Confusion ya Marafiki, Please help!

Confusion ya Marafiki, Please help!

Ili kuwakomesha hao wanaokusema ni wewe kuendeleza tabia njema huku ukijitaidi kwa kadri uwezavyo kuwabadilisha wenzako wenye tabia hiyo isiyo nzuri(yakupendeza)
wakiona wanakusema ila wewe hutetereki na wala hauyafanyi wanayoyasema ni wazi wataazha kuchonga maneno.
hapo umenena rafiki......
hata waseme vipi kuwakomesha wewe baki na tabia yako nzuri, wenyewe wataacha kuchonga
 
.....urafiki una gharama za ki hisia ambazo unawajibika kulipa 'fadhila' ili kudumisha uhusiano wenu.
Kwa kila tabia mbaya ya unayomvumilia rafiki yako, inampasa naye akustahmilie tabia ya kwako mbaya.

mfano;
kama unajua rafiki yako anam cheat mkewe/mumewe, it's most likely nawe una multiple partners, la sivyo
wewe/yeye mmoja wenu anamkuwadia mwenzake.
sijui kwa nyie wakaka hii imekaaje....
lakini mimi kwa jinsi ninavyoona wadada wengi anaweza akacheat lakini hathubutu kumwambia best friend wake.... yaani huyo rafiki atasikia kwa watu tu kuwa rafiki yako anafanya hivi lakini siyo toka kwa mdomo wa rafikiye
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Unajua vitu vikitokea uchukuliwa ndio hivyo kwa watu wote japo kuna ukweli lakini watakao amini kama hizo tabia (mbaya)(nzuri)za rafiki yako wewe hutokuwa nazo au unazo.
Ukweli utabaki kuwa nao mwenyewe uku macho ya walimwenguyakibaki kukutazama
Ni kweli kabisa ukweli utabaki nao mwenyewe....... hii sentensi naipenda sana, ukweli naujua mimi, wengine mtaishia kuhisi tu
 
FP
Embu funguka masahibu gani yamekukuta dada angu?
ha haaa, utasutwa.... shauri yako....
kuna jamaa enzi hizo alinisingizia mambo fulani kwa watu, nilichukia sana na kwa sababu sikuwa na jinsi ya kuwathibitishia watu ukweli wa jambo, nikaishia kumwambia ukweli tunaujua mimi na wewe, hawa wengine waamini wanachotaka
 
ha haaa, utasutwa.... shauri yako....
kuna jamaa enzi hizo alinisingizia mambo fulani kwa watu, nilichukia sana na kwa sababu sikuwa na jinsi ya kuwathibitishia watu ukweli wa jambo, nikaishia kumwambia ukweli tunaujua mimi na wewe, hawa wengine waamini wanachotaka

Kiutu uzima nishaelewa
 
Lisa ameongea kweli tupu, ndege wanaofanana huruka wote, mtoa mada fahamu kitu kikubwa kinachowaunganisha nyie kuwa matafiki ni matengo ya tabia zenu kufanana hivyo huwezi kuwa na urafiki na mtu wakati tabia zenu hazifanani, labda uwe urafiki unakinafiki hapo kina mtu anaweza kuwa na tabia zake
 
Lisa ameongea kweli tupu, ndege wanaofanana huruka wote, mtoa mada fahamu kitu kikubwa kinachowaunganisha nyie kuwa matafiki ni matengo ya tabia zenu kufanana hivyo huwezi kuwa na urafiki na mtu wakati tabia zenu hazifanani, labda uwe urafiki unakinafiki hapo kina mtu anaweza kuwa na tabia zake
na wewe naomba uende ukawasome HorsePower na SMU uone walichoandika kwa kirefu sana
 
Last edited by a moderator:
mpendwa ukiambatana na mwizi nawe utakuwa mwizi, hivyo basi ukiambatana na mwenye tabia mbaya ile tabia mbaya nawe utakuwa na tabia mbaya, tabia huambukiza kwani ukiwa na mtu mwenye tabia nzuri na nawe utakuwa na tabia nzuri tabia inaambukiza na kujenga kitu katika moyo wa yule rafiki yako hivyo basi jua kuwa rafiki yangu tabia inaambukiza ningekupa andiko ila nimesahau nitatafuta nikupe siku ingine
be blessed
 
Nani mwenye mamlaka ya kuamua kuwa hii ni tabia mbaya na hii ni nzuri? Mimi nadhani ni wewe mwenyewe. Pili marafiki hawaji kwa bahati mbaya lazima kuna kitu mnaendana na kama wewe ni mbinafsi basi kuna kitu unatafuta toka kwao ndiyo maana wanakuwa marafiki zako.
Tatizo ni kwamba anayekuwa anajua ukweli huo ni wewe mwenyewe na watu wengine wanakuwa hawajui kwanini fulani ni rafiki yako na wanaanza kutumia vigezo vyao na kumwita huyu mzuri na yule mbaya. Binafsi nasema fuata utaratibu wako na kwa post zako hapa JF unaonaekana wewe ni mtu mzima yaani above 25. Kila la kheri
 
