Comrade Julius Mtatiro

Zitto ndio mwanachadema pekee mwenye akili kuzidi wale wanaotunga sera chama kanisani
Anawezaje kukaa na kufanya kazi na watu wasio na akili? Wewe ndio huna akili, ndio maana hata huko msikitini wamekuchoka ile mbaya na kwakuwa huna uwezo wakutambua mambo unakazana kuleta post zako za kijuha humu. Huijui CCM wala Quran upo tu unatapatapa kaama mbwa koko.
 
Baada ya kusoma post zote nimeamini kitu kimoja WANANDOA WOTE WANATETEANA SANA NA HAKIKA NDOA INOGILE.
 
heeeeeeeeeeeeee, kumbe upo.

unapinga chadema uku unajifanya unampenda zitto. divide and rule imefeli nini?

unafki mbaya sana.

Sijawahi kuipinga chadema,sijawahi kumpenda zito.Ila nimewahi kuichukia chadema na nimewahi kukubaliana na Zito. kama unataka kila anayekubaliana na zito lazima akubaliane na chadema kwa nini usikubaliane na CCM kwa sababu unakubaliana na Nyerere. acha mikumbo bro!! halafu acha kuniogopa kumwita mnafiki ni ishara ya woga, kwani hujajenga hoja yoyote, you need to derive that unafiki. Kinyume na hapo ni inferiority inakutawala na magubu yasiyo ponywa.
 

2015 membe awe mgombea kupitia ccm mshindi atoke c.m teh! teh! ohohh hh hhh oho
 
Na ukatibu amuachie nani?
Kwani CHADEMA mtampa vyeo mdebwedo kama CUF?
 
Hilo kundi la pili ni utopia, hao wanasiasa hawapo si chadema si CCM name it, Pasco kwenye ukweli tuseme na sio upenzi. Ila wako wanaojaribu kuwa sehemu zote mbili.
Waberoya, nakuomba tuwe wakweli kwenye nafsi zetu, tuache ushabiki wa kisiasa, hivi kati ya wanasiasa walioko CCM na wale wa Chadema, nani wako kimaslahi zaidi?. Just be genuine.

Kuna watu wamejiunga CCM na wako CCM sio kwa sababu wanaipenda CCM bali kwa sababu ya opportunities zilizoko CCM. Kuna wana CCM safi ambao wanajua CCM inanuka rushwa na imehodhiwa na wenye pesa, wanaendelea kubaki CCM kwa sababu hawana guts za kukubali kufa njaa. Mimi binafsi sina chama wala sijajipanga kujiunga na chama chochote, nikiamua kuingia siasa ili kupata ulaji, nitajiunga na CCM na kujikomba komba kwa kwenda mbele mpaka niukwae ulaji, siamini kuwa CCM ina uchungu na umasikini wa Tanzania na inatawala kwa malengo ya kuuondoa umasikini huu, CCM inatawala kwa mazoea.

Nikija kwenye Chadema, hivi kuna mwanasiasa anayejiunga Chadema ili kupata ulaji?. Chadema kitakapo pata fursa ya kushika dola (nothing is impossible under the sun), ndipo wanachama wachumia tumbo watakapo kivamia, na wale CCM opportunities ewakishajua there are opportunities no more nao watakihama.

Dhana ya utopia sipingani nayo, ndio maana Mwalimu alisisitiza 'Ujamaa ni Imani', ila utopia huu wa imani kisiasa ni utopia mzuri zaidi, kwani hata usipofanikiwa bado imani itakufariji kuwa the right time is not yet, but one day yes!. Utopia mbaya zaidi ni ule wa kupreech "maisha bora kwa kila Mtanzania", but not practice what you preach!.

Ila pia nakubaliana na wewe, kuwa wako wanasiasa ambao wanataka kuwa kote kote, kupigania maslahi ya taifa na pia, kuchumia tumbo.
 
Kwa mwendo huu tunasafari ndefu kidogo kuja nini maana ya siasa na vyama vingi,
Ni ajabu sana kudhani zaidi ya kuwa CDM ni uganga njaa, unahitaji kufikiri zaidi ya hapo
 

Mkuu unampigia mbuzi gitaa............
 

Nafikiri wewe wamekuchoka huko kanisani..peleka complain yako kwa padre slaa atakusaidia
 
Director na wadau wote, tangu jana nahudhuria vikao muhimu vya kitaifa, na hadi hivi sasa niko katika kikao cha KAMATI YA UTENDAJI. Kwenye saa 6 hivi tutamaliza session ya leo. Nitarudi na majibu ya maswali yako na wadau wengine.

Nitajibu hoja za msingi tu na kutimiza wajibu wangu!

Mtatiro - 30.10.2011
 

Mkuu nashukuru kwa comment yako'nakufikiria sana kwa sababu una uwezo'nakuomba sana do it comrade
 


Natamani sana kama itawezekana Mtatiro huu ujumbe umfikie popote pale alipo..... Mkuu Pasco umesomeka vizuri kabisa!
 

