Pundamilia07
JF-Expert Member
- Oct 29, 2007
- 1,439
- 54
Mimi ninafikiri kuwa mjadala kama huu ni muhimu sana hasa kwa sisi wachangiaji humu kukwaani. Tukiweza kuelewa na kujieleza (kwa kadri ya uwezo wa mtu binafsi) itasaidia ku-reshape thinking capacity zetu na jinsi ya kujitofautisha na wengine. Kuna mchangiaji ametoa rai kuwa watu warudi wakasome kitabu/vitabu nadhani yuko sahihi, lakini pia akumbuke mada hii inajadilika kwa vile wengi tumesoma habari za Capitalism na Communism kwa miongo kadhaa tangu tukiwa shule za msingi na hata vyuoni, kwahiyo basi ni wakati mwafaka wa kuchangia, kama mtu anaona anahitaji kupata recharge ya kuchangia anaweza kurudi kwenye vitabu na halafu akaendelea kuchangia.
Mtazamo wangu juu ya mada:
Bara la Ulaya kwa muda wa karne kadhaa lilikuwa lilitawaliwa na watawala waliokuwa wanaamini katika sera za kuongeza himaya za utawala wao. Hii hali ilizifanya tawala nyingi kutumia nguvu na vitisho ili kutimiza matakwa yao. Ukandamiza, vita vya wenyewe kwa wenyewe ilikuwa ndiyo mazungumzo ya kila siku. Mienendo hiyo ndiyo iliyowezesha kuzaliwa utawala makeke kabisa wa kijerumani. Historia inatuonyesha kuwa utawala wa wajerumani ulikuwa ni utawala wenye nguvu sana na uliweza kuabudiwa na tawala nyingine kama vile Russia na France achilia mbali nchi nyingine ndogondogo. Ujerumani ilikuwa na sauti kubwa ndani ya ulaya na iliweza kuwa na nguvu kubwa ya maamuzi dhidi ya utawala wa Austro-Hungary, ambalo lilikuwa ni eneo muhimu katika mipangilio ya kutwaa himaya zingine za ulaya.
Ujerumani iliweza kutwaa na kushikilia baadhi ya maeneo ya Russia baada ya vita kati ya nchi hizo mbili. Hali kadhalika, Ujerumani iliivamia Ufaransa na kuishinda vitani na kuchukua maeneo ya Ufaransa. Kuendelea kukua kwa Ujerumani kieneo kulileta wasiwasi mkubwa miongoni mwa mataifa mengi ikiwemo hata Uingereza. Nchi kadhaa ziliwekeana mikataba ya kusaidiana kivita endapo Ujerumani itaishambulia moja kati ya nchi zao, mojawapo ya mikataba hiyo ilikuwa ni mkataba kati ya Uingereza na Ufaransa. Ufaransa kijiografia ikiwa imebanwa na Ujerumani ilikuwa haina uwezo wa kujiongezea himaya ndani ya Ulaya na badala yake ndiyo iliyotoa ushawishi mkubwa kwa nchi za ulaya kujigawia maeneo mbalimbali dunia na kuyageuza kuwa makoloni yao.
Kwa upande mwingine, kama ilivyokuwa Ujerumani, Japan nayo ilikuwa ni tishio jingine kwa upande wa bara la Asia. Wajapani waliweza kutwaa maeneo mengi kama vile China, Korea na maeneo mengine ya Asia pamoja na baadhi ya maeneo ya Russia. Utawala wa Kijapani ulikuwa ni utawala wakikatili na uliogopewa sana. Wajapani walikuwa na silaha na jeshi kubwa ambalo liliweza kupigana vita zaidi ya moja kwa wakati mmoja.
Nini Kilitokea baada ya ubabe wa Wajerumani na Wajapani?
Kuendelea kukua kwa makeke (aggressiveness) ya wajerumani, kulihatarisha sana usalama wa Ufaransa. Ufaransa iliona kuwa bila ujerumani kupunguzwa nguvu basi taifa la ufaransa halitaweza kuwepo siku za usoni. Baadhi ya wachunguzi wa mambo wanadai kuwa mauaji ya mtawala wa Astro-Hungary (mshirika mkuu wa ujerumani) yalipangwa kama njia ya kuitingisha ujerumani. Matokeo yake ilikuwa ni Ujerumani kutangaza vita dhidi ya Poland, Russia na Ufaransa na hatimaye kuwa vita kuu ya kwanza ya dunia. Baada ya ujerumani kushindwa vita ile ya kwanza, mataifa kama Ufaransa na Russia yalitumia mwanya huo kujiimarisha kijeshi dhidi ya udhalimu mwingine wowote wa Ujerumani hapo baadae.
