya umri wake, maana alijua akiwa prof maisha yakuwa mazuri, kumbe yamekuwa kinyume chake, angalia sasa anavyopewa visenti kidogo tu na kuanza kupayuka utafiri mtu ambaye hata darasa la kwanza hakupita. Rostamu alisema Mengi ni Nyangumi, leo prof kasema tena Mengi ni nyangumi, jee hii imekaaje!!. Prof katetea turbine za Dowan/Rostamu zinunuliwe huku akijua wazi ni hiyo fraud. Jee watu kama hawa kweli hata akikufundisha utabaki kukalilishwa vitabu vya mwaka 47, mwisho wa yote kwenye practical life unakuwa kama ujaenda shule.
Ndo maana wasomi wengi Tanzania akisoma mpaka apate ajira, maana wanafundishwa kuajiiwa wakati huo, India, US, UK, JAPAN etc wanafundishwa kujiajili. Utakuta mtu na masters Degree au degree mojae anaajiliwa na mhindi wa darasa la saba hapo Dar. hiyo yote ni kwa sababu ya kufundishwa na hawa Maprof uchwara.