Nataka niseme hivi, Kama kuna kosa mnalofanya wanandoa wa siku hizi ni ku cheat. Hakuna rangi hutaiona ukianza tu ku cheat.
Mwanamke lazima uelewe kuwa wewe ni "Shamba" ukipanda mbegu itaota kwani lina rutuba. Sasa, unaporuhusu mtu kuja kuotesha mbegu hapo, wewe unadhani una akili nzuri kweli? Mengi yanakuingia weye mama, zile mb.egu za yule mtu ni uhai wake ulee. Muumba ndiye aliumba hivyo. Sasa unapoamua kuupokea uhai wa huyu na yule na yule weye una akili kweli? Hapa nawahoji wale wa mama wanaoshabikia ujinga huu. Kama una akili, hutakubali kubadili damu za watu kila mara.
Magonjwa je? Haya, dharau je? Mwanaume anatamani aku do tu, ajisikie kuwa huyu ni wa 20 baasi. Hana lolote zaidi. Haswa akiwa na mke tayari hana chochote awezacho kukifanya zaidi. Weye ukiwa mke wa mtu, bahati mbaya mumeo awe mtu mtaratibu asiyetaka ugomvi, hicho kidume kitataka kumfedhehesha popote anapomwona. Huyu atakuletea kifo mara moja.
Wababa, wakikuta labda huyo mwanamke ni ghali kidogo, wanajitutumua mpaka wanafilisi nyumbani. Kilio cha ile familia kitakukuta tu. Mwosha huoshwa!!
Hakuna cheating njema hata kidogo. Yule uliyempenda ukamtwaa awe wako, nasema kamwe HAZEEKI. Nimepima na nimeona. Miaka sasa ni 40 na huyu wangu na kila siku namwona mpya. Kama ni ushamba acha uwe nami naukubali. Mind yu, before her, I can not count them lakin hapa nimefika.