Wajapani ambao walikuwa na nguvu sana walisalimu amri baada ya kushambuliwa kwa mabomu ya atomic miji yake ya Hiroshima na Nagasaki. Maamuzi ya kuishambulia Japan kwa mabomu ya atomic yalitokana na kushambuliwa kwa Marekani pale Pearl Harbor.
Kwanini ukoministi ulianza kukua?
Kimsingi baada ya vita kuu ya kwanza ambayo Wamarekani waliisadia ulaya dhidi ya wajerumani, Wamarekani waliitaka Ulaya ibadilike kutoka katika mifumo ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, ukandamizaji, expansionist na badala yake ijikite katika utawala wa kikapitalist, kidemorasia zaidi na uhuru wa kibiashara (free economy). Pia Wamarekani walipendekeza kuundwa kwa mataifa huru kwa maana ya nchi za ulaya ziachilie makoloni yao yajitawale yenyewe. Ushawishi wa Marekani uliweza kuyafanya mataifa mengi ya ulaya hasa magharibi kuchukua sera za kikapitalist na hivyo kujenga upande uliokuwa na nguvu nyingi sana za kiuchumi na kijeshi. Russia ilitumia mwanya huu wa kushindwa kwa ujerumani kujiimarisha kijeshi huku ikisaidiwa na Marekani. Russia kwa vile ilikuwa nyuma kimaendeleo ukilinganisha na nchi nyingine kama vile Uingereza, Ujerumani na Ufaransa, iliamua kufanya mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kijamii ikiwemo kushikilia uchumi mikononi mwa serikali. Malengo makubwa ya kufanya hivyo ilikuwa ni kuwalazimisha wananchi wa Russia wautumikie utawala wao 100%. Uzalishaji wowote ule wa mtu binafsi au kikundi ulimilikiwa na serikali. Serikali iliweza kujilimbikizia na kumiliki mali zilizozalishwa na wananchi bila ya hiyari zao. Baada ya Russia kuimarika na kufuatia mapinduzi makubwa ya akina Lennin na Stalin, Russia iliamua kurudi katika sera za expansionist ambazo zilikuwa zinapigwa vita barani ulaya. Ilikuendelea kushikilia sera hizo Russia ilibidi kutafuta washirika na kuungwa mkono, mshirika wake wa kwanza akiwa ni China ambaye alinyanyaswa sana na Japan kama alivyokuwa Russia dhidi ya Ujerumani. Malengo ya Russia na China ya kukuza ukominist ilikuwa ni njia ya kuwasaidia kujijenga na kuepuka kushambuliwa na kufanywa wanyonge na mataifa makubwa.
Kama vile ambavyo Marekani ilivyokuwa inasambaza ukapitalist kwa nia ya free economy, Warusi walieneza ukomunist ili wajilinde.
Kwahiyo mimi ninaona sera za kikomunist ni sera ambazo zilikuwepo kwa wakati ule kwa malengo maalum na ndiyo maana leo hii Warusi na Wachina wanaachana nazo kwa vile sababu zilizokuwepo wakati ule hazipo tena. Lakini sera za ukapitalist ndiyo zinaonekana kuwa ndiyo sera sahihi zinazoweza kuleta mabadiliko ya kweli kutoka kwa mtu mmoja mmoja.
Nikirudi hapa Tanzania, Tanzania ilijikuta inapata uhuru wakati mivutano hii miwili ikiwa katika nguvu kubwa. Na ukifuatilia historia ya kupata uhuru kwa nchi nyingi hasa Afrika ni kwamba watawala walikuwa wanatafuta warithi ambao watakuja kuwa viongozi wa nchi zinazopewa uhuru. Kwa mfano makoloni ya mfaransa, wengi waliokuja kuwa viongozi wa nchi hizo walikuwa na mahusiano ya karibu au moja kwa moja na watawala wa kifaransa. Kwa hiyo basi wale ring leaders wa ukomunist waliweza kupandikiza na wenyewe propaganda kwa mataifa haya machanga ikiwemo Tanzania ili waweze kutengeneza block kwa malengo na faida ya Russia na China. Ninakumbuka wakati Tanzania inasherehekea miaka 10 ya Uhuru wa Tanganyika, serikali ya China ilijihusisha kwa gharama kubwa katika kusaidia sherehe zile. China ilikuwa ni recruiter wetu wa kuhakikisha tunaungana nao.
