Clouds TV yaondolewa katika channel lists za digitali

Clouds TV yaondolewa katika channel lists za digitali

Opaque

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2008
Posts
1,359
Reaction score
727
Mambo sio mambo kwa kituo cha runinga cha Clouds TV. Baada ya signal kuwa scrambled usiku wa kuzima mitambo ya analojia, Clouds walikomaa hivyo hivyo kwenye list ya king'amuzi cha Star Times na wakavumiliwa kuendelea kuwepo katika list huku ikiwa channel isiyoonyesha picha yoyote. Jamaa walijitutumua na kupitisha mkanda wa ujumbe katika channels nyingine wakiomba huruma kwamba bado wapo 'dijitali' isipokuwa mafundi wao wanarekebisha mambo.

Hata hivyo uvumilivu umewashinda Star Media (Times) na wameiondoa kabisa Clouds TV katika channels list yao. Ngoma inaanza moja, wazee wa procurement mpo? Kaeni mkao wa ku-bid tender ya kuleta mitambo ya dijitali!
 
Hongera sana Serikali kwa kuwabana wajanja wanjanja clouds tv
 
Siamini macho yangu.

Sent from my GT-P7500 using Tapatalk 2
 
Mi nimeshangaa leo kutwa clouds tv hawapo hewani ktk startimes.
 
Hata kwenye king'amuzi cha ting toka jana ucku clouds tv haionekani!
 
Wao sio ndio wanajiita wajanja wa mjini?! Kumbe kwenye kijiti walikuwa wanataka kuingia ki ujanja ujanja pia?
 
Kwanini wasiwe kama channels nyinginezo wawe na frequency zao ambazo hata sisi wenye dishi za kawaida mikoa tuwapate kirahisi kama channel ten, itv, startv na nyinginezo.
 
Afadhali wameitoa ilikuwa inaniongezea muda wa kuscrol wakati natafuta channel za maana. Sikujua kama ndo pacha wa clouds porojo
 
serikali ilisema tv za ndani zilizo sajiliwa ni tano tu! so inawezekana kwenye hizo tv tano zilizo sajiliwa tv mfu hawamo. mia

Kwa mujibu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) nchi ina vituo 5 tu vilivyo sajiliwa vya televisheni (ITV, EATV, STAR TV, CHANNEL TEN & TBC1 tu) vituo vingine vyote ni community broadcasters tu a.k.a Tv za chumbani..hata wewe ukiamua kuanzisha sawa tu!
 
Back
Top Bottom