Corona: Bila kupeana makavu hatutoboi, kwako mzee baba

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,860
Kwako Rais wetu mpendwa, jembe letu la ukweli, mzee baba, Dr. Magufuli.

Protokali yote imezingatiwa.

Mengi yameandikwa, shauri mbalimbali zimetolewa tangia kabla sana ya ugonjwa huu kuingia nchini takribani miezi miwili sasa.

Ugonjwa uliopaswa kuzuiliwa kuingia, uliingia nchini. Pia ugonjwa uliopaswa kudhibitiwa usisambae haujadhibitiwa na unaendelea kusambaa.

Haitusaidii kuendelea kuoneana aibu. Haitusaidii kuendelea kuficha maradhi. Wala haitusaidii kuacha kuelezana ukweli wazi wazi kwa maana msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Hadi tulipofikia naamini tunakubaliana sote kuwa hatuna jipya tena tokea kwa watendaji wetu waliopewa jukumu la kuudhibiti na hata kuutokomeza kabisa ugonjwa huu kutoka hapa nchini.

Mengine yote ni historia au yatokanayo na historia hiyo.

Mzee baba, tunakupenda sana na ni nia yetu sisi tunaoamini kuwa tu wengi, uendelee kutuongoza ikibidi hata baada ya 2025. Ila mheshimiwa, kwa sasa tunakuomba wewe mwenyewe ulione hili pamoja nasi kwa dhati kabisa:

Mzee baba, tunakuomba tujadiliane mbinu mpya za kupigana katika vita hivi mapema kabla hatujashindwa kabisa.

Tunakuomba mzee baba, iundwe tume nyingine yenye madaraka kamili ya kuongoza vita hii kama itakavyoona yenyewe kuwa inafaa. Ufanisi wake upimwe kwa vigezo vilivyo wazi.

Ni jambo la heri tu mkuu kuwa, wapo wana wa nchi hii wengi tu na wenye uzalendo uliotukuka, wanaoweza kukusaidia kuondosha gharika hili na kulitokomeza kabisa.

Mzee baba, tunayo nafasi ya kurejea katika maisha yetu ya kawaida (na mashule hata yakafunguliwa) ndani ya siku 45 tukiwa salama.

Kwa nini tusijipe nafasi katika kufanikisha jambo hili lenye tija kuu kama hili kwa nchi yetu?

Ni wazi kuwa, kuna maisha mengi yatakayookolewa kwa jitihada kama hizi, ambapo itakuwa ni thawabu kubwa kwako hapa duniani na hata huko mbinguni.

Eeeh mzee baba, hebu yaone haya kwa moyo mweupe, ukayajaribu.

Kwa hakika hautajilaumu.

Ninawasilisha.
 
Ndiomana unaambiwa kaa nyumbani Kama huna ishu yabmaana nje pila vaa mask muda wote na nawa mikono kwa maji tiririka izo ndio njia za kisayans zinazoweza kupunguza maambukizi na Sio kufungulia watu ndan

Sent using Jamii Forums mobile app

Huko ulaya na marekani wameshindwa kukaa ndani walipokuwa hawana issue au kunawa nawa mikono na maji tiririka?

RC yule alisema "sijui ni sharti lipi nimeshindwa kulitimiza".

Sembuse sisi na madaladala, masoko, ferry nk?

Tuacheni mzaha na mambo serious.

Mzee baba anao ufunguo wa kutanzua hili. Tumpe moyo mzee baba kuutumia.
 
Mkuu mbona yanatosha sana. Akiridhia haya ndani ya siku 45 tuko vizuri. Corona yote kwishney!

