CRDB Bank na kinachoendelea?

CRDB Bank na kinachoendelea?

Wameshiba wateja au na wao vifaa vipo kwenye meli
Mie sahivi nimehamia Exim sipendi hela yangu ya jasho initoe jasho kwenye kuila pia
mkuu exim ndio hovyo kabisa mm kwa atm nilikuwa naweza kutoa hadi 1.2M per day lakini sikuhizi wamenipiga pin mwusho laki 3 tuu, nimehamia crdb na sioni tatizo hilo la simbanking mwezi wa sita huu sada
 
Mimi mshahara wangu wapitia huko lakini sijapatwa Na tatizo la namna hiyo.!
 
Afadhali CRDB mara elfu kumi kuliko libenk linaitwa NBC linajifia lenyewe kabisa sasa hv.

Unaenda bank kuweka hela ukisikia tellers wanavyoongea hovyo na wateja, wanafanya kazi kama hawataki, wateja kibao teller wachache ni shida tupu. Unasimama mpaka unahisi miguu kuingia tumboni.

Siku moja wateja wakaja juu kushtaki kwa meneja mbona huduma inakuwa mbovu? Alichojibu meneja sasa; hiyo ndo huduma yenyewe nyie mnatakaje; hahaaaaa....

Kwenye biashara huria... Nilijifungia zangu account, nikatafuta tubenk tudogo dogo nikadondoshea huko tushilingi twangu🙁
 
mzunguko wa PESA kwa sasa ni MDOGO hivyo hakuna ,mifukoni ,katika vibubu HATA benk ktk ATM machine.
 
Siingii ATM simu banking inafanya kazi nahamisha pesa ktk mitandao ya simu kesi inaisha.!
Hiyo SimBanking inapatikana kwa kuvizia sana...ndani ya 24hrs inaweza ikawa hewani masaa matatu...ili kujua hili inahitaji watu wanaofanya transactions nyingi kama mimi...kama unatumia once kwa mwezi huwezi kuona tatizo
 
nmb wapo vizuri sana siku hizi....

top talent ya nbc na crdb wameibeba wao.. management ya nmb kali sana
 
Hiyo SimBanking inapatikana kwa kuvizia sana...ndani ya 24hrs inaweza ikawa hewani masaa matatu...ili kujua hili inahitaji watu wanaofanya transactions nyingi kama mimi...kama unatumia once kwa mwezi huwezi kuona tatizo
Aseeh kweli mkuu...mm leo nlifanya transaction mara kwanza nkaulizwa mbona haijaingia kuchek salio vile vile..nkafanya mara pili napo kimya..jioni hii kanipgia simu mbona umentumia mara 2..kuchek salio kweli wamekata mara 2
 
CRDB ni majanga.. hasa Simbanking na ATM zao.. kama ni ugonjwa ningeita KIFAFA kisichoisha..!! Haiwezekani kila siku mtandao uko chiniiii..!! Shida sana hawa...!!

Ukisema uende kutoa ktk bank foleni ndefu sanaa..!!

Wako vibaya sana kimtandao
 
Jamani mimi Crdb sina hamu nao, mwezi wa tatu mwaka huu karibia nishindwe kwenda kutoa mahari kisa network hakuna. Ilikua jpili Atm zote network haikuwepo kisha nikaenda branch ya mlimani city ndani nako system ilikua haisomi. Wakati huo nilikua natakiwa kwenda ukweni saa tisa mchana ikabidi nikope hela kutoka kwa jamaa zangu ili kuokoa jahazi.
Kuweni makini sana na hiyo bank jamani kwani inaweza kukuharibia mambo yako.
 
Wameshalewa sifa na wateja, kuna huduma nyingi wanaanzisha lakini hazina maintenance, yawezekana wameajiri watoto wao.
Kuna huduma kama E-statement, walikuwa wakituma kwenye email sasa hivi wakiamua wanatuma na wasipoamua hawatumi yaani full ubabaishaji. Mfano walituma mwezi Octoba wakatuma tema mwezi April mwaka huu. Na hiyo miezi ambayo hawatumi wala hawatoi maelezo kwa nini. Ikifika weekend ATM zote hazina hela. Shida kwelikweli
 
Kwani huyo Kigogo wao bado ana muda gani pale CRDB kabla ya mkataba wake kwisha? Isijekuwa kuna rival financial institution/bank ambayo kwa kujua kwamba huyo Kigogo aliyepo anakaribia kumaliza mkataba wake ikaamua kumtumia kwa makubalino maalumu kufanya sabotage kwenye hiyo bank katika kipindi chake hiki cha lala salama. Uaminifu wa kudumu ni nadra sana.
 
