Ningependa kujua mwaka 2000 (kama sikosei) wakati Chadema walipoungana na CUF na kumsimamisha mgombea urais mmoja (Prof. Lipumba) ili swala la ruzuku na viti maalum lilitatuliwaje? Kama mwaka 2000 walipata mhafaka kuhusu ruzuku na viti maalumu kinachoshindikana kwa wakati huu ni nini?
Kwa maoni yangu muungano huu watakaofaidika ni CUF, Nccr na NLD kuliko Chadema maana CUF wana wabunge wawili (kama sikosei) wakuchaguliwa huku bara, na kwa hali ilivyo uwezekano wa Cuf kupata wabunge zaidi bila Ukawa ni mdogo..
Hivyo hivyo kwa NCCR wabunge ni watatu wa kuchanguliwa na hata hivyo mmoja keisha jiengua kwenda ACT na bila shaka hata hawa wawili waliobaki uwezekano wa kwenda ACT ni mkubwa kuliko kubaki NCCR, hivyo basi utaona hata kwa NCCR uwezekano wa kupata wabunge zaidi ya 3 haupo ila kwa kupitia Ukawa NCCR wanaweze kutapa walau wabunge 5 mpk 10 (ukijumlisha na wabunge wa NCCR walipo sasa)
NLD nayo stori ni ile ile..
Tukirudi kwa Chadema uwezekano wa kupata wabunge zaidi iwe ndani ya Ukawa au nje ya Ukawa ni mkubwa maana Chadema wamejijenga tangu mwaka 2010, viongozi wao wanaotarajia kugombea katika majimbo mbali mbali wameweka mzizi yao tangu mwaka 2010 tofauti na vyama vingine.
Hivyo basi ni muhimu kwa vyama vinavyounda Ukawa kuangalia kwa mapana faida zinazopatika wakiwa pamoja.. kuliko kuangalia faida wanazopata viongozi wa hivyo vyama.
Ukawa wekeni maslahi ya Watanzania mbele, watanzania wako tayari kwa mabadiliko..