CUF na Operesheni "Zinduka"

Kweli hata mimi nashangaa sana kusikia maneno kama haya, Hata hiyo operation Zinduka ni kuiga tu kwa CHADEMa ambao walianza muda mwingi, kwanza aje na kuomba samahani kwa Watanzani kwa kupoteza kodi za wananchi Watanzania na pia muda kwa ajili ya mwafaka na pia nyinyi Ndugu zangu mtaona wenyewe baada ya uchaguzi wataanzisha MWafaka 5 na 6 na 7 ni ulaji hakuna jipya juu ya CUF bara, Walipoteza hata jimbo la TEMEKE, Bukoba na kule maswa sijui, Maana inatia shaka msimamo wa huyu jamaa au ndio kwa ajili wanatoka sehemu moja na wakina RA?? CUF mkitaka kupata watu acha kuwasema CHADEMA na Pia Lipumba ni mmoja wa JF aje kusoma humo ndani alama za nyakati juu ya hilo
Wacha wakanyagane maana vizuri ili tupate viongozi wazuri...wasipolumbana tutatoa CCM (mafisadi) tutaingiza "Nyangumi" bora ipi??? for the sake of national interest wacha walumbane tena afadhali wameanza mapema kabla ya uchaguzi .....
 
Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.

Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.

Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?

Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?

Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.

Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.

Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors
 
Wacha wakanyagane maana vizuri ili tupate viongozi wazuri...wasipolumbana tutatoa CCM (mafisadi) tutaingiza "Nyangumi" bora ipi??? for the sake of national interest wacha walumbane tena afadhali wameanza mapema kabla ya uchaguzi .....
Kuna mahali umeulizwa nani kakutuma. Hivi umejibu?
 
Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.

Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.

Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?

Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?

Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.

Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.

Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors
Ni kweli sasa ana maji taka na pia itakuwa shida sana, Labda baada ya kuona kuwa CHADEMA wanapewa support kubwa sana. Mbona yeye huwa anabaki kuongea tu, Sioni sababu yoyote ile ya Kusema juu ya CHADEMa, inabidi waseme kwanini wanafanya vibaya wakati wa uchaguzi wa majimbo mbalimbali hapa Tanzania??
 
Hii ni habari njema kwa Chadema na ni bahati nzuri ilioje CUF kujitokeza wakati huu kwa sura zao halisi. Niliwahi kusema viko vyama vitajimaliza vyenyewe na ndio hali hiyo tunaishuhudia hivi sasa kwa NCCR, TLP na sasa CUF. Mwaka 2010 tunahitaji vyama viwili vichuane - Chadema na CCM !

CUF walipokubali kuingizwa mjini na CCM kwa kilichodaiwa ni muafaka, hata kipofu angetabiri mwisho wake. Utakubalije kupatanishwa au kuwa na muafaka na mwizi kama kweli unachukia wizi. Utapatanishwaje na zimwi lisiloheshimu sheria, linalohujumu haki na linalosigina katiba - wapi na wapi ?
 
Nimejibu kwamba nimetumwa na aliyekutuma!! wewe

Wakuonea huruma kwenye huu ulimbukeni wa CUF ni wapemba.... maskini ona hata wengine walipigwa risasi kama swala kwa kuwaamini viongozi wao... wakitegemea kuwa wana dhamira ya dhati ya kuwakomboa.... kumbe wenzao wanakula hela za mafisadi kina Rostam ... na wanachofanya ni igizo.... ukombozi wa wapemba watausikia kwenye bomba tu....
 
Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.

Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.

Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?

Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?

Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.

Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.

Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors

tatizo la huyu Profesa akianza pumba zake......mh!!!!! Sababu kubwa ni kwamba anatumiwa na RA na analipwa unono, kwa hivyo hua hachunguzi data za kihistoria -- ni aibu kweli kweli. Anapayuka kama vile katiwa funguo.

