Clouds kwa hili la Clouds Plus mmezidi!

Clouds kwa hili la Clouds Plus mmezidi!

Ni ajabu wewe kila kitu unatafuta jinsi ya kuteka pesa iwe kiharali ama kwa mizengwe. Sie watumiaji wa Azam TV tuna vifurushi vyetu 3 ambavyo kwa idadi ya chaneli zote zilizopo zitapatikana pale utakapoweza kulipia kile cha juu kabisa. Sasa sijui huu ndo utaratibu gani kwamba unaamua kachaneli kako ka clouds plus basi wewe unaingia na kifurushi chako cha kipekee kabisa na unahitaji 3000.

Kwamba naweza nikalipia kifurushi cha juu kabisa na nikapata zote ziwe za ndani ama nje, michezo ama habari, vichekesho ama burudani na ntazipata zote isipokuwa ile ya kwako ya Clouds Plus. Hii ni hatari, inaonesha ni kwa kiasi gani wewe ni wa kipekee lakini pia labda chaneli yako ni ya kipekee na nzito kupita zote katika dekoda nzima ya Azam TV .

Najiuliza tu, ikiwa na Azam angesema sie wanamichezo tunatakiwa kulipia labda 5000 kwa ajiri ya chaneli ya Azam sports2 na labda ikasemwa pia kwa sie wafatiliaji wa muvi za Nigeria tukaambiwa tulipie 3000 ili kuiona Chaneli ya AMC sielewi kama leo watizamaji tungeweza kweli kugharamia dekoda kama dekoda na bado tukaweza kumudu kulipia kila chaneli kwa pesa yake. Tunamshukuru sana Bakhresa kwa hili ijapo bado wengi wetu tunajiuliza ni nini haswa nia ya Ruge na Clouds Plus yake.

Kama ni njaa ya pesa basi hii itakuwa ni hatari sana. Tunaelewa umetoka kuchukua viingilio vya ndondo, sahivi unajiandaa kupiga za Fiesta na bado inakuingia akilini kuchajisha bei yako kwa ajiri ya chaneli yako tukufu. Huu kama siyo kukosa utu na aibu basi itakuwa ni tamaa kali sana. Ingekuwa ndo mwendo kwamba tulipie kila kitu kwa kitu sijui kama kweli tungefika, haya bwana.
Ruge amewaiga Sibuka Tv kule Star times!
 
Mifeleji Ya Pesa YA Lazma 1, Ving'amuz 2. Bando Na Dakk APO NIMEACHA POMBE ,SIGARA, DELILA, NDUGU NA MIZINGA 4M ENE WEA
 
Kwani unachokitafuata ktk tv kipo ktk channel ya ckouds plus?kama ni michezo,habari,movies unapata ktk chanel nyingi tofauti tofauti!achane kulalama mkuu!kwani haujui iyo ni biashara!?
 
Hata super sport hawajawahi Fanya huu upuuzi sembuse huu upuuz wa fiesta

usisahau vya kusahau kabla kusahau hAkujakusahau wewe uliye sahau
 
Ile chaneli sijui inavipindi gani vya maana...
 
Wanafanya Research ya watakao jiunga na jinsi itakavyo walipa! Mbona mwanzoni waliiweka bila kulipwa? Ni chaguo lako tu kulipia au kuacha, tupo Katika ushindani wa biashara za soko huria. Kama ni muhimu sana hiyo channel lipia tu usiutese moyo wako, maisha yenyewe mafupi haya kuliko kuangalia channel zisizojulikana.
 
Acha kulalama....hiyo ni add-on channel, lipa hela uione....
Azam wanazo add ons nyingi za kihindi...not a new phenomenon...
Kama huna hela tulizana na package uliyolipia, siyo kuja kutujazia sever kwa useless thread...

Sent using Jamii Forums mobile app
Watanzania watu wa hovyo sana na ndo maana mnatesana sana na kuishi kwa visasi. Sishangai kuona wenzetu wakilalamika kwenye huduma kuongezeka hata senti lakini kwa hapa Tz utaitwa mwehu ... Labda kwa kukusaidia, si kila anayesema basi kashindwa hilo jambo.

Naamini nimeanza kuitumia Azam hata kabla labda hujawaza kuitumia kama kweli unayo na huu ni mwaka wa 5 sasa unaisha naitumia Azam na ukitaka reg# yangu pia ntakupa ukahiki. Nimelipa vifurushi vyote kwa utashi wangu na hakuna mwezi sijalipia wala kukwama kulipa.

Kwahiyo usifikilie tunaongea kisa hatuwezi kumudu ama labda ni pesa nyingi, lah! Tunaongea kama watanzania na kama jamii ya watanzania. Tunaelewa pia ni soko huria lakini mwanadamu unahitaji kuhoji na kutafiti kwasababu una utashi na haliwezi kuwa kosa. Si ajabu kuhoji kwangu hapa kuna kitu nadevelop ambacho wewe huwezi kukielewa badala yake utaona tu eti watu wanalalamika.

