CUF kuirudisha TANGANYIKA

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Na Mwandishi wetu.
Elias Kundecha.
10.08.2010

Habari za kurudi kwa Zanzibar kama nchi nje ya mipaka yake na ndani ya Jamhuri ya Muungano kumeibua hisia mpya za viongozi waandamizi ndani ya Chama cha CUF ambacho kimekuwa mstari wa mbele katika kudai serikali tatu,madai ambayo ni nambari one katika sera za CUF.

Habari zilizozagaa katika mitaa ya Zanzibar ambazo inasemekana zinategemewa kupitishwa katika kikao cha Baraza La Wawakilishi ni kwa kuibadilisha Katiba ya Zanzibar kwa baadhi ya vifungu vinavyoonyesha kuwa Zanzibar itakuwa Nchi kamili yenye kujiamulia na kujipangia mambo yake bila kupitia katika Bunge la Muungano ,baadhi ya mabadiliko hayo ni ‘Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyoizunguuka na bahari yake, ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar’.Hapa wanadai kuwa hata Mombasa ni sehemu ya Zanzibar ,kumbuka tu kuna kesi inategemea kuwakilishwa katika mahakama ya kimataifa ,ikishitakiwa Kenya na UK kuhusiana na Mombasa.

Pia kuna madai yanayoonyesha kuwa
Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Kipande ambacho ndicho kitakachoisukuma CUF kuidai na kuirudisha Tanganyika iwapo itaibuka na Ushindi katika uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,hapo ndipo itakapotekeleza sera ya kuwa na serikali Tatu ,vilevile inatarajia kuibua hoja ya kuitisha kura ya maoni ikiwa wananchi wa Tanganyika watakubali kurudishwa kwa serikali ya Tanganyika kura ambayo maoni au uamuzi wa mwisho ni serikali iliyopo madarakani.

Viongozi hao wa serikali wamesikika wakisema iliobaki ni Tanganyika kwani Zanzibar inazidi kuonyesha mikakati ya kujiongoza katika maendeleo bila ya kuitegemea serikali iliyokuwepo ya Muungano ,serikali ambayo imeshindwa kutekeleza ahadi nyingi ikiwemo suala la kushughulikia wala rushwa wakubwa ,na hivyo kuiwacha nchi ikipoteza dira.Na waliopo madarakani wakiogopana katika kuchukuliana sheria na kuacha ,sheria na hukumu zichukue mkondo wake.

Hata hivyo viongozi hao walisema bado waTanzania wengi wamelala na wapo katika ndoto kuwa ipo siku CCM itawakomboa ,ndoto ambayo haitekelezeki.Na katika mikakati iliyojipangia CUF imesema itaanza harakati zake za kampeni kwa kuwahamasisha wananchi kuwa iwapo itaingia madarakani itahakikisha Serikali ya Tanganyika inarudi na dira watazindua dira mya kwa waTanganyika wote.
 
Anyway time will tell, hawa ccm laikini wana boa kila kitu kwao ni siasa tu. Hata mambo ya msingi watapiga domo. Hapa pana moshi, lakini watalichukulia hili kimzaha tu, mambo yataendelea kukusanyana mpaka kikombe kifulike
 
Kwa mujibu wa katiba mabadiliko yeyote yanayohusiana na suala la mwungano lazima yaidhinishwe na 2/3 ya bunge la Mwungano. Sidhani CUF wana nguvu au watakuwa na nguvu za kiasi hicho katika bunge. Lakini hakuna ubaya wa kuota.
 
Kwa mujibu wa katiba mabadiliko yeyote yanayohusiana na suala la mwungano lazima yaidhinishwe na 2/3 ya bunge la Mwungano. Sidhani CUF wana nguvu au watakuwa na nguvu za kiasi hicho katika bunge. Lakini hakuna ubaya wa kuota.

Hawa CUF watakuwa wamejadiliana Msikitini!
 
Jaribu kujiweka kwenye nafasi ya Rais aliye makini; ungefanyaje kama ni wewe una uchaguzi ambao upepo wake umegeuka ghafla kukupunguzia nafasi ya ushindi, ndani ya chama una kesi kibao za kuamua kutengua matokeo au la! Kila ukiangalia taarifa ya habari wanachama ni au kurudisha kadi ama kutishia kufanya hivyo majina ya watu wao yasiporudi.Wakati huo huo maadui wamepatana na wanafanya maamuzi ki-wendawazimu kubadili historia kwa njia ya Katiba. UTAFANYAJE?!

Yaani, nahisi JK aliko anahisi bora angekubali tu asigombee term hii ya pili.
 
Na Mwandishi wetu.
Elias Kundecha.
10.08.2010

Habari za kurudi kwa Zanzibar kama nchi nje ya mipaka yake na ndani ya Jamhuri ya Muungano kumeibua hisia mpya za viongozi waandamizi ndani ya Chama cha CUF ambacho kimekuwa mstari wa mbele katika kudai serikali tatu,madai ambayo ni nambari one katika sera za CUF.

Habari zilizozagaa katika mitaa ya Zanzibar ambazo inasemekana zinategemewa kupitishwa katika kikao cha Baraza La Wawakilishi ni kwa kuibadilisha Katiba ya Zanzibar kwa baadhi ya vifungu vinavyoonyesha kuwa Zanzibar itakuwa Nchi kamili yenye kujiamulia na kujipangia mambo yake bila kupitia katika Bunge la Muungano ,baadhi ya mabadiliko hayo ni 'Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyoizunguuka na bahari yake, ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar'.Hapa wanadai kuwa hata Mombasa ni sehemu ya Zanzibar ,kumbuka tu kuna kesi inategemea kuwakilishwa katika mahakama ya kimataifa ,ikishitakiwa Kenya na UK kuhusiana na Mombasa.