Ni kama vile yule mama wa Kidosi -- Sakina alivyoboronga kuhusu suala la balozi wa palestina, hakutafiti historia kwa kuwa alilipwa na hao mafisadi.

Tatizo la kufanya kazi kwa malipo ys mafisadi yalimrudia RA mwenyewe pale alipowalipa watu kumpatia data za tuhuma za Mengi -- akarundikiwa data za kizushi kibao.
 
Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.

Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.

Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?

Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?

Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.

Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.

Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors

Keil

Lipumba yeye alijikita zaidi kwenye suala la kulaani mafisadi nyangumi. Hayo ya Makani na Mtei yalitangulia kuzungumzwa na wenzake wakina Maharagande na wengine. Mwenye audio tape ya mikutano yao atuwekee hapa. Kwa kweli wamesema mengi sana

.......ndiyohiyo
 
Keil

Lipumba yeye alijikita zaidi kwenye suala la kulaani mafisadi nyangumi. Hayo ya Makani na Mtei yalitangulia kuzungumzwa na wenzake wakina Maharagande na wengine. Mwenye audio tape ya mikutano yao atuwekee hapa. Kwa kweli wamesema mengi sana

.......ndiyohiyo


Maneno haya yamesemewa kwenye jukwaa la CUF mbele ya Lipumba na hata alipo jikita hakuyakanusha means yeye anayakubali.Waimaliza CUF ya wapemba maana Bara hakuna CUF jamani .
 
Hii ni habari njema kwa Chadema na ni bahati nzuri ilioje CUF kujitokeza wakati huu kwa sura zao halisi. Niliwahi kusema viko vyama vitajimaliza vyenyewe na ndio hali hiyo tunaishuhudia hivi sasa kwa NCCR, TLP na sasa CUF. Mwaka 2010 tunahitaji vyama viwili vichuane - Chadema na CCM !

CUF walipokubali kuingizwa mjini na CCM kwa kilichodaiwa ni muafaka, hata kipofu angetabiri mwisho wake. Utakubalije kupatanishwa au kuwa na muafaka na mwizi kama kweli unachukia wizi. Utapatanishwaje na zimwi lisiliheshimu sheria, linalohujumu haki na linalosigina katiba - wapi na wapi ?
Umesema ukweli kabisa na pia itakuwa vizuri sana kama wakifa hiyo ili tujue chama makini na pia CUF wanacheza pata potea. Kwanza hakuna tatizo la Mgogoro kule Zanzibar wala nini mimi nasema kuwa wanapoteza muda wao kuwasema CHADEMA
 
Keil

Lipumba yeye alijikita zaidi kwenye suala la kulaani mafisadi nyangumi. Hayo ya Makani na Mtei yalitangulia kuzungumzwa na wenzake wakina Maharagande na wengine. Mwenye audio tape ya mikutano yao atuwekee hapa. Kwa kweli wamesema mengi sana

.......ndiyohiyo

Nguvu ya fedha inashindwa na Mungu tu.... jamani ukiangalia ndugu zetu wapemba walivyowaamini viongozi wao mpaka kufikia kujitolea kufa, lakini viongozi wenyewe leo ndio wanawatetea mafisadi na CCM yao! lipunba atakufa kifo kibaya sana kwani ile damu ya wapemba waliouawa kwa risasi za polisi itamlilia.
 
Wakuonea huruma kwenye huu ulimbukeni wa CUF ni wapemba.... maskini ona hata wengine walipigwa risasi kama swala kwa kuwaamini viongozi wao... wakitegemea kuwa wana dhamira ya dhati ya kuwakomboa.... kumbe wenzao wanakula hela za mafisadi kina Rostam ... na wanachofanya ni igizo.... ukombozi wa wapemba watausikia kwenye bomba tu....
Wanasubiri mkombozi aje....pengine atakuja 2010 ya Mungu mengi...sijui kama watakuelewa CUF wanafanya igizo tusubiri uchaguzi mkuu labda watabadilishwa na operation sangara, zinduka na kumekucha. masikio yangu huru kusikia yatakayojiri
 
lipumba na maalim seif... Damu ya wapemba iliyomwagika kwa ajili yenu inawatafuta!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Keil

