CRDB Mnatuibia, acheni

CRDB Mnatuibia, acheni

Najaribu kufikir tu...kama akikopa lak 2. Anapokea lak 90 maanake wamekata 5% ya hela uliyooomba yaan lak 2.

Sasa tuje siku ya malipo...fikiria weww ukiwalipa tu ile lak na 90 uliyochukua cash je wao watakuwa wametengeneza faida?! Jibu ni hapana. Watakuw hawajaingiza income yoyote hapo.

Ukitaka kuelewa zaidi chukulia kama wangekupa lak 2 kamili...bila shaka ungelipa lak 2 na elf 10. Sasa kwasababu walishachukua elf 10 yao toka mwanzo ndo sababu unarudisha lak 2 kamili.

Anyway...najua hesabu hii alikuja nazo Dr living Stone....

Sent using Jamii Forums mobile app

Sawa mkuu,
Sasa fikiria kuwa umepewa 190, na unatakiwa ulipe na 5% utalipa shs ngapi?
Maana kama halali yao ni 5% haupaswi kuwalipa 10%.
Msijifiche nyuma ya kikokotoo. Mngetaka haki bin khalali mngempa hiyo 200 kisha mkate 210 wakati wa mrejesho
 
Awali ya yote naomba usinijumuishe. Wenye majibu zaidi ni wao...lakin la msingi hapa ni kuelewa design ya huduma.

Hapa tuna mfano wa lak 2. Asilimia 5 ya lak ni elf 10. Hvo mkopeshaji anasema mie ada yangu nilipe mapema.....wewe huna lak 2 ila unahitaj akukopeshe...si inakulazim kufuata masharti yake?!


Sasa basi ikiwa shart lake ndilo hilo...wewe hoja yako ya haki bin hak inatoka wapi maana ukumbuke hajakulazimisha uchukue.

Pia hapo alichokata 5% hakuna nyongeza....unadhan wao hawajui kwamba kuna benki kuu inatizama?!
Sawa mkuu,
Sasa fikiria kuwa umepewa 190, na unatakiwa ulipe na 5% utalipa shs ngapi?
Maana kama halali yao ni 5% haupaswi kuwalipa 10%.
Msijifiche nyuma ya kikokotoo. Mngetaka haki bin khalali mngempa hiyo 200 kisha mkate 210 wakati wa mrejesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
bhikola na wadau wengine, huibiwi sema tu hawajakupa maelezo kwa nini unalipia 1180, iko hivi hiyo shule ndo imefungua akaunt crdb, huwa kuna amount wanatakiwa walipie sasa mara nyingi mwanzoni wenye mashule huwa hawalipii wanakwepa hiyo gharama na inahamishiwa kwenu.
Bora shule ilipie halafu wataijumlisha kwenye ada ili kuwaondelea usumbufu wateja/wazaz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuwa mteja wa CRDB miaka 15 sijaona wizi unaouongelea hapa, hii ni benki ya kitanzania ya mwanzo kabisa kufanya maboresho makubwa kwenye utoaji huduma za kisasa za kibenki ikiwemo kupanua mtandao wake katika maeneo mengi ya nchi. Kama kuna huduma umepata isivyotakiwa ni bora kuwaona uongozi kabla ya kuja kutoa shutuma zinazoharibu taswira nzima ya benki
 
Juzijuzi BOT walisema wanaanza kufatilia makato ya benki ambayo wanalipisha wateja kimsingi yanatakiwa kuwa kwao kama sehemu ya gharama zao za uendeshaji sasa sijui wamefikia wapi hata mimi sijawahi kusikia hiyo kitu ndio maana watu wengi hawaweki pesa benki inawezekana kuna kitu hiyo shule inapata kupitia crdb
 
Kwani mwenye shule amekwambia makubaliano aliyonayo na CRDB-Bank PLC? Ingawa unataka kuonesha kuwa umefikia kiwango cha digital, ukweli ni kuwa bado uko analogia, tena sana. Wewe lipa tu karo ya mwanao asome badala ya kulalamikia vijimambo vidogo vidogo. Benki zote hutoza bank charges kwa huduma wanazotoa, na hii hulingana na makubaliano baina ya benki husika na wateja wake. Kwanza inaonekana ni mara yako ya kwanza kusomesha mtoto shule binafsi, na umefanya hivyo reluctantly.
Unamshipa wa ngiri ww, incase hujui kitu bora ufunge bwambwa, unakubali vp kulipia deposits... Mlalamikaji ni haki yake.... People kama ninyi hamfai ktk jamii, yaan roho mbaya, Mwisho
 
Habari wakuu,
Nimetafuta jukwaa la fedha au malalamiko sijaliona, so kama haifit hapa mnisamehe.

