poul
Member
- Apr 21, 2013
- 56
- 17
Habari zenu wakuu
Kama kichwa kinavyosema, hivi hizi Cache na Cookies ni nini na zina kazi gani kwnye simu?
Pia kwanini wameweka hizi Cache na Cookies inakuaje mfano zisipokuwepo?
Nini kitatokea?
Simu itafanyaje yani au itapungukiwa nini hasa katika utendaji wake?
Faida kubwa Cache na Cookies??
Je unavyoambiwa clear cookie cjui enable cache au accept cache ndo nini, je ukiclear unafanya nini yani ple huwa unaboresha nini au unaharibu nini?
Je usipoziruhusu hizo cache au cookie?
Mkuu CHIEF MKWAWA naomba ufafanuzi juu ya hili na Wadau wengine pia naomba msaada wenu ili nipate uelewa sahihi maana napenda nikiwa nafanya kitu nijue nafany nini
NAWASILISHA
Mi sijuagi maskini
1. Cookies (vibiskuti) - ni vifaili vidogo ambavyo hutumwa na tovuti unayoitembelea kwa wakati huo kwenda kwenye kifaa unachotumia, kama ni simu ya mkononi, tabiti, au kompyuta yako kupitia browser yakoumuhimu wake...vinasaidia kukusanya taarifa na kuwasaidia wenye tovuti kujua ni watumiaji wangapi wametembelea tovuti yao, pia inaweza saidia kujua ni vifaa vipi hutumika zaidi kufungua mtandao wao,
2. Cache: hii ni kumbukumbu ambayo huwekwa na browser yako kwa kila tovuti unayotembelea, ili wakati mwingine utakapofungua tovuti hiyo au ukurasa huo iwe rahisi kufungua (itachukua muda mchache kufungua cached page kuliko ukurasa mpya)hasara ya cache: kama pc yako ina nafasi ndogo ya kuhifadhi mafaili , cache inawea kuchukua nafasi kubwa sana na itabidi ku clear mara kwa mara.
3. cookies na cache zinaweza kuwa disabled kama hupendi kufuatiliwa habari zako,
4. chukua muda wako kujifunza mabo mbali mbali kupitia google, itakusaidia sanacc poul
CACHE ni sehemu ya kuhifadhi files kwa mda fulani kwenye device yako, kwa mfano kwenye browser inatumika kuhifadhi vitu kama picha za website unazotembelea localy e.g ukifungua jf kwa mara ya kwanza logo ya jf inakuwa downloaded na kuhifadhiwa kwenye cache so ukienda page nyingine ya jf browser inakuwa haina haja ya kuidownloa logo hiyo hiyo ambayo haijabadilika badala yake inaichukua katika cache, hivyo inapunguza matumizi ya data na kuifanya site ionekane fast zaidi.
Cookies ni text files ambazo website inahifadhi katika devic yako ili kuweza kukutambua baadae, kwa mfano unapologin JF na kuchagua remember me, jf inahifadhi file kwenye device yako ambayo ni unique kwako, so next time unaenda jf inaisoma hiyo file na kukulogin automatically bila ya kuwa na haja ya kuandika username/ppassword tena. Pia site zengine zinatumia cookies kukufuatilia mtandaoni kwa jili ya vitu kama matangazo so unaenda Amazon kwa mfano unaangalia viatu, then unaenda site nyingine kabisa lakini unaona kuna matangazo ya viatu kutoka Amazon, hiyo ni tracking ambayo moja ya njia za kuifanya ni cookies.
Hakuna sababu ya kudelete cache unless umeishiwa nafasi au unataka kuondoa rekodi ya site ulizotembelea, kwa mfano ukienda site ya ngono kutakuwa na picha za ngono kwenye cache yako hata kama haukuzisave mwenyewe. Otherwise ukidelete cache sana sana utapunguza spidi ya browser na kuongeza matumizi ya data Kwa sababu kila kitu kinabidi kiwe downloaded upya.
Cookies kuna umuhimu zaidi wa kuzifuta kwa kuwa ni tatizo kwa privacy yako kufuatiliwa na websites.