Lipumba yeye alijikita zaidi kwenye suala la kulaani mafisadi nyangumi. Hayo ya Makani na Mtei yalitangulia kuzungumzwa na wenzake wakina Maharagande na wengine. Mwenye audio tape ya mikutano yao atuwekee hapa. Kwa kweli wamesema mengi sana

.......ndiyohiyo

Sasa kama ni hivyo kwa nini alilani 'nyangumi" tu na sio 'mapapa?" Haihitaji mtu kuwa na degree yoyote kujua kwamba katumwa na hao "mapapa" -- akina RA. Haindoi ukweli huu -- na kwa kuwa hao viongozi wa CUF sasa wanaona adui yao mkubwa ni Chadema na siyo CCM na hivyo kuishambulia Chadema na siyo CCM ni sababu tosha kuwa CUF ni CCM-B -- hasa huku Bara. Pesa za Kagoda zinatumika hapo -- pesa za wananchi.

halafu hawa viongozi wa CUF wanachekesha sana. Viongozi wote wakuu wamejikita huko MZA wakati Pemba, ambayo ndiyo ngome yao kubwa wafuasi wao wanayimwa waziwazi fursa ya kujiandikisha kupiga kura. wasipoangalia CCM Visiwani itabeba majimbo yao yote ya Pemba wanayoringia nayo. Waachane na mambo ya Bara na waende kuwasaidia wafuasi wao wanaonyimwa kujiandikisha!
 
Sasa kama ni hivyo kwa nini alilani 'nyangumi" tu na sio 'mapapa?" Haihitaji mtu kuwa na degree yoyote kujua kwamba katumwa na hao "mapapa" -- akina RA. Haindoi ukweli huu -- na kwa kuwa hao viongozi wa CUF sasa wanaona adui yao mkubwa ni Chadema na siyo CCM na hivyo kuishambulia Chadema na siyo CCM ni sababu tosha kuwa CUF ni CCM-B -- hasa huku Bara. Pesa za Kagoda zinatumika hapo -- pesa za wananchi.

halafu hawa viongozi wa CUF wanachekesha sana. Viongozi wote wakuu wamejikita huko MZA wakati Pemba, ambayo ndiyo ngome yao kubwa wafuasi wao wanayimwa waziwazi fursa ya kujiandikisha kupiga kura. wasipoangalia CCM Visiwani itabeba majimbo yao yote ya Pemba wanayoringia nayo. Waachane na mambo ya Bara na waende kuwasaidia wafuasi wao wanaonyimwa kujiandikisha!
Nina wasiwasi kama wanasikiliza ushauri...waache wakanyagane ili tujue ukweli zaidi...wakilumbana (kurushana makombora) tutajua viongozi na wababaishaji ni kina nani??..masikio yangu yako huru kusikia chadema wa kijibu tuhuma hizo (wawaumbue CUF)..that will make sense!
 
Ahsante sana Profesa Lipumba kwa kuzidi kuwaanika mafisadi,hii ya Chadema kuwa ni CCM B inajulikana zamani sana ,kwa ufupi CHADEMA ni wanafiki na waongo wakutupwa ni wao wanaowadanganya WaTz kwa ujanja mkubwa sana, CUF imeshindwa kuvumilia maana Chadema imeonysha haivumiliki wala haichukuliki.

Chadema imenaswa pabaya sana ,napenda kuwaonya WaTz kuwa wasiwe na Jazba wala wasiwe wenye kuzidi upande mmoja ,kama hapa JF kuna msemo au heading kuwa the Palace of Great Thinkers & ukiongezea ..We Dare to Talk Openly.

