Club ya Wazee Ilala yarudi tena kwa kishindo!!!

justdoit

Member
Sep 2, 2009
63
4
Baada ya kufungwa kwa mda usiopungua miezi sita Club ya Wazee iliyopo mitaa ya Bungoni Ilala inerudi tena chini ya Uongozi mpya ikiwa na sura tofauti kabisa.

Wahudumu ni wakuvutia,huduma ni ya Haraka,Chakula ni cha ukweli.Katika pitapita zangu huko ilala mitaa ya bungoni kwa mbali nilianza kusikia muziki wa Country ukipig ndipo nikajongea taratibu.Nilipofika hapo Club ya Wazee niliona wahudumu waliovalia vizuri wakiongozwa na meneja wao na ndipo nilipogundua kwamba Club ya Wazee imerudi tena kwa mara nyingine.

Niliposogelea uongozi nikaamiwa kwamba club ya wazee imerudi tena chini ya Ungozi mpya na hii ni soft opening tu.ufunguzi rasmi ni Iddi Mosi.

Nafikiri wadau wote mtakubaliana nami kwamba club ilikuwa ni sehemu ambayo ikikutanisha watu wa kila aina kulingana na mazingira yake ya kuvutia na Huduma safi ambayo ilikuwa ikipatikana pale. Ni mojawapo ya Club ambayo huwezi kuona fujo hata siku moja kutokana na Heshima ambayo imejijengea na wateja wake wastaarabu tofauti na Baa nyingine ambazo ni fujo mtindo mmoja.
 
Back
Top Bottom