Comedian wa Bongo

Comedian wa Bongo

Je, ni komedian (mchekeshaji) gani hapa Bongo anayeweza kulinganishwa na Eric Omondi wa kenya? Kwa mnaomfahamu naomba mnijuze nicheki ukali wake.

KUmbe yule jamaa ni mkenya? By the way siwezi kum judge coz nimeona kazi yake moja tu aliyo copy kwa diamon, so I rate him 2/10
 
Bambo, the guy anajua bwana na kingwendu
Bambo kabarikiwa sana.Ana kipaji cha aina mbili za vichekesho.Aina hizo ni:
1. mimicry comedy
2.visual comedy
Vipaji hivi alivionesha aliposhiriki michezo ya kuigiza kwenye kundi la akina bishanga
wakati ule maigizo hayo yakioneshwa na kituo cha itv
Halafu visual comedy yake ni ya kipekee sana siyo kama ya mr bean au charlie
chaplin.Hiyo visual comedy yake kama utakumbuka, aliionesha wakati fulani
alipomwelezea mtu aliyekunywa dawa chungu anavyofanya.Wakumbuka? Hiyo
ndio uniqueness ya visual comedy ya Bambo.Ina maana anaweza kuchekesha
sana watu kwa kuwaelezea jinsi abiria waliokosa usafiri wanavyofanya etc.
Kingwendu naye kipaji chake cha uchekeshaji kipo kwenye kujibadili sura
(facial contortions)na mimicry.Kuna hii clip ya kingwendu ila bahati mbaya haionekani
vizuri kwa sababu ya poor lighting! KINGWENDU
 
KUmbe yule jamaa ni mkenya? By the way siwezi kum judge coz nimeona kazi yake moja tu aliyo copy kwa diamon, so I rate him 2/10
Hebu nieleze vizuri warumi. Eti uliona kazi ya eric omondi aliyokopi toka kwa diamon?
Ni diamon gani huyo? diamon ni msanii kwenye fani ya uchekeshaji?
 
Last edited by a moderator:
Kwa ujumla hapa Bongo hakuna solo stand-up comedian aliye kwenye class ya anna kansiime, eric omondi au gwiji jimmy carr. Comedian wetu hapa bongo wanafanya kwenye kundi tu - ze komedi, futuhi,pikabom nk.
We nawe umeuliza halafu umeandaa majibu bila kutafakari mzee MAJUTO yupo kundi gani ????????????
 
We nawe umeuliza halafu umeandaa majibu bila kutafakari mzee MAJUTO yupo kundi gani ????????????
Haloo samsu, mzee majuto katika uchekeshaji anatumia staili ya stori za kuchekesha na kukuhamasisha ucheke kwa kutumia uso wake! Mara nyingi hafanyi mwenyewe, anafanyia kwenye kundi.Labda kama kakodishwa na kampuni/shirika
kufanya tangazo kama pspf walivyomtumia kwenye tangazo hivi majuzi.
 
Last edited by a moderator:
Kingwendu ana kipaji kikubwa cha kutumia uso kufanya ucheshi kama HAPA
 
Mpoki unamuonaje
Mpoki nilishamzungumzia kwenye post za mwanzomwanzo ukurasa labda wa pili au tatu hivi.
Nilimwelezea mpoki kama ifuatavyo.
Mpoki ana kipaji tofauti sana kuliko wachekeshaji wengi hapa bongo na hata
duniani kwa ujumla.Kipaji chake kikubwa ni uwezo wake wa kuunda misemo
yenye ukweli na ucheshi ndani yake.Waukumbuka msemo huu?:"Hata mzungu
awe mweupe kiasi gani, kivuli chake kitabaki cheusi tu!"Kuna ucheshi uliomo
kwenye huu msemo na misemo yake mingine mingi.Kipaji hiki cha witty statements
akichanganya na kile cha parting shots alichokionesha akiwa mc kwenye kili music
awards ni vipaji tosha vya kupalilia na kumfanya mchekeshaji mkubwa mwenye
mafanikio tanzania na kokote kiswahili kinakotumika.
 
Changamoto iliyopo upande wa tasnia ya filamu ndio iliyopo kwenye standup comedy, pamoja na kipaji binafsi cha mchekeshaji bado anahitaji kuwa na uwezo wa KUFUNDISHIKA.