So Mheshimiwa Lipumba ametibua hoja kuwaambia WaTz kuwa hata CHADEMA nao ni mafisadi , na akwataja akina Bob Makani(aliewahi kuwepo CUF) na Edwin Mtei kuwa waliibia Benki na kama haitoshi wakaichoma moto ,Sasa waTz hii au hili sio jambo dogo na utawezaje kuwakabili CCM ikiwa ndani mwako wapo watu ambao nao wameiba na kuichoma moto benki ,hivi hapa kuna baya lipi ? Je hilo ni kosa ? Msiukimbie ukweli maana tunahitaji viongozi ambao ni wasafi ,iwe Chadema au CUF ,ni vizuri kama watu wa Chadema mpo hapa basi mlijadili hili ,ili kujisafisha ,kusema Profesa hana isipokuwa pumba huko mtakuwa mnakimbia vivuli vyenu wenyewe ,ila kwa mwenye akili ya kutaka kuijenga Tz yenye viongozi safi ,basi hana wajibu kumuunga mkono Mheshimiwa Lipumba na kuzifanyia kazi hoja zake ,nahisi Chadema wanahitaji kuzijibu hoja hizi ,lakini Lipumba amesema kwa ushahidi sasa kama huko Chadema mkifanya siri mjue ,siku hizi siri zinauzika au zinauzwa , ninachowaomba muwe makini na vyama vya upinzani sio mnafuata tu kwa kuwa Chadema inakuja na mabomu mengi huko bungeni ,inawezekana kabisa mabomu hayo ni kujikinga dhidi ya mashambulizi.


Inaonyesha kabisa kuwa kimya kirefu cha CUF katika mambo ya mafisadi ilikuwa ni kuwasoma wale wote wanaolipua mabomu ,na labda tuseme wananchi wwalikuwa wameshatekwa na watu hawa na kuwaona kuwa ..hawa ndio viongozi wanaoweza kutuletea maendeleo au sio na ikafikia kuwa kila mtu anaona waChadema ni viongozi makini kabisa ,sasa katika uono huo CUF imeweza kuwasoma na kuwakuta kuwa kumbe hata hawa wanaolipua mabomu pale bungeni ni maadui wa Taifa hili kwa msemo mwengine ni mafisadi.

......Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili...!.

Jamani hizo ni tuhuma nzito sana ,tena sana sio mchezo ,hapo wametajwa viongozi wa juu kabisa wa CHADEMA ,kwa maana ingine tusiwe tunawapigia kelele wale wa EPA ,RIchmond ,Twin BOT buildings na mengine ,tukawaacha hawa kwa kuwa tu ni wa CHADEMA ,hilo litakuwa halikubaliki ,tuwe wenye kuwaongoza wananchi pale panapoonekana pana manufaa as a Jamii Forums na sio kuwakandia CCM peke yao ,lazima tuvikubali vile vyama ambavyo vinaoonyesha viongozi wake wapo katika mstari ulio sawa ,hawana madoa madoa ,tukumbuke harakati za uchaguzi wa Marekani ,kitu kidogo tu alichonacho mgombea kinaweza kabisa kuhatarisha uchaguliwaji wake ,sasa tujaribu kuiga yale mambo ambayo wenzetu huwa wanayafuata katika kumchagua kiongozi alie bora.

