Corona: Baada ya kushinda vita hakuna hata wa kutupongeza?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,860
Ama kweli raha jipe mwenyewe. Ukisubiri mwingine kukupa raha, mbona waweza kusubiria mno?

Tumetangaziana kwa bashasha kuwa tumeshashinda vita. Wagonjwa wamekuwa wakipungua tokea mamia hadi mamoja. Haiyumkiniki kwa mwendo huo kufikia sasa, si haba Corona itakuwa kwishney!

Vita hii si ndogo kwani wenzetu wengi hata walio washupavu mno kuliko hata sisi wangalimo bado kulia wala kushoto kungali kufahamika.

Cha ajabu na kweli katika mazingira ya kawaida ushindi huwa haukosi pongezi tokea kwa washirika yaani ndugu na marafiki.

Sasa huu ushindi wetu usiokuwa na pongezi tokea kokote isipokuwa chereko chereko za kivyetu vyetu peke yetu na mh. Makonda tu utakuwa ushindi wa namna gani huu?

Hatuna washirika kweli hata wa kukodi tu? Hata Burundi ambako rais wao mteule atakuja kututembelea sisi kama priority 1 wameshindwa kutupongeza hata kwa kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa na tuko vizuri tu?

Kwa mwendo huu, pana hatari kuwa ushindi wetu huu unaweza kuwa na walakini au wa kimagumashi kama kwingine wanavyoita. Waswahili wanasema "hala hala kabla ya hatari".

Haya mengine ya kuitana majina kuwa ooh pana watu walipenda watanzania wafe kama nzige mbona itakuwa kujaribu kujishasha tu ili kujaribu kuzima mawazo huru pasipo kuwa na hoja?

Kwa nini mtu awe na maslahi yoyote kwa watanzania kufa? Kwanini isiwe kwa warundi, wacongo, wasauzi, wajamaica, wajerumani nk kufa? Kwa nini hakuna nchi yoyote ile duniani yenye mawazo kama haya? Mawazo duni kabisa.

Tupende tusipende, pana vitu (na si kidogo) upande wetu na hii vita haviko sawa hata kidogo.

Pasipo na kupepesa maneno, ushindi huu tunaojinasibu nao utakuwa uko fyongo.
 
Ushindi wa ccm unajulikana, uchakachuaji, na hila za jecha. Korona inafanywa kwa mtindo huo huo!
 
Tulia wewe. Fanya kazi mambo,ya kutishana tishana tz hatutaki. Mbona hata malaria still inaua watu kibao Africa na visa vya maambukizi yake havitangazwi.
 
Ama kweli raha jipe mwenyewe. Ukisubiri mwingine kukupa raha, mbona waweza kusubiria mno?

Tumetangaziana kwa bashasha kuwa tumeshashinda vita. Wagonjwa wamekuwa wakipungua tokea mamia hadi mamoja. Haiyumkiniki kwa mwendo huo kufikia sasa, si haba Corona itakuwa kwishney!

Vita hii si ndogo kwani wenzetu wengi hata walio washupavu mno kuliko hata sisi wangalimo bado kulia wala kushoto kungali kufahamika.

Cha ajabu na kweli katika mazingira ya kawaida ushindi huwa haukosi pongezi tokea kwa washirika yaani ndugu na marafiki.

Sasa huu ushindi wetu usiokuwa na pongezi tokea kokote isipokuwa chereko chereko za kivyetu vyetu peke yetu na mh. Makonda tu utakuwa ushindi wa namna gani huu?

Hatuna washirika kweli hata wa kukodi tu? Hata Burundi ambako rais wao mteule atakuja kututembelea sisi kama priority 1 wameshindwa kutupongeza hata kwa kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa na tuko vizuri tu?

Kwa mwendo huu, pana hatari kuwa ushindi wetu huu unaweza kuwa na walakini au wa kimagumashi kama kwingine wanavyoita. Waswahili wanasema "hala hala kabla ya hatari".