Hayawezi kuwa mabichi haya.
Tuongeze na kuvaa face shield
IMG_20200511_214042.jpg

Cc. FRANCIS DA DON
 
Watu mnasubili muongozwe kama punda husipochukuwa tahadhari msaada wake kwako ni kukuletea watu wa almashauri wakuchimbie futi sita kwenda chini
 
Kila ugonjwa ukitaka uundiwe tume tutakuwa na matume mangapi? Jifunzeni kuishi na corona kama tunavyoishi na malaria, corona will be there forever, kumbuka hata malaria inaua kila siku
 
Nakusoma unaitakia mema nchi, Kwa tulipofika unahisi nini kifanyike hebu pendekeza njia za kufanya, ukiacha hii slogan ya kunawa kuvaa barakoa na kukeep distance?
 
Kila ugonjwa ukitaka uundiwe tume tutakuwa na matume mangapi? Jifunzeni kuishi na corona kama tunavyoishi na malaria, corona will be there forever, kumbuka hata malaria inaua kila siku

Kuna tofauti nyingi kati ya Corona na magonjwa mengine yakiwamo malaria.

Tofauti mojawapo ya Corona na wengine if you like, ni kuwa haina tiba waka chanjo.

Tume huundwa kwenye dharura. Hivi sasa tuna mashule yamefungwa. Waliounda tume za maana kama hizi kwenye hoja wanaelekea kufungua mashule.

Huna habari hata hapa zipo tume 3 za Corona peke yake?

Au wewe uko dunia ipi?
 
Watu mnasubili muongozwe kama punda husipochukuwa tahadhari msaada wake kwako ni kukuletea watu wa almashauri wakuchimbie futi sita kwenda chini

Si kweli mkuu. Mzee baba ana wajibu zaidi ya kukuletea wachimba kaburi.

Wanaougua au kufa kwa ugonjwa huu si kwa ujinga au uzembe wao.
 
Alie kuambia ulaya wanakaa ndan ndio ulitakiwa umlaum Mana kakujaza ujinga
Huko ulaya na marekani wameshindwa kukaa ndani walipokuwa hawana issue au kunawa nawa mikono na maji tiririka?

RC yule alisema "sijui ni sharti lipi nimejifunga".

Sembuse sisi na madaladala, masoko, ferry nk?

Tuacheni mzaha na mambo serious.

Mzee baba anao ufunguo wa kutanzua hili. Time moyo kuutumia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna tofauti nyingi kati ya Corona na magonjwa mengine yakiwamo malaria.

Tofauti ya Corona na wengine if you like, haina tiba waka chanjo.

Tume huundwa kwenye dharura. Hivi sasa tuna mashule yamefungwa. Waliounda tume za maana kama hizi kwenye hoja wanaelekea kufungua mashule.

Huna habari hata hapa zipo tume 3 za Corona peke yake?

Au wewe uko dunia ipi?
Kama unategemea tume mbele ya jiwe niseme tu ni heri ukasubiri meli airport yaweza tia nanga lkn si tume, ila Kama una mapendekezo nje ya lockdown, yaweke mezani serikali yaweza fanyia kazi ushauri wako
 
osho. Tuate pKwa kuwa njia zote za ulaji zishajifungo basi nadhani weye umeamua kubahatisha angalao utumie tume hii ya 4 ya corona angalao upate posho. Hakuna tume wala mtume. Hela iliyokuja ni ya kumalizia sgr
 
Kama unategemea tume mbele ya jiwe niseme tu ni heri ukasubiri meli airport yaweza tia nanga lkn si tume, ila Kama una mapendekezo nje ya lockdown, yaweke mezani serikali yaweza fanyia kazi ushauri wako

Mkuu zipo tume 3 zinazopambana na Corona. Hizi tokea nyakati tofauti zikiwamo kabla ya kuingia ugonjwa.

Hoja iko wazi:

"Tunakuomba mzee baba, iundwe tume nyingine yenye madaraka kamili ya kuongoza vita hii kama itakavyoona yenyewe kuwa inafaa. Ufanisi wake upimwe kwa vigezo vilivyo wazi."

Pana tofauti katika hii. Hii ni tume kamili ya vita yenye mamlaka: council of war. Yenye kupimwa utendaji kwa vigezo vya wazi.

Bottom line maambukizi yanasimamishwa within a time frame.
 
Back
Top Bottom