Comedian wa Bongo

Comedian wa Bongo

Hivi Mr Bean kasimama upande gani ?
Mr Bean, TODAYS, yuko class moja na msanii wa zamani aliyeitwa Charlie Chaplin.
Ucheshi wao ni tofauti na una jina maalum la 'visual comedy' Wasanii wa futuhi
wanachanganya hii visual comedy na sound comedy na matokeo yake ni kitu ambacho hakipo
duniani.
 
Last edited by a moderator:
Hao kina kinyambe na brother k hawafanani na omondi style ya kuchekesha,Eric omondi style yake ni ile ya kina mc pili pili.angalia hata youtube-churchil show Eric omondi ni noma na mbunifu
Ni kweli best yangu Viol. Staili ya brother k ni visual comedy kuchanganya na mimicking comedy.Mchanganyiko huu waweza zalisha uchafu wa ajabu usiopatikana popote duniani. Yeye Omondi staili yake ni ya kawaida ijulikanayo duniani: staili ya jokes punchlines.Jokes punchlines ndo staili itumikayo na comedians wengi duniani.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli best yangu Viol. Staili ya brother k ni visual comedy kuchanganya na mimicking comedy.Mchanganyiko huu waweza zalisha uchafu wa ajabu usiopatikana popote duniani. Yeye Omondi staili yake ni ya kawaida ijulikanayo duniani: staili ya jokes punchlines.Jokes punchlines ndo staili itumikayo na comedians wengi duniani.

Tafuta YouTube MC.Pilipili,yule kwa style yake anaweza akafanya comedy popote,mtu Kama Eric omondi anaweza Fanya show popote akakubalika Kama kina baskethmouth,hawa kina kinyambe style yao hii ya kukunja midomo wataenda kufanya wapi?


Mi huwa wananiboa ubunifu hamna hata hiyo mimicry yenyewe haichekeshi,kwa mbali ningesema Labda kitale,bongo hamna comedy
 
Last edited by a moderator:
Kinyambe ni shida pia tembea yke n ongea yke kma taahira flani yuko poa

hahahahahaaaa basi sawa kweli watu tupo tofauti, mimi nikiingia channel 10 nikikutana nae nitakavyo bonyeza hiyo remote kwa nguvu kutaka kubadilisha chanel batani zaweza dumbukia kwenye vishimo vyake.
 
hahahahahaaaa basi sawa kweli watu tupo tofauti, mimi nikiingia channel 10 nikikutana nae nitakavyo bonyeza hiyo remote kwa nguvu kutaka kubadilisha chanel batani zaweza dumbukia kwenye vishimo vyake.

Yuko poa kifani mpe support kinyambe anaweza sana
 
Yuko poa kifani mpe support kinyambe anaweza sana

hana ubunifu, toka nimuone mwanzo mwisho yeye katahahirika tu, kama hiyo ndio kazi yake ajipange aisee, kiukweli mimi ananiboa, hana tofauti na masanja style yake ya kupindisha miguu na kuongea kama mbondei sijui, ategemee watu watakuwa wanacheka kila siku kwa tembea yake ile??
 
Inaonekana hata kwenye vyuo vya sanaa napo wanafanya comedy
maana inaonekana hawana uelewa wa tofauti ya hizo vichekesho so tuanzishe chuo kama uko na uelewa kamanda.
 
Tafuta YouTube MC.Pilipili,yule kwa style yake anaweza akafanya comedy popote,mtu Kama Eric omondi anaweza Fanya show popote akakubalika Kama kina baskethmouth,hawa kina kinyambe style yao hii ya kukunja midomo wataenda kufanya wapi?


Mi huwa wananiboa ubunifu hamna hata hiyo mimicry yenyewe haichekeshi,kwa mbali ningesema Labda kitale,bongo hamna comedy
Nimemcheki mc pilipili mshikaji Viol. Anatumia jukwaa la maharusi kukuza na kuendeleza kipaji chake cha uchekeshaji na staili yake ni jokes punchline kama Omondi.Namkubali, yuko vizuri.Mwone HAPA kwenye harusi
 
Last edited by a moderator:
Inaonekana hata kwenye vyuo vya sanaa napo wanafanya comedy
maana inaonekana hawana uelewa wa tofauti ya hizo vichekesho so tuanzishe chuo kama uko na uelewa kamanda.
TODAYS, uchekeshaji upo ndani ya mtu; it is an inborn ability. Kumfundisha mtu uchekeshaji ni ngumu, haiwezekani.
Wachekeshaji maarufu duniani walizaliwa na vipaji hivyo, na hata waliposomea fani nyingine walijikuta wanaacha hizo fani walizosomea na kuingia kwenye uchekeshaji.Watu wa aina hiyo ni:Rowan Atkinson (Mr Bean), Jimmy Carr, Anne Kansiime etc
 
Last edited by a moderator:
uuuuwiii kumbe anaitwa kinyambe??? hata jina simjui,dont tell me kuwa eti anakuchekeshaga na yale makengeza yake???
Kinyambe anavutia wachache kwa sababu anachanganya vibaya comedy za aina mbili; visual na mimicry.Kama hujui kuzioanisha vizuri, msukumo wa ucheshi hupungua sana.Tusiandikie mate na wino upo! Mtazame Kinyambe HAPA na mchanganyiko wake usioendana; sauti ya kuiga na miondoko ya kinamna!
 
Kinyambe anavutia wachache kwa sababu anachanganya vibaya comedy za aina mbili; visual na mimicry.Kama hujui kuzioanisha vizuri, msukumo wa ucheshi hupungua sana.Tusiandikie mate na wino upo! Mtazame Kinyambe HAPA na mchanganyiko wake usioendana; sauti ya kuiga na miondoko ya kinamna!

Tuko tofauti mi namuonaje sijui kinyambe,mc pilipili omondi na kansime ndo the best kwangu
 
Halafu mzurimie, cheki ujinga wa braza k wanayemsifia HAPA.Ukiwa na wanao au mtu unayemheshimu itabidi uzime tv au utafute kisingizio cha kuondoka haraka usiendelee kusikiliza!

Ok nashukuru.
 
Last edited by a moderator:
Kama ni stand up comedy kwa bongo hakuna anayemzidi Eric Omond.
Ingawa kijana wangu mc pilipili ni mkali ila bado underground akikaza atafikia level za kina Eric na Anne.

Kwa comedy za kawaida hapa bongo no. 1 ni Joti halo halina ubishi.
Joti anafanya kwenye group mheshimiwa, siyo solo stand-up. Kwa mc pilipili umepatia, nimemcheki leo ana kipaji anachokikuza kwenye sherehe za harusi.
 
Tumemsahau dada wa kiganda, Anne Kansiime.Staili ya huyu dada ni tofauti sana.Si visual wala jokes punchline ila ni kuchimba social issues zinazokera. Hebu mwangalie HAPA akiwachimba watu wanaopiga simu kisha kukuambia ni wrong number. Pia jinsi akina mama/dada wanavyopenda ugomvi.
 
Back
Top Bottom