Mimi siamini katika hilo. Kuwa marafiki mwafanana tabia. But imeniweka pabaya kwa mpenzi wangu kwa sababu ya marafiki nilionao amekuwa haniamini kabisa.
Imenifanya nianze kupotezea urafiki for the sake of my love for him.
Hivi vitu ni vigumu sana na kuna wengine hata ukieleza vp hakuelewi.
 
kwa mtazamo wangu binafsi, siwezi kuiga tabia ya mtu kisa tupo marafiki..na kwa upande mwingine nikiwa na rafiki ana tabia fulani iliyopitiliza na hamna dalili akapunguza au kuacha basi nitamsaidia ajitahidi kubadilika!! Hii ni kwa rafiki niliyenae karibu ambaye uwepo wake kwangu nami kwake unaonekana na una thamani...
 
Inawezekana tatizo lako kubwa ni kujua maana ya rafiki FP. Kujuana na watu, kuongea nao na kuambatana nao hakuwafanyi kuwa marafiki. Marafiki ni mutual feeling, communal understanding. Hao unaosema wewe kuwa wanaweza kuwa na tabia mbaya ukawa nao ni watu tu uliowazoea kwa sababu mazingira na mazoea yamekufanya uwe nao katika muda fulani lakini kamwe si marafiki

Angalia wale watu (marafiki) unaowatafuta kwa mara ya kwanza unapokuwa kwenye matatizo (kwa kiinglish tunasema IN DEEP SHIT). Hao lazima mna tabia zinazofanana kwa kiasi fulani. Na hao ndio hasa marafiki zako.
 
Rafiki definition ya "Tabia mbaya" ni pana mno na ina differ kati ya watu na watu. Kwa mfano kuna watu wengine watakwambia Mama XYZ ana tabia mbaya sana, "Yule mama anaweza kwenda Bar na wanawake wenzake na wakakaa na kunywa bia zao." Hapa tabia mbaya ya Mama XYZ ni kwenda bar bila kufuatana na mumewe. Wengine wanaweza kukwambia yule Mama ABC ana tabia mbaya sana, "Anapenda kuva nguo za kisichana wakati ameshakuwa mtu mzima. Lazima atakuwa mhuni yule" Hapa tabia mbaya ya Mama ABC ni kuvaa nguo fupi juu ya magoti, kaptula, vimini, skin tight etc. Kumbe hizo nguo anazovaa mumewe ndiyo anapenda avae hivyo kutokana na umbo la mkewe basi yeye haoni tatizo la mkewe kupendeza.

Mama mwingine katika jitihada za kuongeza kipato anaweza kabisa kuwa anajiuza kwa namna anayoijua yeye ambayo si ajabu watu wengi wamemshtukia. Sasa Mama kama huyu kuambatana naye katika macho ya jamii ni kujiharibia reputation. Inawezekana kabisa muhusika anafuatana na mama huyu hajui tabia yake ya kujiuza lakini machoni jamii wote wanaonekana lao moja na si ajabu mama huyu akijua tabia ya rafiki yake anaweza kabisa kumuepuka.

Watu wengine wana ile tabia ya "Don't care attitude" hata kama jamii iliyowazunguka inasema fulani ana tabia mbaya na yeye anazijua kabisa tabia za huyu rafiki yake kwamba ni mbaya ali mradi kuna mambo ambayo wanaelewana basi anatia pamba masikioni na kuendelea na urafiki wao bila kujali jamii inayowazunguka inasemaje kuhusu hao marafiki kuwa na "tabia mbaya"

Marafiki wengine wanaweza kabisa kuwashawishi marafiki zao waachane na hizo "tabia mbaya" zao bila masharti yoyote yale na huku urafiki ukiendelea bila dosari yoyote ile.

Hebu fafanua hizi "tabia mbaya" unazozizungumzia hapa ni zipi? Ukiziweka hata mbili tatu utasaidia sana katika mjadala huu.

Sayonara Rafiki.




Jamani tumesalimika ndugu zangu?
Nina hili jambo huwa naliwaza sana na labda sielewi kwa nini watu wengi wana mtazamo tofauti na ninavyoamini mimi...
Ni hili swala la marafiki wa kuambatana nao (hapa naongelea marafiki wa kawaida tu na siyo wapenzi).
Watu wengi wanasisitiza sana watu wasiambatane na marafiki wenye tabia "mbaya" kwa sababu wanazozijua wao. na hili limenichanganya zaidi baada ya kulisikia jana kwa mtu ambaye sikutegemea angewaza hivi.
Mimi naamini unaweza kuwa na marafiki wenye hizo tabia na wewe usiwe/usiige hizo tabia zao.
Labda mimi sielewi mtu mzima unawezaje kuwa influenced na tabia ya mtu mwingine ambayo unaona siyo nzuri?


