Clouds FM: Katika hili mnastahili pongezi

Ni juhudi nzuri kwa kweli. Hela zikishachangwa zinapelekwa kwa nani ambaye anapeleka misaada kwa wahanga?

Gazeti la Habari Leo limeuliza vizuri
Maafa ya Kilosa yasigeuzwe mtaji
Imeandikwa na Neophitius Kyaruzi; Tarehe: 27th January 2010

KWANZA nichukue fursa hii kuwapa pole waathirika wa mafuriko yaliyotokea Kilosa, Morogoro ambao sikupata bahati ya kuwasiliana nao tangu walipopatwa na maafa hayo.

Pili, nipongeze watu au taasisi zilizojitolea kwa hali na mali kuwasaidia waathirika hawa, kwani mchango wao umewarahisishia kidogo ugumu wa maisha wanaokabiliana nao hivi sasa.

Baada ya kusema hayo sasa nizungumzie jambo muhimu ambalo tunapaswa kulizingatia katika kipindi hiki na siku nyingine, iwapo Taifa letu litakumbwa na mahafa kama hayo.

Kwa wanaofutailia vyombo vya habari, bila shaka, watakuwa wamesikia juu ya njia mpya ya ukusanyaji fedha kwa ajili ya waathirika kwa kutumia simu za mkononi.

Njia hiyo ambayo inatumia teknolojia ya kisasa ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu hizo inaendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.

Ukweli ni kwamba teknolojia hiyo si ngeni nchini, kwani tumekuwa tukiishuhudia katika kampuni nyingi za simu zikiitumia kukusanya fedha kupitia mashindano kama vile maoni ya kipima joto, promosheni za kushindania magari, bahati nasibu ya Kismat Sms, Pata Vichekesho, Mistari ya Biblia na nyingine nyingi.

Kinachofanyika katika teknolojia hiyo ni kwamba kampuni hizo zimekuwa zikikusanya fedha kwa njia ya kielektroniki huku wateja wakipeleka fedha halisi kwenye kampuni hizo kwa kununua zaidi muda wa maongezi.

Ukweli ni kwamba njia hiyo ya ukusanyaji fedha imekuwa na mafanikio makubwa, kiasi kwamba hivi sasa hakuna biashara inayovuna fedha nyingi za walalahoi kama huduma za simu za mikononi, hasa kwa kutumia mbinu hiyo.

Kwa kutambua ukweli huo, baada ya Vodacom kuombwa na wadau wa ukusanyaji fedha kwa ajili kusaidia wathirika wa maafa, imekubali kukusanya fedha kwa njia ya wateja wake kutuma ujumbe mfupi wa maneno ambapo kwa kila ujumbe (Maafa), mteja atakatwa Sh 250 katika akaunti yake ya muda wa maongezi, hivyo atakuwa amechangia waathirika kwa njia hiyo.

Kilichonishangaza ni kwamba gharama hizo pia zinahusisha asilimia 20 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), wakati Serikali inatambua kwamba fedha zinazokusanywa ni za dharura kwa ajili ya kukabiliana na maafa.

Hivi kweli ni sahihi kutoza kodi walalahoi wanaojitolea kuwasaidia wenzao katika maafa? Kodi hii ya nini kama fedha hizo si za kibiashara?

Jambo lingine la kushangaza, ni kwamba wakati tunahamasishwa kuchangia, hakuna maelezo yanyoonesha mgawanyo wa fedha hizo na kiasi gani kinachohitajika kukamilisha sehemu ya msaada inayohitajika.

Wakati huo huo, hatujui kiasi gani kitapelekwa kwa waathirika na kiasi gani kitabaki Vodacom. Najiuliza maswali haya kwa kuwa kiasi kinachokusanywa kwa kila SMS ni kikubwa, kwani ni sawa kabisa na kiwango ambacho kimekuwa kikikusanywa katika mashindano mengi ya bahati nasibu ambayo huendeshwa na kampuni za simu ikiwamo Vodacom.

Kampuni kama Vodacom yenye wateja zaidi ya milioni saba, iwapo wateja wake milioni mbili, kila mmoja akituma ujumbe mmoja kwa siku itakuwa imekusanya Sh milioni 500 - kwa siku, ikiwa kiasi hicho hicho kitakusanywa kwa siku 30 nadhani fedha hizo zinaweza kutumika kuwajengea waathirika wote nyumba za gharama nafuu za matofali ya kuchoma na kuwapa mitaji ya kuanzia maisha.

