CRDB Kitengo cha Refunds Acheni wizi

rkgx

Senior Member
Nov 30, 2013
100
80
Natumia huduma ya kadi kufanya manunuzi online na kwa muda mrefu nimekuwa nikinunua vitu online kupitia paypal (gateway) lakini huwa inatokea muda mwingine nikanunua kitu halafu seller akashindwa kuleta nafungu kesi paypal na baadaye seller anaamua kunilipa (refund) lakini cha ajabu nikishalipwa na seller hela yangu huwa hairudi kwenye akaunti. Na mara nyingi nikirudishiwa hela paypal nao huwa wananitumia email kwamba nimerudishiwa hela na kwakuwa huwa nanunua kwa kutumia CRDB Visa Card hela yangu huwa inarudi kwenye akaunti yangu.

Hivi karibuni yapata kama mwezi mmoja na siku kadhaa hivi nilifanya transaction online ya $139.99 ambayo kwa hela ya kibongo ni kama 316,632 Tsh. Baadaye seller akasema kwamba ameishiwa na stock kwahiyo atarudisha hela yangu ili baadaye akiwa na bidhaa stock atanitaarifu nilipie tena. Baada ya siku tatu seller akanitumia meseji kwamba ameni-refund tayari na baadaye paypal wakathibitisha kwamba nimerudishiwa hela na imerudi kwenye akaunti yangu. Niliwasiliana na watu wa customercare kwa email nikawaambia juu ya suala hilo nao wakawasilisha kwenye Idara ya Refunds, baada ya hapo nikapokea email kutoka kwao kwamba niwatumie receipt ya refund hiyo kwa pdf nikafanya hivyo na nikawatumia na refunds zangu za nyuma ambazo kwa kipindi chote sikuwahi ziona kwenye bank statement yangu kama zimerudi.

Sasa cha ajabu tangu niwatumie hizo receipt hadi leo ni mwezi mzima hakuna mtu yeyote aliyetoa jibu kwamba nini kinaendelea, nimewaandikia emails zaidi ya saba hawajibu na nimewasiliana na watu wa customercare wanasema tatizo lako tumeliwasilisha wanalishughulikia. Lakini cha ajabu kwa kipindi hiki chote ninachosubiri kupata majibu kutoka kwao kuna harufu ya wizi naiona. Kuna thread kama hii niliisoma hapa kwenye jukwaa inaelezea jinsi wanavyoshirikiana kuzila hizo pesa za refunds kwa kugawana kuanzia kwa wakubwa wa vitengo hivyo ndio maana kwenye suala langu la kudai refunds zangu kuna kigugumizi kikubwa.

Najua kuna wengine wanaweza kuwa na experience kama hii nawaombeni mjitokeze hapa maana nafikiri hii siyo misingi bora ya utoaji huduma especially kwa Benki kubwa kama CRDB ambayo wateja wengi tunaiamini. Inaweza kuwa kuna watu wachache wanafanya hizo mambo na kuichafua Bank lakini nashangaa hata watu wa customer service nao kutojibu querry za wateja ni maadili ya kazi zao?
 
CRDB ni sheedah sana. Imeshanitokea mara kadhaa kwa kweli pesa hairudishwi kama inavopaswa. One time nilikuwa na refund ya $700 hivi. Baada ya kufuatilia sana ilinilazimu kuandika barua ndio nikafanikiwa....ilikuwa kwa mbinde kweli kweli.
 
Mpaka ninavyoandika hapa ni returns za takribani Euro 400. Yapata miezi miwili sasa. CRDB International House nahisi ndio wanaosababisha kadhia hii kwa wateja. Kuna mtu amenishauri niumie Kado za Exim. Hawana usumbufu wa aina hii and kwa wateja.
 
Pole Mkuu. Huko kwa wenzetu, mabenki ndiyo taasisi zinazopigiwa mfano kwa best customer services. Lakini hapa Bongo ni kinyume chake. Mabenki ndizo taasisi zilizokubuhu kwa urasimu na utendaji duni. Huwa nawashangaa sana akina Dr. Kimei ninapowaona kwenye TV wakijinadi kwa mafanikio ya taasisi zao. Ni kweli hawajui? hawaongei hata na wateja wao wakapata feedback? CRDB, NBC and NMB zote ni disaster.
 