Tuacheni jazba na tujaribu kuutafuta ukweli ,na ukweli wa viongozi ambao tunategemea ipo siku watatuongoza , Sasa habari ndio hiyo ipo magazetini ,tuwajadili akina viongozi hawa wa CHADEMA ambao kama wengine mnavyoona kuwa wana nafasi ya kuwa viongozi au kushika madaraka ya nchi hii ,na hivyo kuwaelekeza wananchi pale ambapo patagunduliwa kuwa ni kweli ,aidha Chadema wanayo nafasi ya kuwasafisha viongozi hao ikiwa wanasafishika ,kwa maana ingine kuonyesha kuwa tuhuma walizopachikwa ni uongo ,na sio kusema uongo tu ,tunahitaji kuona CHADEMA inadai uthibitisho kutoka kwa CUF juu ya tuhuma hizo ,kukaa na kusema Lipumba au CUF ni wababaishaji ,wameishiwa ,hawana jipya ,sijui wamechemsha na menginetele ,kwa kweli hakutowasaidia CHADEMA ,aidha natarajia kuona viongozi wa CHADEMA wakikusanya vyombo vya habari na kupinga ,ila kama mambo hayo ni kweli basi watakuwa wamefwulia.
 
Nguvu ya fedha inashindwa na Mungu tu.... jamani ukiangalia ndugu zetu wapemba walivyowaamini viongozi wao mpaka kufikia kujitolea kufa, lakini viongozi wenyewe leo ndio wanawatetea mafisadi na CCM yao! lipunba atakufa kifo kibaya sana kwani ile damu ya wapemba waliouawa kwa risasi za polisi itamlilia.

Kweli inasikitisha. sasa hivi Wapemba wanayimwa kujiandikisha kupiga kura ili CCM wayachukue majimbo yao 2010 viongozi wao wako huku Bara wanatumikia agenda za RA dhidi ya maadui zake.

Profesa, tulikuamini sana, achana na hao akina Jussa na Maalim, pigania haki ya wazalendo hapa wanaoibiwa fedha zao kila siku na majambazi ya CCM. Achana kuikandia Chadema kwa agizo la RA, ungana na Chadema katika kuutokomeza ufisadi ndani ya CCM kwa lengo la kuleta utawala bora. Achana na tamaa ya pesa za wizi, pigania haki ya wazalendo hata bila malipo, kwani siasa za kweli ni kujitolea.

Kama kweli una uchungu wa nchi hii, adui yako inapasa awe CCM, na siyo Chadema. Unapotea sana. Utakimbiwa na wengi.
 
Ahsante sana Profesa Lipumba kwa kuzidi kuwaanika mafisadi,hii ya Chadema kuwa ni CCM B inajulikana zamani sana ,kwa ufupi CHADEMA ni wanafiki na waongo wakutupwa ni wao wanaowadanganya WaTz kwa ujanja mkubwa sana, CUF imeshindwa kuvumilia maana Chadema imeonysha haivumiliki wala haichukuliki.

Chadema imenaswa pabaya sana ,napenda kuwaonya WaTz kuwa wasiwe na Jazba wala wasiwe wenye kuzidi upande mmoja ,kama hapa JF kuna msemo au heading kuwa the Palace of Great Thinkers & ukiongezea ..We Dare to Talk Openly.

So Mheshimiwa Lipumba ametibua hoja kuwaambia WaTz kuwa hata CHADEMA nao ni mafisadi , na akwataja akina Bob Makani(aliewahi kuwepo CUF) na Edwin Mtei kuwa waliibia Benki na kama haitoshi wakaichoma moto ,Sasa waTz hii au hili sio jambo dogo na utawezaje kuwakabili CCM ikiwa ndani mwako wapo watu ambao nao wameiba na kuichoma moto benki ,hivi hapa kuna baya lipi ? Je hilo ni kosa ? Msiukimbie ukweli maana tunahitaji viongozi ambao ni wasafi ,iwe Chadema au CUF ,ni vizuri kama watu wa Chadema mpo hapa basi mlijadili hili ,ili kujisafisha ,kusema Profesa hana isipokuwa pumba huko mtakuwa mnakimbia vivuli vyenu wenyewe ,ila kwa mwenye akili ya kutaka kuijenga Tz yenye viongozi safi ,basi hana wajibu kumuunga mkono Mheshimiwa Lipumba na kuzifanyia kazi hoja zake ,nahisi Chadema wanahitaji kuzijibu hoja hizi ,lakini Lipumba amesema kwa ushahidi sasa kama huko Chadema mkifanya siri mjue ,siku hizi siri zinauzika au zinauzwa , ninachowaomba muwe makini na vyama vya upinzani sio mnafuata tu kwa kuwa Chadema inakuja na mabomu mengi huko bungeni ,inawezekana kabisa mabomu hayo ni kujikinga dhidi ya mashambulizi.


