Comedian wa Bongo

Comedian wa Bongo

Naombeni link kama wanarusha youtube...na mie nicheke sitaki uso uzeeke mie.
 
Kama ni stand up comedy kwa bongo hakuna anayemzidi Eric Omond.
Ingawa kijana wangu mc pilipili ni mkali ila bado underground akikaza atafikia level za kina Eric na Anne.

Kwa comedy za kawaida hapa bongo no. 1 ni Joti halo halina ubishi.
 
wabongo wengi wanadhania kufanya fanya kama mazombi ndio wanachekeshaaa.
 
Thanks nitafurahi, Eric nimemfahamia insta anajua kujipa promo vizuri
Halafu mzurimie, cheki ujinga wa braza k wanayemsifia HAPA.Ukiwa na wanao au mtu unayemheshimu itabidi uzime tv au utafute kisingizio cha kuondoka haraka usiendelee kusikiliza!
 
Last edited by a moderator:
Eti bwana! Kama hayo mafutuhi wa startv! Ujinga mtupu.

kuna yule mwingine kule channel 10 yule anayefanyafanya kama tahahira flani, nitashangaa sana mtu akiniambia huwa anachekeshwa naye.
 
Mpoki (alifanya stand up comedy kwenye tuzo za kili)
Ile ya Mpoki kwenye kili awards strictly siyo stand-up comedy ila ile ilikuwa ni hilarious MC. Kwenye kili awards Mpoki alikuwa MC, hakuwa comedian.
 
mzurimie, ukimaliza huko nilikokuwekea links mbalimbali karibu umwone
comedian wa kimataifa, Jimmy Carr akionesha UKALI WAKE HAPA
 
Last edited by a moderator:
Ile ya Mpoki kwenye kili awards strictly siyo stand-up comedy ila ile ilikuwa ni hilarious MC. Kwenye kili awards Mpoki alikuwa MC, hakuwa comedian.

Mwe! Asante kwa kunitoa ushamba...but i think he is good too if he can give a try to it
 
kuna yule mwingine kule channel 10 yule anayefanyafanya kama tahahira flani, nitashangaa sana mtu akiniambia huwa anachekeshwa naye.
Bahati mbaya sana Paula kilaki channel 10 siipatagi ninakoishi.Ni kweli kuna watu sense ya humour kwao ni vitu vya ajabu, kama baadhi ya watu wanaosema eti braza k wa futuhi ni kiboko kwa uchekeshaji. Kama braza k anakuchekesha, basi hata mtu anayecheua kwa sauti kubwa atakuchekesha!
 
Last edited by a moderator:
Hivi Mr Bean kasimama upande gani ?
 
Mwe! Asante kwa kunitoa ushamba...but i think he is good too if he can give a try to it
Sana, tena sana proto cute. Naona kipaji kikubwa sana cha uchekeshaji ndani ya ubongo wa Mpoki.Akipata training na maelekezo ya do's na dont's kwenye uchekeshaji Mpoki ana potential ya kuwa mchekeshaji mkubwa hapa tanzania.Akichanganya ni ile misemo yake iliyojaa ukweli wa ucheshi eg 'hata mzungu awe mweupe kiasi gani kivuli chake kitakuwa cheusi tu' Mpoki atakuwa tishio tanzania.Hakuna wa kumsaidia hivyo dhahabu inakanyagwa na ng'ombe tu!
 
Last edited by a moderator:
Hao kina kinyambe na brother k hawafanani na omondi style ya kuchekesha,Eric omondi style yake ni ile ya kina mc pili pili.angalia hata youtube-churchil show Eric omondi ni noma na mbunifu
 
Back
Top Bottom