Ndugu wadau, nimesoma kwenye magazeti kuwa kuna mchezo mchafu unaendelea Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) - wanafunzi wanabadilirishiwa matokeo yao. Nimeshangaa sana! Hali kama hii inaondoa imani na baadaye hakuna atakayekuwa na imani na matokeo ya wanafunzi kwa vile itakuwa vigumu sana kujua kama ni ya kweli au yamebadilishwa.
Itaweza kusababisha wanachuo wanaohitimu OUT, wakitaka kujiunga na vyuo vingine itabidi wafanye mitihani tena ili kubaini kama wana sifa zinazostahili au la. Hii siyo hatari?
Itaweza kusababisha wanachuo wanaohitimu OUT, wakitaka kujiunga na vyuo vingine itabidi wafanye mitihani tena ili kubaini kama wana sifa zinazostahili au la. Hii siyo hatari?