ni kitu gani kipya mtu unaweza kufanya leo ambacho hakuna mtu duniani amewahi kukifanya...IMO, kuiga si tatizo kwani huwezi leo kuja na jambo jipya kabisa hapa bongo ambalo halipo duniani hasa kwenye TV business.
tatizo ni kuiga halafu ukashindwa kuboresha kiasi cha kumpita unayemuiga kwani kwa kufanya hivyo..watu hawatovutika sana b'se watahisi hawaoni cha mno cha kuwavutia.
mheshimiwa mmoja hapo amedai kuwa ukiangalia EATV ni kama unaangalia TV za mbele...subconciously anasema kuwa EATV wameweza kuiga channel za mbele kiasi ukiitazama unajihisi kama unaangakia channel ya mbele!
kwa hiyo wandugu, msitokwe na mapovu kuwashambulia hao wafu station...kuiga kupo tu, hata we hapo ulipo umevaa pengine, jinsi, suti na tai etc..umeiga, maana tukisoma historia ya kwenu si ajabu tukakuta kwenu kwa asili walikuwa wakivaa vibwaya kama komredi kipepe wa gazeti la sani.
hahaaa hii imenikumbusha huu wimbo wao walioimba kina mchovu na wenzake unaohusu fiesta,wameimba kama wamarekani yani hamna kitu ni ujinga tuu...sometimes ni vizuri kuwa real.
Tuwe objective katika ku-critic ni kweli kwamba wamekopy na kupaste lakini unashauri nini? Mimi binafsi nawapongeza CLOUDS kwa sababu ni wachache sana wenye uthubutu na ni mfano bora kwa vijana wenye kiu ya mafanikio. Nikiri hawa jamaa wanajitahidi sana na naamini wataleta ushindani mzuri. Kuhusu EATV ukijaribu kuangalia nao kwa kiasi fulani wameiga mpangilio wa programu zao channel O. Na hakuna anayebisha, hata hivyo kwa sasa EATV wako hatua ya mbali ingawa sidhani kama wanagenerate revenues kutoka nchi nyingine za Afrika Mashariki pamoja na kwamba lengo lao ni kuteka soko la Afrika Mashariki. Hata hivyo safari bado ni ndefu. Tujiangalie wenyewe kwanza ndipo tuangalie wengine. CLOUDS na EATV kazeni buti nyinyi ni watanzania mafanikio yenu yanaiwakilisha Tanzania.
ubunifu ni kitu pekee kinachoweza kuitofautisha brand moja hadi nyingine/kampuni nyingine ambazo/yo inatoa huduma zinazolingana/fanana.
Nirudi kwenye topic,sina shaka na uwezo wa clouds media Group katika ubunifu na mambo mengine linapokuja suala la burudani hapa Tanzania, ila kwa hili niseme Clouds TV wamekosa ubunifu na walichoishia kufanya ni kukopy na kupaste vipindi vyao kutoka TV stations nyingine mfano EATV.Vifuatavyo ni baadhi ya vipindi ambavyo Clouds TV wamekopy na kupaste kutoka EATV....
1.Siz kitaa- City sound (kilichokuwa kikiendeshwa na Seki)
2.Take One-Bongo movie (kilichokuwa kinaendeshwa na Joyce Kiria).
3.Ongea na Janeth-The Mboni show (kinachoendeshwa na Mboni)
4.Wazee wa Madebe-Friday Night Live(kinachoendeshwa na Sam Misago).
5.kipindi cha Paradise cha Irene uwoya nayo ni programu ambayo inendeshwa na TV stesheni nyingi za nje katika mtindo wa documentary,lakini kipindi hiko kinafanana kabisa na kipindi ambacho hufanywa huko Nigeria na moja ya TV stesheni,so sio kitu kipya pia.
Mdau unaweza kuongeza vipindi unavyovijua ambavyo jamaa wamecopy ila si kwa nia mbaya.
Not all the times, always ni muhimu kuwa real...sasa wanajifanya wamarekani weusi ili iweje? Yaani wangejuwa jinsi wamarekani weusi wanavyochukia waafrika sijuwi wangefanyaje hawa panya buku?
unategemea nini toka kwa wahuni,wizi wanaita fursa..wauz sembe tu hao
Ha ha ha ha ha
Not all the times, always ni muhimu kuwa real...sasa wanajifanya wamarekani weusi ili iweje? Yaani wangejuwa jinsi wamarekani weusi wanavyochukia waafrika sijuwi wangefanyaje hawa panya buku?
Penye Ukweli unasemwa, Redio na Tv nimekuja gundua ni vitu tofauti sana,
Kama ambavyo EA Radio wanavyohangaika kushika namba na bado wameachwa mbali sana ndivyo na Clauds TV hivyo hivyo Wanapata shida sana kuwakamata EATV. Ingawa katika general performance ya Entertainment Industry bado Clauds wapo juu.
Hajaniniingia akilini fafanua hiyo kauli yako ya entertainment imdustry au na we umekurupuka kutoka kubwia unga nini?
Ataebisha hapa hana wivu ila ni MCHAWI haswaEntarteinment industry inajumuisha vitu vingi,matamasha,tv,radio,majarida ya burudan , ni industry kubwa ambayo ndan yake kuna vitu vingi ,sasa kwa hapa kwetu katika makampun yanayojihusisha nayo yale yaliyo chini ya Clauds media group ndo yanayoongoza ktk nyanja nyingi za burudan isipokuwa tu katika TV kama ambapo naona clauds tv imeshindwa kutake lead kama ambavyo vitu vingine toka clauds media group zinazofanya lead mf.radio clauds,coconut ,bang magazine,THT ,teentz ,primetime promotion (fiesta) etc etc etc
Huwa nawaona wapuuuzi tuu
kwa upande wa TV wakabidhi kijiti tu hakuna kitu kabisa pale. hakuna kipindi kinachonikera kama BIBI BOMBA.
kinakera kweli kweli.
Mi nakerwa na hao wanaopeleka mama na bibi zao wakadhalilike.
sasa ndugu kitengo cha creativity kinakuwa kinafanya nini?huwezi kuwa unacopy kutoka stesheni za hapahapa bongo na vipindi tunavifahamu halafu uje utuambie wewe ni creative au ndio kutumia fursa huko? Bac hata kama unaiga iga toka huko mbali na kiwe kipya hapa bongo ili wateja tuone kweli kitu ni kipya na kina mvuto kuanzia mpangilio hadi presenters