Kimsingi mwisho vita baridi kati ya Marekani na Urusi ndiyo iliyohitimisha ukomunist.
Kwa mtazamo wangu, Tanzania sasa hivi inapaswa kutamka kuwa sera za ujamaa zimeachwa na badala yake tutaendelea na hii ya kujitegemea (Ukapitalist).
Mtazamo wangu juu ya mada:
Bara la Ulaya kwa muda wa karne kadhaa lilikuwa lilitawaliwa na watawala waliokuwa wanaamini katika sera za kuongeza himaya za utawala wao. Hii hali ilizifanya tawala nyingi kutumia nguvu na vitisho ili kutimiza matakwa yao. Ukandamiza, vita vya wenyewe kwa wenyewe ilikuwa ndiyo mazungumzo ya kila siku. Mienendo hiyo ndiyo iliyowezesha kuzaliwa utawala makeke kabisa wa kijerumani. Historia inatuonyesha kuwa utawala wa wajerumani ulikuwa ni utawala wenye nguvu sana na uliweza kuabudiwa na tawala nyingine kama vile Russia na France achilia mbali nchi nyingine ndogondogo. Ujerumani ilikuwa na sauti kubwa ndani ya ulaya na iliweza kuwa na nguvu kubwa ya maamuzi dhidi ya utawala wa Austro-Hungary, ambalo lilikuwa ni eneo muhimu katika mipangilio ya kutwaa himaya zingine za ulaya.
Ujerumani iliweza kutwaa na kushikilia baadhi ya maeneo ya Russia baada ya vita kati ya nchi hizo mbili. Hali kadhalika, Ujerumani iliivamia Ufaransa na kuishinda vitani na kuchukua maeneo ya Ufaransa. Kuendelea kukua kwa Ujerumani kieneo kulileta wasiwasi mkubwa miongoni mwa mataifa mengi ikiwemo hata Uingereza. Nchi kadhaa ziliwekeana mikataba ya kusaidiana kivita endapo Ujerumani itaishambulia moja kati ya nchi zao, mojawapo ya mikataba hiyo ilikuwa ni mkataba kati ya Uingereza na Ufaransa. Ufaransa kijiografia ikiwa imebanwa na Ujerumani ilikuwa haina uwezo wa kujiongezea himaya ndani ya Ulaya na badala yake ndiyo iliyotoa ushawishi mkubwa kwa nchi za ulaya kujigawia maeneo mbalimbali dunia na kuyageuza kuwa makoloni yao.
Kwa upande mwingine, kama ilivyokuwa Ujerumani, Japan nayo ilikuwa ni tishio jingine kwa upande wa bara la Asia. Wajapani waliweza kutwaa maeneo mengi kama vile China, Korea na maeneo mengine ya Asia pamoja na baadhi ya maeneo ya Russia. Utawala wa Kijapani ulikuwa ni utawala wakikatili na uliogopewa sana. Wajapani walikuwa na silaha na jeshi kubwa ambalo liliweza kupigana vita zaidi ya moja kwa wakati mmoja.
Nini Kilitokea baada ya ubabe wa Wajerumani na Wajapani?
Kuendelea kukua kwa makeke (aggressiveness) ya wajerumani, kulihatarisha sana usalama wa Ufaransa. Ufaransa iliona kuwa bila ujerumani kupunguzwa nguvu basi taifa la ufaransa halitaweza kuwepo siku za usoni. Baadhi ya wachunguzi wa mambo wanadai kuwa mauaji ya mtawala wa Astro-Hungary (mshirika mkuu wa ujerumani) yalipangwa kama njia ya kuitingisha ujerumani. Matokeo yake ilikuwa ni Ujerumani kutangaza vita dhidi ya Poland, Russia na Ufaransa na hatimaye kuwa vita kuu ya kwanza ya dunia. Baada ya ujerumani kushindwa vita ile ya kwanza, mataifa kama Ufaransa na Russia yalitumia mwanya huo kujiimarisha kijeshi dhidi ya udhalimu mwingine wowote wa Ujerumani hapo baadae.
Wajapani ambao walikuwa na nguvu sana walisalimu amri baada ya kushambuliwa kwa mabomu ya atomic miji yake ya Hiroshima na Nagasaki. Maamuzi ya kuishambulia Japan kwa mabomu ya atomic yalitokana na kushambuliwa kwa Marekani pale Pearl Harbor.