Kutokana na ukweli huo, tunapaswa kuhoji mchanganuo wa mgawanyo wa fedha hizo, tusijikute tunafaidisha kundi fulani huku waathirika wakiendelea kukabiliwa na umaskini. Ukweli ni kwamba makusanyo mengine yamekuwa yakionekana kama yana lengo la kuisaidia jamii, kumbe mwisho wa siku yananufaisha kundi fulani tu, mifano ipo mingi, chunguzeni!
 
Mwanakijiji nahisi unavisa na Hawa watu basi tupige kampeni ya kuamua mambo haya yawe wazi tunavyochanga tuelezwe imetumikaje na mahesabu yawekwe wazi kwa watu wote kwenye magazeti na kadhalika lakini hilo lianzie hapa ambapo kuna watu wanachangia jf , wengine TPN and so on , tuanze na sisi kama mfano
 
Mwanakijiji nahisi unavisa na Hawa watu basi tupige kampeni ya kuamua mambo haya yawe wazi tunavyochanga tuelezwe imetumikaje na mahesabu yawekwe wazi kwa watu wote kwenye magazeti na kadhalika lakini hilo lianzie hapa ambapo kuna watu wanachangia jf , wengine TPN and so on , tuanze na sisi kama mfano

Mara ya mwisho Vodacom Foundation kuchangisha watu ili iweze kupata fedha za kusaidia majukumu yake ilikuwa lini? Michango yetu sisi imeshawekwa wazi angalia kule kwenye sticky points na michango yetu (japo kiduchu) ya sehemu ya pili tunakabidhi Ijumaa hii kwa Chama cha Msalaba Mwekundu.

Shy, ungependa Vodacom Foundation wachangie chama cha Msalaba Mwekundu au la?
 
Ningependa kuona hivyo lakini wana foundation yao yenye malengo ya kusaidia jamii kwa namna mbalimbali kwahiyo watumie yao kama wanaona inaweza kufanya kile wanachotaka wao
 
Ningependa kuona hivyo lakini wana foundation yao yenye malengo ya kusaidia jamii kwa namna mbalimbali kwahiyo watumie yao kama wanaona inaweza kufanya kile wanachotaka wao

kwa hiyo mchango huu unaoendelea sasa ni kuwachangia walioapatwa na maafa ya mafuriko au ni kuchangia Vodacom Foundation ili ipate uwezo wa kusaidia waliopatwa na maafa?
 
MKJJ nachosema Neophitius Kyaruzi ni sahihi kabisa ila inabidi kuwa waangalifu in future tusije tukazuia watu kusaidia wahanga kutokana na tunayofanya hivi sasa.

I can see the problem that Vodacom is facing now; I do believe kuwa kweli wanajitangaza lakini tunaweza kuondoa hizo tuhuma kwa kuangalia their past experience. Vodacom foundation wamejitahidi kujenga shule na misaada mbalimbali yet hatujawasema kuwa wanajitangaza! japo walikuwa wanajitangaza! kila wakifanyacho wao ni kujitangaza, haizuiliki!

This is an unavoidable circumstances because that could trigger a questions kuwa hata sisi JF tulijitangaza, TPN, Clouds , watakuja watu binafsi, tutasema wanapiga kampeni....

I think what we should learn here is that there must be a watchdog from government that can oversee these issues, kuwa kama Vodacom wanataka kuchangisha wakatoe taarifa na wamulikwe, same to Clouds FM, etc cha kuangalia ni kuondoa mlolongo! This government agency wanaweza wakawa wanatoa matuzo/prizes za heshima kwa hayo makampuni etc
 
Kilichonishangaza ni kwamba gharama hizo pia zinahusisha asilimia 20 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), wakati Serikali inatambua kwamba fedha zinazokusanywa ni za dharura kwa ajili ya kukabiliana na maafa.

Hivi kweli ni sahihi kutoza kodi walalahoi wanaojitolea kuwasaidia wenzao katika maafa? Kodi hii ya nini kama fedha hizo si za kibiashara?

Hayo mengine ya mgawanyo nk pengine ni sawa lakini hapo kwenye suala la kodi mtawabebesha Voda lawama za bure tu. Tatizo lipo kwenye sheria zetu za kodi ambazo hazitoi unafuu inapokuja huduma za namna hii. Tatizo jingine lipo kwenye mfumo wenyewe kwenye makampuni yote ya simu (sio Voda pekee). VAT na ushuru inakusanywa na serikali pale vocha inapouzwa sio baada ya kutumika hivyo kimsingi matumizi yoyote ya salio (airtime) yanakuwa yameshatozwa kodi. Pengine ingeweza kuepuka kodi endapo michango hiyo isingetumia mfumo wa SMS na airtime.
 
kwa hiyo mchango huu unaoendelea sasa ni kuwachangia walioapatwa na maafa ya mafuriko au ni kuchangia Vodacom Foundation ili ipate uwezo wa kusaidia waliopatwa na maafa?
VodaCom hawataki kupitisha michango hii kule Red Cross kama TPN walivyofanya. Kilichonishangaza mimi ni Clouds kupitisha michango hii VodaCom ndipo iende kunakohusika! Mlolongo huu una gharama zake pia.
 