Watu humu shule sijui tunaenda kufanya nini umesema umenunua kupitia PayPal na pesa iko PayPal sasa hapo Crdb atarudishaje hela wakati iko kwenye acc yako ya paypal? Ni lazima wewe uhamishe pesa iliyoko PayPal kwenda bank kwasababu bank haina access na account yako ya paypal
 
Wahuni sana maana wana kigugumizi sana kurudisha hela, hapo hapo ukiwauliza wanasema eti lazima tupate ushahidi kama kweli seller amerudisha.
Mie huwa natumia StanChart, refund inaingia kwenye akaunti hapo kwa papo hakuna figisu.
Pole sana.
hata mi najiuliza kwanini wasiweke hela moja kwa moja kwenye account?
 
Watu humu shule sijui tunaenda kufanya nini umesema umenunua kupitia PayPal na pesa iko PayPal sasa hapo Crdb atarudishaje hela wakati iko kwenye acc yako ya paypal? Ni lazima wewe uhamishe pesa iliyoko PayPal kwenda bank kwasababu bank haina access na account yako ya paypal
Tulia mkuu paypal ni gateway labda kama hukuelewa basi bado kuna nafasi ya kueleweshana tu.
 
Watu humu shule sijui tunaenda kufanya nini umesema umenunua kupitia PayPal na pesa iko PayPal sasa hapo Crdb atarudishaje hela wakati iko kwenye acc yako ya paypal? Ni lazima wewe uhamishe pesa iliyoko PayPal kwenda bank kwasababu bank haina access na account yako ya paypal

Haujaelewa kabisa.. bila shaka wewe ni mmoja kati ya wale wanne. Mleta maada jaribu kutumia cash card ya bank ABC sijawahi kupata usumbufu wowote kwenye refund ingawa nao wana usumbufu kwenye kudeposit pesa kwenye kadi hasa kwa kuhamisha kutoka mpesa, hata ukienda mwenyewe bank kwa cashier ukadeposit inaweza kuchukuwa hata wiki hadi pesa zionekane
 
Haujaelewa kabisa.. bila shaka wewe ni mmoja kati ya wale wanne. Mleta maada jaribu kutumia cash card ya bank ABC sijawahi kupata usumbufu wowote kwenye refund ingawa nao wana usumbufu kwenye kudeposit pesa kwenye kadi hasa kwa kuhamisha kutoka mpesa, hata ukienda mwenyewe bank kwa cashier ukadeposit inaweza kuchukuwa hata wiki hadi pesa zionekane
Shida ya shule za kata kwani pesa amekwambia iko bank au paypal ? Na PayPal acc ni ya benki au mteja?
 
Mpaka ninavyoandika hapa ni returns za takribani Euro 400. Yapata miezi miwili sasa. CRDB International House nahisi ndio wanaosababisha kadhia hii kwa wateja. Kuna mtu amenishauri niumie Kado za Exim. Hawana usumbufu wa aina hii and kwa wateja.
Hata mi nafikiria kuhama ngoja wanilipe hela yangu kwanza........Benki imeanza kuwa ya hovyo kabisa yaani ukikaa kimya hela hairudi sasa kwanini Benki ikae na hela za wateja ambazo ziko directed kwenye akaunti ya mteja?
 
Tulia mkuu paypal ni gateway labda kama hukuelewa basi bado kuna nafasi ya kueleweshana tu.
Paypal ni gateway ndio kwani kabla ya kununua si unahamisha pesa kwenda PayPal then to seller? Na kwenye PayPal si ndo umemkabidhi pesa toka bank? Sasa hiyo acc ya PayPal benki inaijua? Benki ina access na akaunti yako ya PayPal? Were ndo unatakiwa kuhamisha tena pesa toka PayPal to bank account kama ulivyohamisha toka bank kwenda PayPal sio unalopoka kwakuwa una mb za kujitoa ufahamu JF
 
Natumia huduma ya kadi kufanya manunuzi online na kwa muda mrefu nimekuwa nikinunua vitu online kupitia paypal (gateway) lakini huwa inatokea muda mwingine nikanunua kitu halafu seller akashindwa kuleta nafungu kesi paypal na baadaye seller anaamua kunilipa (refund) lakini cha ajabu nikishalipwa na seller hela yangu huwa hairudi kwenye akaunti. Na mara nyingi nikirudishiwa hela paypal nao huwa wananitumia email kwamba nimerudishiwa hela na kwakuwa huwa nanunua kwa kutumia CRDB Visa Card hela yangu huwa inarudi kwenye akaunti yangu.