Iko hivi, jananimekwenda kulipa ada kwaajili ya kijana wangu anaanza Kidato cha kwanza (shule ipo Dodoma). Sakata lilianzia shuleni, hawataki malipo ambayo hayajapitia dirishani kwa benki.

Yaani lazima uwe na pay slip ya bank. So, hauwezi kufanya mobile payment wala internet banking. Hii ikawa kero kubwa sana maana kwa ulimwengu huu ulivyo sipiiiidiiii haifai watu hasa taasisi kubaki analojia.

Kufika bank (CRDB tawi lipo Moro), nikaambiwa, kila transaction ya kuweka pesa kwenye akaounti ya hiyo shule natakiwa nilipie charge ya Tshs 1,180.00 Hii kwangu ilikuwa na mpya, ya ajabu na wizi. Unaanzaje kutozwa fedha kwa kudeposit? Sijawahi kuiona popote dunia nzima

CRDB acheni hizi mambo, mnatuibia, hakuna gharama ya kudeposit
Ni hayo tu
Mkuu kuna tofauti kati ya ku deposite na ku transact.nadhani tatizo ni interpretation
 
Miaka ya nyuma kidogo NMB walishanifanyia huu mchezo, sikuelewa..ila walikuja kuacha
 
mbona hyo ya kudeposi tsh 1000 kwa ada za shule kupitia CRDB ipo tangu zamani mm nimedeposit ada yangu mwaka 2009-2012 na nikatoa hela ya deposit ili branch ya CRDB karagwe..sasa sijui n wizi au ndo utaratibu wa baadhi ya branch zao
 
Habari wakuu,
Nimetafuta jukwaa la fedha au malalamiko sijaliona, so kama haifit hapa mnisamehe.

Iko hivi, jananimekwenda kulipa ada kwaajili ya kijana wangu anaanza Kidato cha kwanza (shule ipo Dodoma). Sakata lilianzia shuleni, hawataki malipo ambayo hayajapitia dirishani kwa benki.

Yaani lazima uwe na pay slip ya bank. So, hauwezi kufanya mobile payment wala internet banking. Hii ikawa kero kubwa sana maana kwa ulimwengu huu ulivyo sipiiiidiiii haifai watu hasa taasisi kubaki analojia.

Kufika bank (CRDB tawi lipo Moro), nikaambiwa, kila transaction ya kuweka pesa kwenye akaounti ya hiyo shule natakiwa nilipie charge ya Tshs 1,180.00 Hii kwangu ilikuwa na mpya, ya ajabu na wizi. Unaanzaje kutozwa fedha kwa kudeposit? Sijawahi kuiona popote dunia nzima
L
CRDB acheni hizi mambo, mnatuibia, hakuna gharama ya kudeposit
Ni hayo tu

Kasome Tangazo lao la viwango vya malipo ya huduma liloanza tumika tarehe 1.1.2019 viwngo vyote hivyo vime ainishwa
 
aani lazima uwe na pay slip ya bank. So, hauwezi kufanya mobile payment wala internet banking
Samahani Mukuu, Hata POS walikataa, Ile kwa wakala wa CRDB bank?? Naona Umezungumzia Channel mbili tu Mobile na Internet
 
hili linekuwa libenki la kijizi, mara liwachome wateja wake kwa majambazi, mara liwachome wateja kwa polisi yaani kwa sasa nishida tupu!

Na ukienda kuchukua pesa ndani kuanzia kama 5M na ku endelea utaulizwa maswali mia kidogo mara pesa umewekea na nani na wapi kutokea wapi ukiwajibu bado eti mpaka wapige simu toka kwenye iyo branch kiukweli wanaboa kinyama ila izi ni dalili ya kufa apo dawa ni kutoa pesa yako yote iyo imenikuta jana tu j3 hawafai
 
Mfano ile Salary Advance wife akikopa 200,000/= wanampa 190,000/= mshahara ukitoka hawakati hiyo 190,000/= wanamlima tena 200,000/= nilimwambia bora ukope VICOBA tu.

Acha ushamba. Kwa mengine tulaumu lakini kwa hili wewe ni mshamba. Vicoba ukikopa laki 2 unarudisha ngapi pamoja na riba?
Salary advance ya CRDB riba ni 5%. Maana yake ukikopa laki 2, utarudisha 210,000. Sasa wewe unataka ukope laki 2 alafu urudishe laki 2? hapo wao wanafaidikaje na huduma hiyo? Jifunze mahesabu broo. Kinachofanyika wao wanakukopesha kimahesabu laki 2, lakini wanakata kabisa riba yao 5%, ndo maana unapewa 190,000. kwa kuwa wameshakata riba, wakati wa kurejesha watakata ile ile laki 2 tuu. Haina tofauti na ungepewa laki 2 alafu urudishe laki 2na elf kumi.
 
Back
Top Bottom