Ha! Ha! Ha! Comrade Waberoya mtu wa shoka!
 

Mkuu wanasiasa sio watu wa kuwaamini kivile....

Leo wanaweza wakaonekana wapiganaji wazuri kwa sababu hajawapata nafasi ya kufanye yale madudu yanayofanywa na wenzao. mpaka sasa upiganaji wa chadema uko kwenye maneno, sera nzuri na wishful thinking at least we can have a hope kwa sababu ya wanachokisema lakini si kwa sababu ndivyo walivyo!

Sita, mwakyembe, kilango et al nao wanaweza wakawa anaonekana kuwa ni wapiganaji wazuri ,laini ukija kwenye logic za ethics hawafai kuwamo ndani ya ccm, lakini ukweli katika maisha yao wanafanya yaleyale wanaoyafanya wenzao

ushaihidi upo, Kibaki aliyeaminiwa na wakenya kumuondoa moi, ndiye aliyekuja kusababisha vita mud mfupi tu.....yuleyule ambye alionekana mkombozi leo hii kaonekana alivyo

Hivi CCM wasingemuangusha Slaa kwenye kura za maoni si Slaa angekuwa CCM, au kwake yy muonekano wa CCM miaka hiyo ulikuwa positive na ghafla imegeuka. au unataka kusema nini akina marando walifahamu lini chadema na wamejiunga lini na kwa nini? akina mpendazoe wametokea wapi? we have very very reason to believe that we have people whose their behaviours are so dynamic and unpredictable..

The only way to overcome this is to establish robust system,systems that they will accomodate any character and punish it accordingly. Ukiwa na system nzuri akina mr.Clean kama akina Mkapa ambao wanatoka wachafu wanashughulikiwa vilivyo na sio kuanza kutumia akili zetu na kujudge eti amefanya mazuri hivyo mwache aende.

I am still believing kuwa viongozi wengi CCM ni wezi na wanaweza ghafla wakawa malaika na wazuri kama system ya kuwafanya hivyo ipo..yaani kuwa accountable kwa matendo yao.

However to touch that achievement we need fight and changes....ambazo kwa uelewa wangu wa siasa za kushiriki na kusikia hatuna vyama vya style ya akina Odinga,Sata na akina morgan Tsvangirai!!!! chadema lacks clear startegy kuichukua nchi na wakitaka uwezo huo wanao, ila sijaona wakifanya hivyo. sijaona wakija na utatuzi mbadala kwa kila tatizo linaloikumba nchi hii. Nimeona nguvu nyingi ikitumika unnecessary na ukija nyuma ya pazia....tetesi au ukweli wowote wa kuihusisha chadema na akina Lowassa NA YA kuwa mwaka 2005 akina JK na Lowasa wangeamia CDM (confirmed) kama wasingepitishwa na kk ya ccm ni skendo nyingine ambayo inakiweka CHADEMA KUWA ANOTHER MISSION TOWN party!


hatuna vyama vya upinzani, chadema ni kivuli cha chama kizuri cha upinzani ambacho kingekuwepo CCM wasingetamba hivi.

Tunataka maandamano ya kudai katiba, tume huru ya uchaguzi, kushiriki uchaguzi ambao unajua mwisho wa siku uamuzi wa nani awe mshindi uko mikononi mwa tume ambayo ya CCM still vyama hivi vinapokea ruzuku kwa ajili ya uchaguzi while we are crying poverty every corner BADO kuna maswali mengi sana.
 

Mkuu nimekupata'mwanasiasa ni binadam mwenye madhaifu yake
 
Mkuu Waberoya uliadimika!!!!! Nilizimiss sana changamoto zako!
 
Waberoya bana.
Kuwa independent thinker ni jambo zuri, lakini linaweza kukuondoa kwenye connecting joints za bigger picture.
Mkuu, ikitokea tukawa na katiba mpya, tume huru ya uchaguzi....unategemea ccm wageuke kuwa malaika kwavile kuna machinery ya accountability in place?...i dont think so. Chadema kinaweza kisiwe chama kilicho kamili sana kwa sasa, but think of it, kipi kina ubora zaidi ya chadema kwa sasa?
Kujenga chama cha siasa sio kazi rahisi, lazima tukubali kwamba Chadema wamejitahidi kufanya yale yanayoonekana machoni pa wengi kama wazaleendo wenye uchungu.
 
tunakusubiri!!
 
Mtatiro kama una masikio utasikia kile mleta uzi amekiandika,kama una macho utakuwa uliona kilichotokea kule Igunga na kile kinalichotokea kwenye bunge lililopita.
Think twice you still have a long way to go and you have a good chance,what is needed is just the wise decision.ila ulipo kwa sasa hapo uliweka kekundu ka pesa sio hako mdogo wangu.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…