Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (DUCE) chasem CCM ndio chaguo lao kwa sasa

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,664
59,735
CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM (DUCE) CHASEMA CCM NDIO CHAGUO LAO KWA SASA.

Tarehe 23 desemba 2018 Ndg Said Said Nguya Afisa wa CCM Makao makuu ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Tawi la Chuo Kikuu Kishiriki Cha Dar es salaam (DUCE) uliyofanyika katika ukumbi wa Iddi Nyundo Wilayani Temeke kama Mgeni Mzungumzaji.

Katika mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Tawi Ndg Paul Kawawa umehudhuriwa na wanafunzi takribani 320, ambapo Ndg Said Said Nguya ametumia fursa hiyo kuwaeleza wanafunzi mambo makubwa ya maendeleo yanayofanywa na Serikali ya CCM inayoongozwa na Ndg John Pombe Joseph Magufuli, hivyo amewataka vijana nchi nzima wawe walinzi kwa yeyote anayetaka kumvunja moyo ama kumkatisha tamaa kiongozi wetu.

Wakati huo uo kumefanyika zoezi la ugawaji wa kadi kwa wanachma wapya wa CCM takribani 220, na kwa kauli moja wameahidi kuwa wanachama waaminifu kwa CCM siku zote.

Wamesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Rais wetu na Mwenyekiti wa CCM Ndg Magufuli hasa katika utoaji wa mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya juu, Ununuzi wa Ndege, Ujenzi wa Reli ya kisasa, ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa Stieglers gorge n.k ambapo yote haya yanalenga kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati.

Mkutano huo pia umehudhuriwa na mjumbe wa mkutano mkuu wa Taifa Mkoa wa Tanga Ndg Fredrick Chagoha, Mjumbe wa Halmashauri kuu Wilaya ya Mkuranga Ndg Bofu, na viongozi wengine ambao wote kwa wakati tofauti wamewaasa Wanafunzi mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Nidhamu, bidii ya kazi pamoja na kujitolea katika kufikia malengo.

Imetolea na Katibu Hamasa
TAWI LA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM ( DUCE).
IMG-20181224-WA0040.jpg
IMG-20181224-WA0039.jpg
IMG-20181224-WA0038.jpg
 
Tuseme ukweli tu, hivi upinzani kuna nini cha maana....fikirieni eti mtu kama Zitto ama Mbowe ndiyo awe kiongozi wa nchi hii, si ushenzi huu jamani? Ukweli ni kwamba hapa Tanzania hakuna kiongozi yeyote toka upinzani mwenye darubini ya maendeleo kama Magufuli. Walishindwa kina Mwinyi, Mkapa na Kikwete, waweze hawa wehu wapiga kelele wasiojitambua kweli?
 
Tuseme ukweli tu, hivi upinzani kuna nini cha maana....fikirieni eti mtu kama Zitto ama Mbowe ndiyo awe kiongozi wa nchi hii, si ushenzi huu jamani? Ukweli ni kwamba hapa Tanzania hakuna kiongozi yeyote toka upinzani mwenye darubini ya maendeleo kama Magufuli. Walishindwa kina Mwinyi, Mkapa na Kikwete, waweze hawa wehu wapiga kelele wasiojitambua kweli?
Wape heshima yao marais wastaafu.
 
Wape heshima yao marais wastaafu.


Marais wastaafu hawastahili heshima hata kidogo, wametuyumbisha sana as a nation. Kwa wenzetu wanauliwa ila hapa Tanzania wanalindana tu na ndiyo maana ninaichukia CCM ila upinzani inatuangusha kwani hakuna wa maana kule, ni uozo mtupu.
 
Hawa waalimu watarajiwa, tusiwaone mnakuja kulalamika maisha magumu wakati DUCE kimekuwa kama chuo cha ideology cha CCM.
 
CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM (DUCE) CHASEMA CCM NDIO CHAGUO LAO KWA SASA.

Tarehe 23 desemba 2018 Ndg Said Said Nguya Afisa wa CCM Makao makuu ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Tawi la Chuo Kikuu Kishiriki Cha Dar es salaam (DUCE) uliyofanyika katika ukumbi wa Iddi Nyundo Wilayani Temeke kama Mgeni Mzungumzaji.

Katika mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Tawi Ndg Paul Kawawa umehudhuriwa na wanafunzi takribani 320, ambapo Ndg Said Said Nguya ametumia fursa hiyo kuwaeleza wanafunzi mambo makubwa ya maendeleo yanayofanywa na Serikali ya CCM inayoongozwa na Ndg John Pombe Joseph Magufuli, hivyo amewataka vijana nchi nzima wawe walinzi kwa yeyote anayetaka kumvunja moyo ama kumkatisha tamaa kiongozi wetu.

Wakati huo uo kumefanyika zoezi la ugawaji wa kadi kwa wanachma wapya wa CCM takribani 220, na kwa kauli moja wameahidi kuwa wanachama waaminifu kwa CCM siku zote.

Wamesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Rais wetu na Mwenyekiti wa CCM Ndg Magufuli hasa katika utoaji wa mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya juu, Ununuzi wa Ndege, Ujenzi wa Reli ya kisasa, ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa Stieglers gorge n.k ambapo yote haya yanalenga kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati.