Haya mengine ya kuitana majina kuwa ooh pana watu walipenda watanzania wafe kama nzige mbona itakuwa kujaribu kujishasha tu ili kujaribu kuzima mawazo huru pasipo kuwa na hoja?

Kwa nini mtu awe na maslahi yoyote kwa watanzania kufa? Kwanini isiwe kwa warundi, wacongo, wasauzi, wajamaica, wajerumani nk kufa? Kwa nini hakuna nchi yoyote ile duniani yenye mawazo kama haya? Mawazo duni kabisa.

Tupende tusipende, pana vitu (na si kidogo) upande wetu na hii vita haviko sawa hata kidogo.

Pasipo na kupepesa maneno, ushindi huu tunaojinasibu nao utakuwa uko fyongo.

Achana na siasa Jamaa COVID19 yupo na anafanya kazi kwa kasi sana hadi wa watoa takwimu wameshindwa kutoa takwimu, wamebaki tu kutoa takwimu za nchi nyingine, utafikiri Tanzania ni kisiwa ambacho hakina maingiliano na watuwengine.
 
tulia wewe ..fanya kazi mambo,ya kutishana tishana tz hatutaki..Mbona hata malaria still inaua watu kibao Africa na visa vya maambukizi yake havitangazwi
Miezi mitatu tumeshapoteza watanzania karibu 1000.Meko corona ikimfyekelea mbali akili zitawarudia.
 
Mabeberu yana wivu sana

Mabeberu hayo yawaonee wivu watanzania tu dunia yote hii? Kwa lipi?

Ndiyo maana hata wa kutupongeza hamna na tunajiaminisha sisi tuko sahihi Ila wengine wote?

Ilikuwa ni kitendo cha maendeleo sana kustuka na kijiangalia wenyewe kwanza kama kweli tungali hata tuna mawazo yoyote ya kibinadamu tu yaliyo bakia.
 
Ama kweli raha jipe mwenyewe. Ukisubiri mwingine kukupa raha, mbona waweza kusubiria mno?

Tumetangaziana kwa bashasha kuwa tumeshashinda vita. Wagonjwa wamekuwa wakipungua tokea mamia hadi mamoja. Haiyumkiniki kwa mwendo huo kufikia sasa, si haba Corona itakuwa kwishney!

Vita hii si ndogo kwani wenzetu wengi hata walio washupavu mno kuliko hata sisi wangalimo bado kulia wala kushoto kungali kufahamika.

Cha ajabu na kweli katika mazingira ya kawaida ushindi huwa haukosi pongezi tokea kwa washirika yaani ndugu na marafiki.

Sasa huu ushindi wetu usiokuwa na pongezi tokea kokote isipokuwa chereko chereko za kivyetu vyetu peke yetu na mh. Makonda tu utakuwa ushindi wa namna gani huu?

Hatuna washirika kweli hata wa kukodi tu? Hata Burundi ambako rais wao mteule atakuja kututembelea sisi kama priority 1 wameshindwa kutupongeza hata kwa kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa na tuko vizuri tu?

Kwa mwendo huu, pana hatari kuwa ushindi wetu huu unaweza kuwa na walakini au wa kimagumashi kama kwingine wanavyoita. Waswahili wanasema "hala hala kabla ya hatari".

Haya mengine ya kuitana majina kuwa ooh pana watu walipenda watanzania wafe kama nzige mbona itakuwa kujaribu kujishasha tu ili kujaribu kuzima mawazo huru pasipo kuwa na hoja?

Kwa nini mtu awe na maslahi yoyote kwa watanzania kufa? Kwanini isiwe kwa warundi, wacongo, wasauzi, wajamaica, wajerumani nk kufa? Kwa nini hakuna nchi yoyote ile duniani yenye mawazo kama haya? Mawazo duni kabisa.

Tupende tusipende, pana vitu (na si kidogo) upande wetu na hii vita haviko sawa hata kidogo.

Pasipo na kupepesa maneno, ushindi huu tunaojinasibu nao utakuwa uko fyongo.
Hujasikia Ufaransa kupitia Balozi wao nchini?
 
Back
Top Bottom