Ukisoma hili jarida la high times (lipo mtandaoni) utaona kwamba kipindi cha bob jamaica kulikua na vyama viwili vya siasa vyenye nguvu sana JLP na PNP, PNP kilikua na sera za Ki socialist wakati JLP sera zao zilikua za ki capitalist ambazo bob alikua haziungi mkono kwakua zilikua zina nyonya na kukandamiza wanyonge (babylonian system), sera hizi ziliungwa mkono na CIA kwakua ziliwapa fulsa mbalimbali.
Aidhaa bob alikua anaandaa matamasha ya bure jamaica na kufafanua madhara ya sera hizo za ki capitalist kwa njia ya nyimbo. Wajamaica walimpenda na kumuamini sana bob, jambo lililo wakwamisha sana JLP
BOB alinusulika kuuawa (ambush in the night) siku chache kabla ya tamasha lake la bure la smile jamaica lililokua na udhamini wa PNP, hii ilitafsiriwa na JLP kama kukipa kick chama cha PNP.