Mkutano huo pia umehudhuriwa na mjumbe wa mkutano mkuu wa Taifa Mkoa wa Tanga Ndg Fredrick Chagoha, Mjumbe wa Halmashauri kuu Wilaya ya Mkuranga Ndg Bofu, na viongozi wengine ambao wote kwa wakati tofauti wamewaasa Wanafunzi mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Nidhamu, bidii ya kazi pamoja na kujitolea katika kufikia malengo.

Imetolea na Katibu Hamasa
TAWI LA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM ( DUCE).
View attachment 976375View attachment 976376View attachment 976377
Walimu watarajiwa. Nikikosa kazi mnaanaa kulalia. Idiots
 
kutoka "serikali ya viwanda" hadi "serikali ya miradi mikubwa ya maendeleo". ikifika 2020 ndio mtajua kuwa hiyo miradi wala sio "mikubwa" ni poor planing and implementation tu!
 
Tuseme ukweli tu, hivi upinzani kuna nini cha maana....fikirieni eti mtu kama Zitto ama Mbowe ndiyo awe kiongozi wa nchi hii, si ushenzi huu jamani? Ukweli ni kwamba hapa Tanzania hakuna kiongozi yeyote toka upinzani mwenye darubini ya maendeleo kama Magufuli. Walishindwa kina Mwinyi, Mkapa na Kikwete, waweze hawa wehu wapiga kelele wasiojitambua kweli?
Wakati Nyerere anazunguka kutafuta uhuru alifanana je? Je, hakuwa hoe hahe kama wengine na kulipiwa nauli? Magufuli pesa anayoitumia ameitengeneza kwa mikono yake? Je vitu vilivyofanyika si vilibuniwa na kutafutiwa mikopo na waliomtangulia?
 
CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM (DUCE) CHASEMA CCM NDIO CHAGUO LAO KWA SASA.

Tarehe 23 desemba 2018 Ndg Said Said Nguya Afisa wa CCM Makao makuu ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Tawi la Chuo Kikuu Kishiriki Cha Dar es salaam (DUCE) uliyofanyika katika ukumbi wa Iddi Nyundo Wilayani Temeke kama Mgeni Mzungumzaji.

Katika mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Tawi Ndg Paul Kawawa umehudhuriwa na wanafunzi takribani 320, ambapo Ndg Said Said Nguya ametumia fursa hiyo kuwaeleza wanafunzi mambo makubwa ya maendeleo yanayofanywa na Serikali ya CCM inayoongozwa na Ndg John Pombe Joseph Magufuli, hivyo amewataka vijana nchi nzima wawe walinzi kwa yeyote anayetaka kumvunja moyo ama kumkatisha tamaa kiongozi wetu.

Wakati huo uo kumefanyika zoezi la ugawaji wa kadi kwa wanachma wapya wa CCM takribani 220, na kwa kauli moja wameahidi kuwa wanachama waaminifu kwa CCM siku zote.

Wamesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Rais wetu na Mwenyekiti wa CCM Ndg Magufuli hasa katika utoaji wa mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya juu, Ununuzi wa Ndege, Ujenzi wa Reli ya kisasa, ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa Stieglers gorge n.k ambapo yote haya yanalenga kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati.

Mkutano huo pia umehudhuriwa na mjumbe wa mkutano mkuu wa Taifa Mkoa wa Tanga Ndg Fredrick Chagoha, Mjumbe wa Halmashauri kuu Wilaya ya Mkuranga Ndg Bofu, na viongozi wengine ambao wote kwa wakati tofauti wamewaasa Wanafunzi mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Nidhamu, bidii ya kazi pamoja na kujitolea katika kufikia malengo.

Imetolea na Katibu Hamasa
TAWI LA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA DAR ES SALAAM ( DUCE).
View attachment 976375View attachment 976376View attachment 976377
kadi za chama hazigawiwi
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhido ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.
 
Hapo utasikia labda fununu na ahadi no priority ya kupewa kazi baada ya kumaliza masomo
 
Vijana wa Ccm mnawaza kwa kutumia vijambioo ajira ziko wapi mkishamaliza chuo
 
Una u
Marais wastaafu hawastahili heshima hata kidogo, wametuyumbisha sana as a nation. Kwa wenzetu wanauliwa ila hapa Tanzania wanalindana tu na ndiyo maana ninaichukia CCM ila upinzani inatuangusha kwani hakuna wa maana kule, ni uozo mtupu.
Una umri gani? Unaonekana kinda usiyetaka kujua na umelishwa sumu!

Mimi siipendi CCM lakini huwezi linganisha mtu wako na mtangulizi yeyote, Mkapa alikuwa charismatic, Hata JK lakini si huyu.

Hebu tuambie kitu gani kipya chake amefanya? Anasoma wenzie walitaka kufanya nini anakopa na kufanya. Unajua mkapa ndie alianziaha TRA? Na SUMATRA nk? Huyu kaanzisha TRURA! Are they performing?
 
Back
Top Bottom