Kwanini ukoministi ulianza kukua?
Kimsingi baada ya vita kuu ya kwanza ambayo Wamarekani waliisadia ulaya dhidi ya wajerumani, Wamarekani waliitaka Ulaya ibadilike kutoka katika mifumo ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, ukandamizaji, expansionist na badala yake ijikite katika utawala wa kikapitalist, kidemorasia zaidi na uhuru wa kibiashara (free economy). Pia Wamarekani walipendekeza kuundwa kwa mataifa huru kwa maana ya nchi za ulaya ziachilie makoloni yao yajitawale yenyewe. Ushawishi wa Marekani uliweza kuyafanya mataifa mengi ya ulaya hasa magharibi kuchukua sera za kikapitalist na hivyo kujenga upande uliokuwa na nguvu nyingi sana za kiuchumi na kijeshi. Russia ilitumia mwanya huu wa kushindwa kwa ujerumani kujiimarisha kijeshi huku ikisaidiwa na Marekani. Russia kwa vile ilikuwa nyuma kimaendeleo ukilinganisha na nchi nyingine kama vile Uingereza, Ujerumani na Ufaransa, iliamua kufanya mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kijamii ikiwemo kushikilia uchumi mikononi mwa serikali. Malengo makubwa ya kufanya hivyo ilikuwa ni kuwalazimisha wananchi wa Russia wautumikie utawala wao 100%. Uzalishaji wowote ule wa mtu binafsi au kikundi ulimilikiwa na serikali. Serikali iliweza kujilimbikizia na kumiliki mali zilizozalishwa na wananchi bila ya hiyari zao. Baada ya Russia kuimarika na kufuatia mapinduzi makubwa ya akina Lennin na Stalin, Russia iliamua kurudi katika sera za expansionist ambazo zilikuwa zinapigwa vita barani ulaya. Ilikuendelea kushikilia sera hizo Russia ilibidi kutafuta washirika na kuungwa mkono, mshirika wake wa kwanza akiwa ni China ambaye alinyanyaswa sana na Japan kama alivyokuwa Russia dhidi ya Ujerumani. Malengo ya Russia na China ya kukuza ukominist ilikuwa ni njia ya kuwasaidia kujijenga na kuepuka kushambuliwa na kufanywa wanyonge na mataifa makubwa.
Kama vile ambavyo Marekani ilivyokuwa inasambaza ukapitalist kwa nia ya free economy, Warusi walieneza ukomunist ili wajilinde.
Kwahiyo mimi ninaona sera za kikomunist ni sera ambazo zilikuwepo kwa wakati ule kwa malengo maalum na ndiyo maana leo hii Warusi na Wachina wanaachana nazo kwa vile sababu zilizokuwepo wakati ule hazipo tena. Lakini sera za ukapitalist ndiyo zinaonekana kuwa ndiyo sera sahihi zinazoweza kuleta mabadiliko ya kweli kutoka kwa mtu mmoja mmoja.
Nikirudi hapa Tanzania, Tanzania ilijikuta inapata uhuru wakati mivutano hii miwili ikiwa katika nguvu kubwa. Na ukifuatilia historia ya kupata uhuru kwa nchi nyingi hasa Afrika ni kwamba watawala walikuwa wanatafuta warithi ambao watakuja kuwa viongozi wa nchi zinazopewa uhuru. Kwa mfano makoloni ya mfaransa, wengi waliokuja kuwa viongozi wa nchi hizo walikuwa na mahusiano ya karibu au moja kwa moja na watawala wa kifaransa. Kwa hiyo basi wale ring leaders wa ukomunist waliweza kupandikiza na wenyewe propaganda kwa mataifa haya machanga ikiwemo Tanzania ili waweze kutengeneza block kwa malengo na faida ya Russia na China. Ninakumbuka wakati Tanzania inasherehekea miaka 10 ya Uhuru wa Tanganyika, serikali ya China ilijihusisha kwa gharama kubwa katika kusaidia sherehe zile. China ilikuwa ni recruiter wetu wa kuhakikisha tunaungana nao.
Kimsingi mwisho vita baridi kati ya Marekani na Urusi ndiyo iliyohitimisha ukomunist.
Kwa mtazamo wangu, Tanzania sasa hivi inapaswa kutamka kuwa sera za ujamaa zimeachwa na badala yake tutaendelea na hii ya kujitegemea (Ukapitalist).