Inaonyesha kabisa kuwa kimya kirefu cha CUF katika mambo ya mafisadi ilikuwa ni kuwasoma wale wote wanaolipua mabomu ,na labda tuseme wananchi wwalikuwa wameshatekwa na watu hawa na kuwaona kuwa ..hawa ndio viongozi wanaoweza kutuletea maendeleo au sio na ikafikia kuwa kila mtu anaona waChadema ni viongozi makini kabisa ,sasa katika uono huo CUF imeweza kuwasoma na kuwakuta kuwa kumbe hata hawa wanaolipua mabomu pale bungeni ni maadui wa Taifa hili kwa msemo mwengine ni mafisadi.

......Viongozi hao wameeleza kwamba hata viongozi wa CHADEMA waliofuata wakina Freeman Mbowe, Dr Slaa na Zitto Kabwe wote wana tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazowakabili...!.

Jamani hizo ni tuhuma nzito sana ,tena sana sio mchezo ,hapo wametajwa viongozi wa juu kabisa wa CHADEMA ,kwa maana ingine tusiwe tunawapigia kelele wale wa EPA ,RIchmond ,Twin BOT buildings na mengine ,tukawaacha hawa kwa kuwa tu ni wa CHADEMA ,hilo litakuwa halikubaliki ,tuwe wenye kuwaongoza wananchi pale panapoonekana pana manufaa as a Jamii Forums na sio kuwakandia CCM peke yao ,lazima tuvikubali vile vyama ambavyo vinaoonyesha viongozi wake wapo katika mstari ulio sawa ,hawana madoa madoa ,tukumbuke harakati za uchaguzi wa Marekani ,kitu kidogo tu alichonacho mgombea kinaweza kabisa kuhatarisha uchaguliwaji wake ,sasa tujaribu kuiga yale mambo ambayo wenzetu huwa wanayafuata katika kumchagua kiongozi alie bora.

Tuacheni jazba na tujaribu kuutafuta ukweli ,na ukweli wa viongozi ambao tunategemea ipo siku watatuongoza , Sasa habari ndio hiyo ipo magazetini ,tuwajadili akina viongozi hawa wa CHADEMA ambao kama wengine mnavyoona kuwa wana nafasi ya kuwa viongozi au kushika madaraka ya nchi hii ,na hivyo kuwaelekeza wananchi pale ambapo patagunduliwa kuwa ni kweli ,aidha Chadema wanayo nafasi ya kuwasafisha viongozi hao ikiwa wanasafishika ,kwa maana ingine kuonyesha kuwa tuhuma walizopachikwa ni uongo ,na sio kusema uongo tu ,tunahitaji kuona CHADEMA inadai uthibitisho kutoka kwa CUF juu ya tuhuma hizo ,kukaa na kusema Lipumba au CUF ni wababaishaji ,wameishiwa ,hawana jipya ,sijui wamechemsha na menginetele ,kwa kweli hakutowasaidia CHADEMA ,aidha natarajia kuona viongozi wa CHADEMA wakikusanya vyombo vya habari na kupinga ,ila kama mambo hayo ni kweli basi watakuwa wamefwulia.

Hiki Chama cha wapemba ndiyo kinazikwa rasmi huku bara na Lipumba anarudi CCM rasmi maana hawezi kula pesa zao then awaseme.Seifu anakula marupurupu ya CCM muda sasa na ndiyo maana kauchuna .Kazi hii ina mwisho wake .
 
Back
Top Bottom