MKJJ nachosema Neophitius Kyaruzi ni sahihi kabisa ila inabidi kuwa waangalifu in future tusije tukazuia watu kusaidia wahanga kutokana na tunayofanya hivi sasa.

I can see the problem that Vodacom is facing now; I do believe kuwa kweli wanajitangaza lakini tunaweza kuondoa hizo tuhuma kwa kuangalia their past experience. Vodacom foundation wamejitahidi kujenga shule na misaada mbalimbali yet hatujawasema kuwa wanajitangaza! japo walikuwa wanajitangaza! kila wakifanyacho wao ni kujitangaza, haizuiliki!

This is an unavoidable circumstances because that could trigger a questions kuwa hata sisi JF tulijitangaza, TPN, Clouds , watakuja watu binafsi, tutasema wanapiga kampeni....

I think what we should learn here is that there must be a watchdog from government that can oversee these issues, kuwa kama Vodacom wanataka kuchangisha wakatoe taarifa na wamulikwe, same to Clouds FM, etc cha kuangalia ni kuondoa mlolongo! This government agency wanaweza wakawa wanatoa matuzo/prizes za heshima kwa hayo makampuni etc

Waberoya, tatizo ambalo naliona kwenye suala hili ni kuwa Vodacom hawaweki wazi ni nani anachangiwa; ndio maana shy anashindwa kujibu swali langu moja hapa.

a. Michango inaoitishwa na vodacom inapelekwa kwa nani? - Vodacom Foundation.

b. Kwa vile (tunaamini hivyo kutokana na past experience) Vodacom wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali ya kijamii huko nyuma basi tunaamini wanakusanya fedha ili kuawsaidia wahanga wa mafuriko.

c. Kama (b) ni kweli swali langu ambalo bado sijapatiwa jibu vizuri ni kuwa kwanini miaka yote hii Vodacom Foundation imekuwa ikitoa misaada mbalimbali bila kwenda radioni kutafuta misaada. Hivi kweli, kama wakichangisha leo na kupata milioni 7 tunaweza kusema wamefanikiwa? Yawezekana kuwa Vodacom Foundation iko katika hali mbaya ya kifedha kiasi cha kuhitaji misaada ya kuchangiwa. Kama hili ni kweli mimi naunga mkono.

d. Kati ya Vodacom Foundation na Red Cross Society ni Red Cross Society inayohitaji msaada zaidi, ina miundo mbinu ya kupeleka misaada na ina mfumo na uzoefu wa kushughulikia majanga makubwa. Hii ndiyo sababu baada ya tetemeko la ardhi la Haiti taasisi ya kwanza kuanza kuchangiwa ni Red Cross Society ya huko.

e. Je Vodacom Foundation itatoa baadhi ya fedha inayokusanya kwenda kwa Red Cross ili kukipa nguvu chama hicho?

f. Sisi michango yote tunayokusanya kwenye kampeni yetu (kiduchu as it may) tunapeelka kwa Red Cross Society. NI asilimia ngapi ya michango ya sasa inayopelekwa kwa Red Alert itatumika sasa hivi kwa wahanga wa sasa na kiasi gani kitabaki kwa majanga ya baadaye?
 
VodaCom hawataki kupitisha michango hii kule Red Cross kama TPN walivyofanya. Kilichonishangaza mimi ni Clouds kupitisha michango hii VodaCom ndipo iende kunakohusika! Mlolongo huu una gharama zake pia.

Wildcard, kwanini Vodacom Foundation inahitaji kuchangiwa ili iweze kutoa misaada?
 
Hayo mengine ya mgawanyo nk pengine ni sawa lakini hapo kwenye suala la kodi mtawabebesha Voda lawama za bure tu. Tatizo lipo kwenye sheria zetu za kodi ambazo hazitoi unafuu inapokuja huduma za namna hii. Tatizo jingine lipo kwenye mfumo wenyewe kwenye makampuni yote ya simu (sio Voda pekee). VAT na ushuru inakusanywa na serikali pale vocha inapouzwa sio baada ya kutumika hivyo kimsingi matumizi yoyote ya salio (airtime) yanakuwa yameshatozwa kodi. Pengine ingeweza kuepuka kodi endapo michango hiyo isingetumia mfumo wa SMS na airtime.

