Kama sikosei swala la wabunge wa viti maalum kwa limeanza mwaka 2005 au?Nimesema hivi: Ningependa kujua mwaka 2000 (kama sikosei) wakati Chadema walipoungana na CUF na kumsimamisha mgombea urais mmoja (Prof. Lipumba) ili swala la ruzuku na viti maalum lilitatuliwaje? Kama mwaka 2000 walipata mhafaka kuhusu ruzuku na viti maalumu kinachoshindikana kwa wakati huu ni nini?
Utaona kuwa swala la muugano wa vyama vya siasa si jambo geni kwani Cuf walishaungana na Chadema pia NCCR mageuzi walishaungana na Chadema katika urais.. Swali langu ni je swala la ruzuku lilitatuliwaje?
CUF na Chadema hawakuwahi kuungana bali walifikia maridhiano ya mwanzo kusimamisha mgombea Urais mmoja, wakati wakipingana Ubunge katika majimbo na walishindwa vibaya. Na 2005 kila mmoja alikwenda kivyake, Muafaka bora ulikuwa ule wa vyama vyote vya Upinzani baada ya uchaguzi huu (2005) lakini wakaja korofishana kwenye kugawana majimbo katika serikali ya mitaa 2009. Wwakabakia CDM na CUF, nao wakaweka Uhasama baada ya CCM na CUF kuweka muafaka juu ya Zanzibar..
Swala la Ruzuku haliwezi kutatuliwa na moyo wa kimaskini hata siku moja, isipokuwa kwa wao VYAMA kuungana. Kama mirathi wanapotaka ndugu kugawana mirathi, udugu huwekwa kando na mali imechukua nafasi kubwa. Kwa hiyo hapo hakuna UMOJA mnapogombania ruzuku za majimbo.