NOTE: HII NAONGELEA WATU WAZIMA AMBAO WANAJUA KUTOFAUTISHA JEMA NA BAYA, TUSIHUSISHE WATOTO KATIKA MJADALA HUU


 
mpendwa ukiambatana na mwizi nawe utakuwa mwizi, hivyo basi ukiambatana na mwenye tabia mbaya ile tabia mbaya nawe utakuwa na tabia mbaya, tabia huambukiza kwani ukiwa na mtu mwenye tabia nzuri na nawe utakuwa na tabia nzuri tabia inaambukiza na kujenga kitu katika moyo wa yule rafiki yako hivyo basi jua kuwa rafiki yangu tabia inaambukiza ningekupa andiko ila nimesahau nitatafuta nikupe siku ingine
be blessed
ladyfurahia, hapa kumbuka tunaongelea watu wazima na si watoto.
yaani wewe kama siyo mwizi umekuwa mtu mzima utakuwa mwizi sababu una rafiki mwizi?
labda nikuulize wewe na rafiki zako wote mnafanana tabia? hata zile nzuri tu
 
Last edited by a moderator:
Nani mwenye mamlaka ya kuamua kuwa hii ni tabia mbaya na hii ni nzuri? Mimi nadhani ni wewe mwenyewe. Pili marafiki hawaji kwa bahati mbaya lazima kuna kitu mnaendana na kama wewe ni mbinafsi basi kuna kitu unatafuta toka kwao ndiyo maana wanakuwa marafiki zako.
Tatizo ni kwamba anayekuwa anajua ukweli huo ni wewe mwenyewe na watu wengine wanakuwa hawajui kwanini fulani ni rafiki yako na wanaanza kutumia vigezo vyao na kumwita huyu mzuri na yule mbaya. Binafsi nasema fuata utaratibu wako na kwa post zako hapa JF unaonaekana wewe ni mtu mzima yaani above 25. Kila la kheri
haya hayajanikuta mimi. kama unavyosema mimi ni mtu mzima na siwezi kuwa influenced na tabia za mtu mwingine, labda mimi mwenyewe nitake kufanya hivyo. ninachoangalia hapa tu ni kwa nini watu waseme mtu ana tabia mbaya sababu tu ana rafiki wa tabia zile!
 
Mimi siamini katika hilo. Kuwa marafiki mwafanana tabia. But imeniweka pabaya kwa mpenzi wangu kwa sababu ya marafiki nilionao amekuwa haniamini kabisa.
Imenifanya nianze kupotezea urafiki for the sake of my love for him.
Hivi vitu ni vigumu sana na kuna wengine hata ukieleza vp hakuelewi.
pole sana Remmy, hao ndo wakaka, lol!
ila kuwa mwangalifu na huyo mpenzi, unaweza kujikuta mwisho wa siku umebaki peke yako huna hata wa kumwomba maji ya kunywa, lol!
 
Last edited by a moderator:
kwa mtazamo wangu binafsi, siwezi kuiga tabia ya mtu kisa tupo marafiki..na kwa upande mwingine nikiwa na rafiki ana tabia fulani iliyopitiliza na hamna dalili akapunguza au kuacha basi nitamsaidia ajitahidi kubadilika!! Hii ni kwa rafiki niliyenae karibu ambaye uwepo wake kwangu nami kwake unaonekana na una thamani...
mimi pia nafikiria hivyo. kwanza kujitahidi kumsaidia rafiki aachane na hiyo tabia yake mbaya
 
Inawezekana tatizo lako kubwa ni kujua maana ya rafiki FP. Kujuana na watu, kuongea nao na kuambatana nao hakuwafanyi kuwa marafiki. Marafiki ni mutual feeling, communal understanding. Hao unaosema wewe kuwa wanaweza kuwa na tabia mbaya ukawa nao ni watu tu uliowazoea kwa sababu mazingira na mazoea yamekufanya uwe nao katika muda fulani lakini kamwe si marafiki

Angalia wale watu (marafiki) unaowatafuta kwa mara ya kwanza unapokuwa kwenye matatizo (kwa kiinglish tunasema IN DEEP SHIT). Hao lazima mna tabia zinazofanana kwa kiasi fulani. Na hao ndio hasa marafiki zako.
Mjasiri mimi naongelea marafiki na si watu ninaofahamiana au nakutana nao wakati fulani tu. hao hao marafiki unaoweza kuwakimbilia siyo kweli kama mtafanana 100%. hapo kwenye RED nakubaliana na wewe kabisa, huwezi kuwa na urafiki na mtu ambaye mna tabia tofauti kabisa, hapo sasa sijui mtakuwa mlipatanaje.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom