Kituo cha television cha clouds, kwa kweli kwenye upande wa tv mlikuwa hamjajipanga kabisa kifupi mlikurupuka!!
Kwani haiwezekani kwa matukio ya habari yanayotokea nchini kila siku, nyie mnakuwa na habari moja tu!
Mfano leo local news wametangaza habari moja tu, na jicho la mwewe, eti taarifa ya habari imekwisha!!!
Kwani lazima muwe na taarifa za habari??!!
Mkuu we umeliona leo hili? Lipo Kitambo saaana
Juzi bila mkutano wa CCM wasingekuwa na habari hata moja,maana walipiga hiyo habari kwa urefu kisha Mwewe Mchepuko huyoo(Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni,Kitengo cha Jicho la Mwewe nakikubali saana)
Sasa kali zaidi,hawana muda maalum wa Taarifa ya Haabri,Schedule yao inasema saa Moja na Nusu,ila wanakupigia mbili kasobo,wamewahi saaana mbili kasoro dak 20 au 25.
Habari zao za Ndani haizidi dakika 5 wamemaliza,na ndio maana huwa wanaanza na Ngonjera kwanza Kama mrisho mpoto,hadi uje upate habari umeishaletewa madudu teleee hata yasioendana na tukio,sijui nani kawaambia hii style ni nzuri,maana usipokuwa makini unaweza hata usielewi kama taarifa ya Habari.
Clouds Ni Chama langu ila kwa Hili wapo Hovyo kabisa
Mie Clouds naangalia Kipindi cha Michezo tu cha Usiku kina Shaffii Dauda basi kile cha Sports Bar,maana pale mpange mzima.
Na pia Antonio Nugaz kwenye Kipindi Cha Kambi Popote,Big up Brother hili ni Bonge la Kipindi
Ila taarifa ya Habari waachie wenye Fani zao
Ila lazima tujue kwamba umaskini nao ni Janga,walikurupuka kuatangaza Taarifa ya Habari bila kujua kwamba Cameras kwa Reporters inabidi ziwe za Kutosha.Sasa utakuta Camera ikienda kenye mkutano basi kama reporter hajapata tukio jingine wakati anarudi studio basi ndio imetoka,hahahah aiseee