Usipende kudharau vitu vidogo ukafikiri ni vikubwa pekee ndo vinakufanya kuwa mwanadamu ama kwasababu tu wewe vidogo vyote unavyo. Katika kuongea hivi tunapata nafasi ya kuwasaidia wengine wengi sana na ndo maana ya kuongea haijalishi hicho kitu kwako kinahusika kiasi gani.
Grow big and not fat!
 
Mkuu aisee hata me nimeshangaa jaman ndio hivyo tunaopenda ile channel inabidi tujiunge tu kwa shingo upande ila hawatutendei hakiii kabisaa
siangaliagi hiyo channel,kwani ina nini very special?
 
Umeyataka mwenyewe,, acha wenzio watumie fursa,, we endelea kupiga kelele hapa wakati kuna watu wanalipia tuuu,,
 
That how capitalist work to exploit the surplus population

Let's the game begin

Nampenda shunie........

Don't mind me
 
Download Afrobox japo ni yao, me naTafuta App ambayo in Channels za tz, at the end huyu lazma niangalie kvyovyote bila buku3.
 
Ni ajabu wewe kila kitu unatafuta jinsi ya kuteka pesa iwe kiharali ama kwa mizengwe. Sie watumiaji wa Azam TV tuna vifurushi vyetu 3 ambavyo kwa idadi ya chaneli zote zilizopo zitapatikana pale utakapoweza kulipia kile cha juu kabisa. Sasa sijui huu ndo utaratibu gani kwamba unaamua kachaneli kako ka clouds plus basi wewe unaingia na kifurushi chako cha kipekee kabisa na unahitaji 3000.

Kwamba naweza nikalipia kifurushi cha juu kabisa na nikapata zote ziwe za ndani ama nje, michezo ama habari, vichekesho ama burudani na ntazipata zote isipokuwa ile ya kwako ya Clouds Plus. Hii ni hatari, inaonesha ni kwa kiasi gani wewe ni wa kipekee lakini pia labda chaneli yako ni ya kipekee na nzito kupita zote katika dekoda nzima ya Azam TV .

Najiuliza tu, ikiwa na Azam angesema sie wanamichezo tunatakiwa kulipia labda 5000 kwa ajiri ya chaneli ya Azam sports2 na labda ikasemwa pia kwa sie wafatiliaji wa muvi za Nigeria tukaambiwa tulipie 3000 ili kuiona Chaneli ya AMC sielewi kama leo watizamaji tungeweza kweli kugharamia dekoda kama dekoda na bado tukaweza kumudu kulipia kila chaneli kwa pesa yake. Tunamshukuru sana Bakhresa kwa hili ijapo bado wengi wetu tunajiuliza ni nini haswa nia ya Ruge na Clouds Plus yake.

Kama ni njaa ya pesa basi hii itakuwa ni hatari sana. Tunaelewa umetoka kuchukua viingilio vya ndondo, sahivi unajiandaa kupiga za Fiesta na bado inakuingia akilini kuchajisha bei yako kwa ajiri ya chaneli yako tukufu. Huu kama siyo kukosa utu na aibu basi itakuwa ni tamaa kali sana. Ingekuwa ndo mwendo kwamba tulipie kila kitu kwa kitu sijui kama kweli tungefika, haya bwana.
Mbaya zaidi hiyo channel haina lolote la maana, utumbo mtupu. Angeanzisha tu na yeye king'amuzi chake afanye aina ya biashara aitakayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muhaya Hugo anajuwa kuitafuta pesa. Lakini mmsiezi kulipia 3000 kwa Chanel ya movie za kibongo
 
MTU hujalazimishwa kulipia povu jiiiiingi shida n nn kwan? Anatumia gharama kuandaa fiesta we ulitaka uone bure kama nan?... Pesa inawekwa juu ya pesa ili izae hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii Mara papu fiesta hii hapa...usichukie wala nn mkuu fursa ndio hiyo
 
U
Ni uzembe wa TCRA
Umeelewa mkuu, kuna watu hawaelewi kwamba hili ni zao la udhaifu fulani katika mamlaka ila kwa upeo wao watakujadiri wewe uliyeamua kusema kana kwamba umeongea kitu cha hovyo. Ni lazima tukiri hili ni ombwe na si suala la kusema eti "hujalazimishwa, si lazima, kama huwezi uache" n.k. Hizi kauli ni kukwepa ama kulinda udhaifu uliopo badala yake unaamua kuuzunguka mbuyu kwasababu huwezi ama kwenye hilo wewe ni kanyanga
 
U
Ni uzembe wa TCRA
Umeelewa mkuu, kuna watu hawaelewi kwamba hili ni zao la udhaifu fulani katika mamlaka ila kwa upeo wao watakujadiri wewe uliyeamua kusema kana kwamba umeongea kitu cha hovyo. Ni lazima tukiri hili ni ombwe na si suala la kusema eti "hujalazimishwa, si lazima, kama huwezi uache" n.k. Hizi kauli ni kukwepa ama kulinda udhaifu uliopo badala yake unaamua kuuzunguka mbuyu kwasababu huwezi ama kwenye hilo wewe ni kanyanga
 
Back
Top Bottom