Hivi karibuni yapata kama mwezi mmoja na siku kadhaa hivi nilifanya transaction online ya $139.99 ambayo kwa hela ya kibongo ni kama 316,632 Tsh. Baadaye seller akasema kwamba ameishiwa na stock kwahiyo atarudisha hela yangu ili baadaye akiwa na bidhaa stock atanitaarifu nilipie tena. Baada ya siku tatu seller akanitumia meseji kwamba ameni-refund tayari na baadaye paypal wakathibitisha kwamba nimerudishiwa hela na imerudi kwenye akaunti yangu. Niliwasiliana na watu wa customercare kwa email nikawaambia juu ya suala hilo nao wakawasilisha kwenye Idara ya Refunds, baada ya hapo nikapokea email kutoka kwao kwamba niwatumie receipt ya refund hiyo kwa pdf nikafanya hivyo na nikawatumia na refunds zangu za nyuma ambazo kwa kipindi chote sikuwahi ziona kwenye bank statement yangu kama zimerudi.

Sasa cha ajabu tangu niwatumie hizo receipt hadi leo ni mwezi mzima hakuna mtu yeyote aliyetoa jibu kwamba nini kinaendelea, nimewaandikia emails zaidi ya saba hawajibu na nimewasiliana na watu wa customercare wanasema tatizo lako tumeliwasilisha wanalishughulikia. Lakini cha ajabu kwa kipindi hiki chote ninachosubiri kupata majibu kutoka kwao kuna harufu ya wizi naiona. Kuna thread kama hii niliisoma hapa kwenye jukwaa inaelezea jinsi wanavyoshirikiana kuzila hizo pesa za refunds kwa kugawana kuanzia kwa wakubwa wa vitengo hivyo ndio maana kwenye suala langu la kudai refunds zangu kuna kigugumizi kikubwa.

Najua kuna wengine wanaweza kuwa na experience kama hii nawaombeni mjitokeze hapa maana nafikiri hii siyo misingi bora ya utoaji huduma especially kwa Benki kubwa kama CRDB ambayo wateja wengi tunaiamini. Inaweza kuwa kuna watu wachache wanafanya hizo mambo na kuichafua Bank lakini nashangaa hata watu wa customer service nao kutojibu querry za wateja ni maadili ya kazi zao?
Hiyo benki ni ya wapigaji, nenda NBC,EXIM au STANDARD CHARTERED
 
Watu humu shule sijui tunaenda kufanya nini umesema umenunua kupitia PayPal na pesa iko PayPal sasa hapo Crdb atarudishaje hela wakati iko kwenye acc yako ya paypal? Ni lazima wewe uhamishe pesa iliyoko PayPal kwenda bank kwasababu bank haina access na account yako ya paypal
Hata direct refund za Visa haziendi kwenye akaunti. Nafikiri usiongelee kitu amabacho hukijui. Tuliokumbana na kadhia huyo tunajua tunachokiongeaa
 
Paypal ni gateway ndio kwani kabla ya kununua si unahamisha pesa kwenda PayPal then to seller? Na kwenye PayPal si ndo umemkabidhi pesa toka bank? Sasa hiyo acc ya PayPal benki inaijua? Benki ina access na akaunti yako ya PayPal? Were ndo unatakiwa kuhamisha tena pesa toka PayPal to bank account kama ulivyohamisha toka bank kwenda PayPal sio unalopoka kwakuwa una mb za kujitoa ufahamu JF
ngoja wengine wakujibu maana naona unatafuta kiki isiyo na sababu
 
CRDB in recent years ni kama wamebweteka kimtindo mm nliacha itumia maana nlikuwa nakuta madeni mtu wa saving a/c unambiwa una overdraft na hiyo hela ww ujawah iona na hata ukiomba bank taarifa zako za transaction wanakuzunguusha mpk unaona kero
 
Back
Top Bottom