You have quoted a wrong person ndugu..
 
Wildcard, kwanini Vodacom Foundation inahitaji kuchangiwa ili iweze kutoa misaada?
Hapa nyumbani siku hizi polisi wetu wana kitu kinaitwa ulinzi shirikishi. VF nao wanawashirikisha wateja wao kwenye hili sambamba na kujinadi pia!
 
Waberoya, tatizo ambalo naliona kwenye suala hili ni kuwa Vodacom hawaweki wazi ni nani anachangiwa; ndio maana shy anashindwa kujibu swali langu moja hapa.

a. Michango inaoitishwa na vodacom inapelekwa kwa nani? - Vodacom Foundation.

b. Kwa vile (tunaamini hivyo kutokana na past experience) Vodacom wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali ya kijamii huko nyuma basi tunaamini wanakusanya fedha ili kuawsaidia wahanga wa mafuriko.

c. Kama (b) ni kweli swali langu ambalo bado sijapatiwa jibu vizuri ni kuwa kwanini miaka yote hii Vodacom Foundation imekuwa ikitoa misaada mbalimbali bila kwenda radioni kutafuta misaada. Hivi kweli, kama wakichangisha leo na kupata milioni 7 tunaweza kusema wamefanikiwa? Yawezekana kuwa Vodacom Foundation iko katika hali mbaya ya kifedha kiasi cha kuhitaji misaada ya kuchangiwa. Kama hili ni kweli mimi naunga mkono.

d. Kati ya Vodacom Foundation na Red Cross Society ni Red Cross Society inayohitaji msaada zaidi, ina miundo mbinu ya kupeleka misaada na ina mfumo na uzoefu wa kushughulikia majanga makubwa. Hii ndiyo sababu baada ya tetemeko la ardhi la Haiti taasisi ya kwanza kuanza kuchangiwa ni Red Cross Society ya huko.

e. Je Vodacom Foundation itatoa baadhi ya fedha inayokusanya kwenda kwa Red Cross ili kukipa nguvu chama hicho?

f. Sisi michango yote tunayokusanya kwenye kampeni yetu (kiduchu as it may) tunapeelka kwa Red Cross Society. NI asilimia ngapi ya michango ya sasa inayopelekwa kwa Red Alert itatumika sasa hivi kwa wahanga wa sasa na kiasi gani kitabaki kwa majanga ya baadaye?

Asante kwa ufafanuzi nimewauliza watu hapo kwanza sikupata jibu nilihisi kuna tatizo somewhere na watu walikuwa wanaongea lugha wanayoelewana wao. Now I know the problem...

Kama haijawekwa wazi basi ni hatari hasa kwa watoaji, walitakiwa kuwa na mwakilishi wa Redcross hapo studio ambaye anaona shughuli nzima inaendaje( huyo jamaa wa red cross naye angekuwa anatoa maneno mawili matatu) Hii wataalamu wa sociology wanaita social license. Kuwa kampuni inapata undisputable licence from everyone katika society; hii inawaongezea credibility wao kama kampuni.

Sadly makampuni mengi yanakurupuka bila kufanya hii partial risk assessment.
 
La kushangaza ni kwa nini wameamua ku-team up na VODACOM badala ya kujisimamia wao wenyewe kama wanavyofanya kwenye fiesta zao.
Vodacom started it and the aim is to help the floods affected kilosa people. This is not about ingenuity but it is about raising funds for helping people. They are trying to let people know they have responsibility to help the society especially the musicians and other artists who also normally get a lot of money through people voting for them through sms should also show their full partcipation in this and that is what was the goal for Cloudsfm.
They are shouldering with what TPN, Jamii Forums had earlier started. They have taken their air time to back up the initiative. Bravo to Clouds FM and big claps for them. But the money/contributions of whatsoever nature should reach the intended society!!!!!
 
utaona kuwa uliyoyanukuu hayakuwa maneno yangu..

Hilo ni kweli na nililiona. Nimejaribu kuelezea tu kwa ujumla kwa sababu nimeona linajitokeza na kuna uwezekano ukatokea upotoshaji.

Kama imekutatiza, niwie radhi tu.
 
Hilo ni kweli na nililiona. Nimejaribu kuelezea tu kwa ujumla kwa sababu nimeona linajitokeza na kuna uwezekano ukatokea upotoshaji.

Kama imekutatiza, niwie radhi tu.

not really... sikutaka kutake credit za mtu mwingine.
 
Back
Top Bottom