Corona hakuna nchini, lakini majirani zetu wanayo

MIGNON

JF-Expert Member
Nov 23, 2009
4,083
5,066
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu.

Jambo moja ambalo binafsi sikubaliani nalo ni hili la kuweka matumaini makubwa katika dua na maombi na kuanza kulegeza taratibu zingine za kujikinga. Duniani wanaoathirika na Covid wengine ni wacha Mungu kuliko hata sisi na hatuna ubora wa kiimani kuliko wao.

Naamini ya kuwa mafanikio makubwa tuliyopata mwaka jana pamoja na hizo dua na maombi ni kuanza kuchukua hatua mapema kuhamasisha watu kwa kupitia njia mbalimbali.

Ugonjwa upo South Africa, Malawi, Kenya na Uganda achilia mbali Burundi na Rwanda na kwa mantiki hiyo ni suala la muda tu.

Serikali iendelee kutangaza kuwa hakuna Covid-19 lakini irudishe uhamasishaji wa kujikinga. Barakoa katika public places (hasa daladala) iwe lazima, vifaa vya kunawia mikono sehemu za biashara virudishwe, shule zote taratibu za awali ziwekewe mkazo.

Kwa kuwa ugoNjwa umeonyesha kuwa na athari kubwa kwa watu walio na magonjwa mengine (co morbidity kama kisukari, Pressure na HIV), kliniki za magonja haya ziwekewe utaratibu mzuri.

TANZANIA KORONA HAKUNA ILA KWA JIRANI IPO!
 
Ukweli ni kuwa tumekuwa kama kuku aliyrkimbizwa sana, baada ya kuchoka ameamya kuingiza kichwa kwenye kichaka ili asione anayemkimbiza, akiamini kuwa kwa kuwa yeye hamwoni anayemkimbiza basi na anayemkimbiza hamwoni, wakati amerahisisha kukamatwa kwake.

Corona ipo, watu wanaugua, watu wanapoteza maisha. Chukua tahadhari zote za kujikinga.
 
Umejuaje uchamungu wao au kwakuwa wanavaa majoho na kushinda mazahabuni?

Hujapata kusikia kisa cha IMAMU anakwenda MOTONI mlevi mnzinzi anaingia PEPONI

Ninachofahamu TANZANIA CORONA na AFRCA kwa ujumla tushaumwa na miili yetu imejijengea kinga madhubuti ya ugonjwa huo hvyo huo ugonjwa si tishio tena kwetu na kuna memba mmoja alielezea kwa kina hasa kwann tumeweza kuishinda CORONA sifa kwa kiasi zimuendee JPM japo alifanya hatua ya hatari kuacha usambae kwa kila mtu lakini matokeo yake ni bora kwa kila mtanzania anayependa Famiria yake na maisha yake.

Hvyo Pongezi zinakwenda kwake nyingi kwa kuzuia LOCKDOWN ambayo imekuwa tiba bora zaidi kwa kutuwezesha watanzania kujenga IMMUNE SYSTEM imala kabisa ya kuishinda CORONA.

CORONA si THREAT tena kwetu watanzania amini hivyo mkuu

Naandika haya mm nikiwa mmoja wapo wa tulioathirika na dalili zote za CORONA kati ya MARCH 2020 mpk JUNE 2020 nilipopona kabisa dalili zote za COROBA kwa kutumia mitishamba mbalimbali na PANADOL.
 
Ugonjwa upo. Watu wanaugulia majumbani. Walioko mahospitalini ni wengi na taarifa hazitolewi. Mwenye kupona na apone. Mwenye kufa ni bahati mbaya. Tunategemea "herd immunity".
 
Umejuaje uchamungu wao au kwakuwa wanavaa majoho na kushinda mazahabuni?

Hujapata kusikia kisa cha IMAMU anakwenda MOTONI mlevi mnzinzi anaingia PEPONI..
Kuna kitu kinaitwa "pre conceived ideas" na hiki ulikuwa nacho ulikuwa unasubiri mahali pa kutolea.

Nisome vizuri unielewe na kama kawaida ya Waafrica kama shida haipo kwako basi sio shida tena, sad!

Wewe ulipona mbona huzungumzii waliokufa na kuacha familia?
 
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu.....
Nchi ya kishenzi hii! Corona katika epidemiology ina tofauti gani na Malaria, TB and other infectious diseases, kuna siku itatangazwa kuwa hatuna malaria... wakati tumezungukwa na malaria kwa majirani
 
Ugonjwa upo. Watu wanaugulia majumbani. Walioko mahospitalini ni wengi na taarifa hazitolewi. Mwenye kupona na apone. Mwenye kufa ni bahati mbaya. Tunategemea "herd immunity".
Kweli kabisa. Ugonjwa upo, kikubwa kuzingatia maonyo ya wataalamu wa afya, kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.
 
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu....
Tanzania kuna Nimonia tu basi
 
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu...
Ulipima watz wote ukaambiwa conona imeisha?
 
Mwandishi! Hivi hujawahi kuona ama kusikia kwamba, Basi la abiria lilikuwa na abiria zaidi ya 60 likapata ajali watu wakafa na akanusurika mmoja tu???

Unadhani aliyebaki ktk ajali hiyo, yeye ndiye mcha Mungu kuliko hao 59 waliokufa??

Mawazo ya Mungu si kama mawazo ya wanadamu, Elewa Sana hii mkuu!!

La mwisho, Sisi ni mazao ya Mungu, itakapomfaa yeye kutuvuna, atachagua aanzie wapi na amalizie wapi, ni yeye mwenye shamba lake, hatuwezi kumlaumu kwamba Kwa nini Tanzania havuni Wakati ni muda wa kuvuna?
Eti kwa nini kwengine anavuna kasoro kwetu na Wakati nasi tu kama wao!!

Yeye kaamua kuanzia huko, ikimpendeza ataivuna Tanzania kwa Wakati wake

Shika Hilo na unyamaze na Usiandike tena mambo ya korona!!
 
Kazi na sala.
Miongozo wizara ya Afya kuhusu kujikinga ipo. Wewe usijali, jiachie uone utakavyoaga.
Magonjwa hayachagui.
Hii kitu ipo.
Haiitaji siasa kulinda maisha.
 
Imani ndivyo inataka hivyo! Magufuli anaishi kwa Imani, ana mwamini Mungu wake na ndivyo Mungu anavyotaka. Imani haitaki uangalie mwingine anafanya nini! Kiufupi Imani inataka uwe kama mwendawazimu fulani hivi
 
Kuna kitu kinaitwa "pre conceived ideas" na hiki ulikuwa nacho ulikuwa unasubiri mahali pa kutolea....
Kufa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu
Hata wanasayansi wanatambua seli za mwili zikianza kufa basi kikomo cha maisha yako kinakaribia hakuna namna
Hakuna atakayekimbia KIFO
Ila Kulinda afya yako ni jukumu lako namba 1 na familia yako watu zako hivyo unapaswa ufanye vyovyote kuilinda AFYA yako na familia yako
Mimi na Magufuri Tumechagua njia hii kulinda afya ya familia zetu na kutafuta ridhiki pia
Wewe vaa BARAKOA tembea na SANITIZER kaa mbari mita 1 nawa na maji tililika kila unapoingia sehemu au kutoka
jipige LOCKDOWN na familia yako MIEZI 6 na Mwaka huu acha upite peleka watoto wako shule mwakani kuwakinga na CORONA
Hujakatwaza mkuu fanya hayo yote wala huvunji sheria hiyari yako
 
Back
Top Bottom