Clouds FM Michezo: Kiswahili- Kiingereza cha nini?

Clouds FM Michezo: Kiswahili- Kiingereza cha nini?

ngumbuke

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
502
Reaction score
535
Labda nijitambulishe kuwa mimi ni mdau wa Lugha ya Kiswahili na mpenzi wa hiki kituo cha Redio.
Kwa kweli nakereka mno na watangazaji wa kipndi cha michezo cha Redio hii akina Edgar, Lwambano, Jeff na wengine kutuchanganyia lugha.
Sielewi kwa nini wasitumie lugha moja tu? Amueni lugha ya kuendeshea kipndi chenu iwe ipi? Kuchanganya lugha ni ishara kuwa ninyi hamzifahamu lugha hizo vilivyo?
Hebu jisikieni fahari kuiongea na kuitumia lugha hii kwenye matangazo yenu!
 
Labda nijitambulishe kuwa mimi ni mdau wa Lugha ya Kiswahili nya mpenzi wa hiki kituo cha Redio.
Kwa kweli nakereka mno na watangazaji wa kipndi cha michezo cha Redio hii akina Edgar, Lwambano, Jeff na wengine kutuchanganyia lugha.
Sielewi kwa nini wasitumie lugha moja tu? Amueni lugha ya kuendeshea kipndi chenu iwe ipi? Kuchanganya lugha ni ishara kuwa ninyi hamzifahamu lugha hizo vilivyo?
Hebu jisikieni fahari kuiongea na kuitumia lugha hii kwenye matangazo yenu!
Anayechanganya lugha ni Jeff.Yule ni mkenya
 
Anayechanganya lugha ni Jeff.Yule ni mkenya

Jeff sio mkenya bali ni mtanzania ila shule ya msingi alisoma Kenya na sekondari alisoma Tanzania form 1 hadi form 2 Makongo form 3 na 4 alisoma Tegeta na kuhitimu mwaka 2004.
 
Tatizo hizi radio mbao hazina utaratibu kabisa. Mtu anaongea kiswahili mara kadakia kingereza basi tu ilmradi vurugu. Hasa akina dada watangazaji wanadhani kuongea kingereza kwa lafudhi ya kizungu ndio ujanja kumbe upumbv mtupu.
 
Jeff sio mkenya bali ni mtanzania ila shule ya msingi alisoma Kenya na sekondari alisoma Tanzania form 1 hadi form 2 Makongo form 3 na 4 alisoma Tegeta na kuhitimu mwaka 2004.

Bora mie ninaesikiliza Praise Power au WAPO masaa 24. Sikutani na kero za kijinga kama hizo zaidi ya furaha na raha ya nafsi na roho
 
Labda nijitambulishe kuwa mimi ni mdau wa Lugha ya Kiswahili na mpenzi wa hiki kituo cha Redio.
Kwa kweli nakereka mno na watangazaji wa kipndi cha michezo cha Redio hii akina Edgar, Lwambano, Jeff na wengine kutuchanganyia lugha.
Sielewi kwa nini wasitumie lugha moja tu? Amueni lugha ya kuendeshea kipndi chenu iwe ipi? Kuchanganya lugha ni ishara kuwa ninyi hamzifahamu lugha hizo vilivyo?
Hebu jisikieni fahari kuiongea na kuitumia lugha hii kwenye matangazo yenu!

Mimi mpaka sasa sina hamu ya kusikiliza kabisa maana wanakera sana
 
Hizo niredio za FIESTA Mtangazaji anaingia studi hajui anaingia kufanya nini wanafamya studio ni kijiwe cha kupiga porojo si unajua nchi yangu kwa POROJO hatujambo
 
nawachukiaje watu wanakubali kuwa watumwa wa lugha za kigeni na kuona ndio fasheni.
Nalog off
 
Tatizo hizi radio mbao hazina utaratibu kabisa. Mtu anaongea kiswahili mara kadakia kingereza basi tu ilmradi vurugu. Hasa akina dada watangazaji wanadhani kuongea kingereza kwa lafudhi ya kizungu ndio ujanja kumbe upumbv mtupu.


Tena inakera mno!
Nahisi furaha kumsikiliza mama Tibaijuka akizungumza kiingereza chenye ladha ya kihaya au wale waigizaji wa filamu za kinaijeria wanapozungumza kiingereza katika lafudhi ya kikwao.
Acheni ushamba, kama kipindi ni kwa lugha ya Kiswahili, lugha husika itumike.

Kiswahili ndiyo lugha yetu,
Tuiongee kivyetu vyetu,
Tusiichanganye na ya wenzetu,
Na iwe ndo chakula chetu.
Tubadilike!
 
huo ni ugonjwa wetu watanzania wengi kuanzia huko mashuleni mpaka mavyuoni mbona hatulalamiki kwann sekondari tunafundishwa kwa kiingereza wakati sisi lugha yetu ni kiswahili?
 
Back
Top Bottom