Naipenda CRDB,isipokuwa kuna siku nilifanya malipo kwa njia hii sijui mnaita TT,nilijuta masaa arobaini pesa haijahama,mhindi kagoma kunipa mzigo,nawafuata pale Lumumba, wananiambia na wao hawaelewi,duuh! Hapo natakiwa niwahi kurudi mkoa,Ratiba yangu yote ilivurugika,kwa hasira nika cancel transaction, nikachukulia ndani, nikasema potelea mbali wazee wa boxer wakinipa chai, 'usijaribu kufanya malipo kutoka crdb kwenda banks zingine kama una haraka.
 
Hawa jamaa wanakera sana..Hakuna maelezo... Hata kwenye ATM zao kwa siku za hivi karibuni wamekuwa wakiweka note za 5000 tu.. elfu kumi hakuna
Hao kawaida yao,
Kila ikifika saa 12:30 jioni ,lazima network ikate.
Hiyo ina daily routine
 
Humu zimejaa propaganda tu,kila mtu anasema analojiskia and what i see is hatred and misinformed minds.
Tukiongelea benki ambayo ina wigo mkubwa zaidi wa bidhaa za zenye uhitaji wa moja kwa moja kwa mteja huwezi kuiacha CRDB.Kwa Benki hasa ukizingatia benki halisi za kitanzania na pengine za kigeni,ipi inafanya vyema katika innovation ya service delivery channels kama CRDB?
Achana na logic ya kizamani ya kusema unajenga tawi kila wilaya kama NMB which is getting old as time goes,kwanini hamkiri Service centers/Agencies lukuki zilizopo karibia wilaya zote na tena kuna wilaya zinafika hadi tano plus za CRDB Microfinance.Mawakala wa Fahari Huduma zaidi ya 1000 nchi nzima,Internet Banking,Sim Banking etc lakini bado watu mnatumia akili finyu kung'ang'ana na mere complaints mara ATM zina shida.People here are too arrogant to switch to better and mobile services ends wanakalia kulalamika tu.Labda nnachoweza kukiri kwa mwezi huu ulioisha sababu Benki ime-upgrade its core banking system ndio maana kulikuwa na multiple cases za kusua sua sababu ya ile migration process ambacho ni kitu cha kawaida.People,mara nyingine tujifunze kutumia alternatives nyingine ambazo tunapewa kurahisisha maisha kuliko kung'ang'ana na mazoea yale yale ambayo ndo yanafanya mnalalamika.Sikuhizi CRDB ukiwa Dar kwa mfano,sio lazima ukapange foleni kwenye Branch kubwa sababu kwa Dar tu kuna Service centers kibao ambapo unaweza deposit,withdraw,loan processing,mentioned them all..
Tuache kulalamika,tuappreciate penye ukweli lkn pia tusisahau na mazingira yetu.Maana haya haya tunayolalamikia,mara nyingine ht kwenys familia zetu kwa level kuna ambayo hayako sawa kabisa and still u can blame yourself simply because you have one big reason as to why those faults can drag u down to failure.
Mtazamo wangu..
 
Wameshalewa sifa na wateja, kuna huduma nyingi wanaanzisha lakini hazina maintenance, yawezekana wameajiri watoto wao.
Kuna huduma kama E-statement, walikuwa wakituma kwenye email sasa hivi wakiamua wanatuma na wasipoamua hawatumi yaani full ubabaishaji. Mfano walituma mwezi Octoba wakatuma tema mwezi April mwaka huu. Na hiyo miezi ambayo hawatumi wala hawatoi maelezo kwa nini. Ikifika weekend ATM zote hazina hela. Shida kwelikweli
Tell us on the other hand which bank has been perfoming this consistently and perfectly?
Statement ya mwezi wa Jan,Feb,April zote nnazo..
Cry cry babies
 
Back
Top Bottom