Pia kuna madai yanayoonyesha kuwa
Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Kipande ambacho ndicho kitakachoisukuma CUF kuidai na kuirudisha Tanganyika iwapo itaibuka na Ushindi katika uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,hapo ndipo itakapotekeleza sera ya kuwa na serikali Tatu ,vilevile inatarajia kuibua hoja ya kuitisha kura ya maoni ikiwa wananchi wa Tanganyika watakubali kurudishwa kwa serikali ya Tanganyika kura ambayo maoni au uamuzi wa mwisho ni serikali iliyopo madarakani.

Viongozi hao wa serikali wamesikika wakisema iliobaki ni Tanganyika kwani Zanzibar inazidi kuonyesha mikakati ya kujiongoza katika maendeleo bila ya kuitegemea serikali iliyokuwepo ya Muungano ,serikali ambayo imeshindwa kutekeleza ahadi nyingi ikiwemo suala la kushughulikia wala rushwa wakubwa ,na hivyo kuiwacha nchi ikipoteza dira.Na waliopo madarakani wakiogopana katika kuchukuliana sheria na kuacha ,sheria na hukumu zichukue mkondo wake.

Hata hivyo viongozi hao walisema bado waTanzania wengi wamelala na wapo katika ndoto kuwa ipo siku CCM itawakomboa ,ndoto ambayo haitekelezeki.Na katika mikakati iliyojipangia CUF imesema itaanza harakati zake za kampeni kwa kuwahamasisha wananchi kuwa iwapo itaingia madarakani itahakikisha Serikali ya Tanganyika inarudi na dira watazindua dira mya kwa waTanganyika wote.

CUF kwa sera hizo itazidi kujimaliza Bara, labda watuambie Serikali ya Tanganyika itamalizaje umaskini wetu? Au wanataka tu neno "Tanganyika" lionekane kwenye karatasi and that's it! Hatutaweza kudanganyika kwa sera ambazo hazina mantiki yoyote!
 
Hizo habari za kutaka Mombasa iwe sehemu ya Zenj ni kujitakia matatizo na Wakenya kwa nguvu!
 
CUF wanaota ndoto ya mchana - kama Tanzania bara hawakuweza kumpata hata mwakilishi moja wa kuchaguliwa bungeni, sasa hiyo nguvu ya kuirudisha Tanganyika wataitoa wapi ?
 
Wenye Tanganyika hawajaidai na wako powaa, kwa nini mdai nyie? Hawawezi kupata kura kwa hoja za "nyuma ya pazia". Jengeni hoja za msingi kwa kuleta sera zenye mashiko! Agghhhh, Malari Sugu, ka njomba waeleze ndugu zako ati !! :glasses-nerdy:
 
CUF wanaota ndoto ya mchana - kama Tanzania bara hawakuweza kumpata hata mwakilishi moja wa kuchaguliwa bungeni, sasa hiyo nguvu ya kuirudisha Tanganyika wataitoa wapi ?

Hiyo Nguvu hawana lakini kuna tatizo la kuitambua Zanzibar kama nchi ktk katiba ya Z'bar. Hili jambo serikali inayoitwa ya muungano hailitaki kabisa! (kumbuka maelezo ya PM Pinda juu ya Zbar ni nci au la). Lakini pia Serikali ya Muungano haina madaraka ya contents za katiba ya Zanzibar!

Tusubiri maelewano ya Z'bar yataleta makubwa tu!
 
CUF wanaota ndoto ya mchana - kama Tanzania bara hawakuweza kumpata hata mwakilishi moja wa kuchaguliwa bungeni, sasa hiyo nguvu ya kuirudisha Tanganyika wataitoa wapi ?

kanza kabisa hakuna Tanzania Bara, ipo Tanganyika....CUF wanataka kuirejesha Tanganyika kwa maslahi ya watanganyika...
 
Ndoto za Alinacha ile sema serikali CCM nayo ni chanzo cha matatizo.

Lwa nini wankaa kimya kwenye issues kama hizi? Ilipaswa watu wakewe immediately.
 
ningekua mimi rais wa muungano kama wazanzibar kweli wanaona muungano hawautaki, basi mara moja ningeuvunja kwani hauna faida yoyote, ni sawa uwe na mke unamlisha, unamvisha, anakuzalia mitoto mipumbavu lakini bado hakutaki, wa nini kuendelea kukaa nae?
 
ningekua mimi rais wa muungano kama wazanzibar kweli wanaona muungano hawautaki, basi mara moja ningeuvunja kwani hauna faida yoyote, ni sawa uwe na mke unamlisha, unamvisha, anakuzalia mitoto mipumbavu lakini bado hakutaki, wa nini kuendelea kukaa nae?

Huu mfano si mzuri. Upumbavu saa ingine unatoka kwa baba!
Halafu wanawake wa siku hizi, hata kijijini wenye kulishwa, kuvishwa na waume zao, idadi ya ni ndogo mno. Wanawake siku hizi (na hata zamani) ndio wanaolisha familia ati
 
Back
Top Bottom