Duh! Kumbe kweli Manji ana haki ya kulalamika kwamba nchi yake haimthamini manake ingawaje bandiko la
Kibanga Ampiga Mkoloni halimtaji Manji kama mnufaika lakini bado raia tunamkomalia Manji!!! Kibanga anauliza:
Mbona sioni manji wala Quality Company humu? naona mabank tu na Kinondoni manispaa, Je manji anaingia vipi humu?
Sakarasi mzima ya huu mradi ni kwamba Manispaa ya Kinondoni iliingia mkataba na Manji kwa ajili ya kuuendeleza juu ufukwe in 2007. Hata hivyo, baadae Manispaa wakamnyang'anya kwa maelezo kwamba Manji alishindwa kutekeleza masharti ya mkataba husika na badala yake Manispaa wakaihamishia hiyo project kwa wadau wengine kama wanavyosomeka hapo juu.
Manji baada ya kunywang'wanywa huo mradi, akaenda mahakama kuu kitengo cha ardhi na at the end of story, Mahakama ikatoa hukumu in favor of Manji... kwamba, Yusuph Manji ana haki zote na hiyo project ingawaje manispaa hawajaridhika na maamuzi ya mahakama ambayo hata hivyo; ama bado hawajayakatia rufaa na kama wameshakatia bado hayajatolewa maamuzi.
Hivi majuzi Mkuu wa Mkoa wa Dar es saalam Mecky Sadick alinukuliwa akimuomba Manji aachie ufukwe! Watu wakamkejeli Sadicky kwamba how come aombwe ingawaje wakati ule ule nilishasema Mecky Sadick ana kila sababu za kuwa mpole coz' hadi hapa tunapoongea Manji ndie anaonekana mwenye haki zote tofauti na taarifa ya hapo juu unless mahakama i-rule out vinginevyo au mamlaka za juu kabisa; zitengue maamuzi hayo ya mahakama ikiwa kuna mtu aliye juu ya sheria!!!
SAED KUBENEA:
Huyu nae haipaswi kukunja jamvi bila kumzungumzia kidogo kutokana na hatua yake ya kumtetea Mussa Natty, the ex-Kinondoni Director.
Kwamba Mussa Natty sie ambae aliuuza ufukwe wa Oysterbay kwa Manji ni kweli kwa 100% coz', mwaka 2007 Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni alikuwa Bw. Hussein Katanga ambae alitoka Kinondoni 2008. Kwahiyo Kubenea hapo yupo sahii. Mussa Natty amekuwa MD wa Kinondoni from 2013.
HOWEVER, hivi issue ni ufukwe kuwa mikononi mwa Yusuph Manji au ufukwe kuwa mikononi mwa sekta binafsi? Kama tatizo ni ufukwe kuendelezwa na Yusuph Manji basi Saed Kubenea alikuwa sahihi kumtetea Mussa Natty lakini ikiwa kinachonasisha CD ni ufukwe kuwa mikononi ya private sector basi Kubenea alichemka kumtetea Mussa Natty coz' ama uendelezwe na hao TIB na wenzake au uendelezwe na Manji; yote ni yale yale sana sana Kubenea atakuwa tu anachochea madai kwamba Mussa Natty ni mtu wao.