Wapo wengi wanaoweza kuchekesha kwenye vikundi vya watu mashuleni, sehemu za kazi n.k...lakini inapokuja haja ya kutaka kufanya hivyo "kikazi zaidi" unahitaji zaidi ya kipaji tu...na kama unatamani jukwaa la kimataifa zaidi basi lazima na kichwani uwe vyema, kwa kupata elimu ya darasani au la basi uwezo mkubwa wa kuelewa mambo.

Wasanii wakubwa wa kimataifa wa kuchekesha jukwaani huwa na mtu au timu nyuma yao, sidhani kama wengi wetu tunajua kuwa wanayoongea pale huandikwa kabla (hata kama sehemu kubwa au yote ni mawazo ya mchekeshaji mwenyewe), kisha hufanyika reharsal chini ya wa/mtaalamu/director/sound/lights/camera operators n.k....mchekeshaji huandaliwa jinsi ya kupangilia hoja ya mwanzo, kati na ya mwisho, jinsi ya kutumia jukwaa, kupatiwa taarifa sahihi kwa kila analotaka kuongelea pale jukwaani, na sio kwa kuwa ni mchekeshaji basi unaongea tu chochote bila kujali usahihi wake.

Hivyo utaona kipaji pekee hakitoshi, bali mtu anahitaji skills za kuelewa miongozo na kukumbuka mistari (lines) hata kama yeye ndio ameandika script, Hakuna jambo linalofanywa hovyohovyo tu haswa katika level ya kimataifa.

Hivyo tujiulize kati ya wasanii wetu wote tunaowataja wangapi tunaona wapo kwenye nafasi hiyo ? Nimeshaangalia kazi kadhaa za Eric, kwa kweli anajitahidi sana kulinganisha na wasanii wetu.
 
Changamoto iliyopo upande wa tasnia ya filamu ndio iliyopo kwenye standup comedy, pamoja na kipaji binafsi cha mchekeshaji bado anahitaji kuwa na uwezo wa KUFUNDISHIKA.

Wapo wengi wanaoweza kuchekesha kwenye vikundi vya watu mashuleni, sehemu za kazi n.k...lakini inapokuja haja ya kutaka kufanya hivyo "kikazi zaidi" unahitaji zaidi ya kipaji tu...na kama unatamani jukwaa la kimataifa zaidi basi lazima na kichwani uwe vyema, kwa kupata elimu ya darasani au la basi uwezo mkubwa wa kuelewa mambo.

Wasanii wakubwa wa kimataifa wa kuchekesha jukwaani huwa na mtu au timu nyuma yao, sidhani kama wengi wetu tunajua kuwa wanayoongea pale huandikwa kabla (hata kama sehemu kubwa au yote ni mawazo ya mchekeshaji mwenyewe), kisha hufanyika reharsal chini ya wa/mtaalamu/director/sound/lights/camera operators n.k....mchekeshaji huandaliwa jinsi ya kupangilia hoja ya mwanzo, kati na ya mwisho, jinsi ya kutumia jukwaa, kupatiwa taarifa sahihi kwa kila analotaka kuongelea pale jukwaani, na sio kwa kuwa ni mchekeshaji basi unaongea tu chochote bila kujali usahihi wake.

Hivyo utaona kipaji pekee hakitoshi, bali mtu anahitaji skills za kuelewa miongozo na kukumbuka mistari (lines) hata kama yeye ndio ameandika script, Hakuna jambo linalofanywa hovyohovyo tu haswa katika level ya kimataifa.

Hivyo tujiulize kati ya wasanii wetu wote tunaowataja wangapi tunaona wapo kwenye nafasi hiyo ? Nimeshaangalia kazi kadhaa za Eric, kwa kweli anajitahidi sana kulinganisha na wasanii wetu.
Asante FYATU kwa uelewa wako mkubwa kuhusu fani ya uchekeshaji. Comedy za maana zinahitaji a concerted team work of experts -script writers, costume and trade mark designers, etc. Lakini kijana wa kitanzania aneyejua kukunja uso ukafanana na uso wa fisi halafu watu wakamshangaa na kucheka anasema na kutamba yeye ni mchekeshaji (comedian) na hataki kusikia chochote eti kuhusu kupanua ujuzi nk. Sijui kwa nini vijana wengi wa kitanzania ni so complacent (betweka).Wakiingia kwenye kikundi wakapata laki mbili tatu za kununua smartphone wanaona wameshafika na wanashindwa kabisa kufanya maonesho ya solo stand-up comedy kama afanyayo eric omondi.

Asante sana mdau kwa input yako murua sana!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom