Chuo gani kizuri kwa kusomea ualimu

Chuo gani kizuri kwa kusomea ualimu

Kuna watu bado wanasomea uticha hapa tz....pole sn mwanazengo
Wewe ni chizi Kama mpwayungu ..kwa hiyo unadhani wote wana ndoto Kama zako? Kuna watu ni makamishna kwenye mawizara na Wana BA au Bsc with education
Mwaka nilomaliza advance Kuna mwamba alipata grade ndoto ya wengi Tena PCM akapiga Bsc. With education sa iv ni senior lecturer
 
Nashauri kabla hajachukua maamuzi ya kwenda kusomea ualimu.. Mpwayungu village atoe maoni yake kwanza.😄😄
Wakurugenzi,ma DEO, Katibu mkuu Elimu watakuwa wachoma mkaa?
Mnaangalia upande mmoja tu.
Vyuo havihitaji walimu ni sekondari tu?
Msikatishe vijana tamaa.
Halafu sio ukisoma ualimu lazima uwe nwalimu unaweza ingia hata jeshi polisi kote wanataka wataalamu.
Narrow minded people, mnalipoteza sana hili taifa.
 
Labda nikueleze kitu

Shule nyingi waliosomea ualimu na walimu Tanzania hawajui kugeuza ualimu wao kuwa biashara

Mfano mzuri ni Uganda. Uganda walimu wazuri wa masomo tofauti huungana pamoja na kufungua shule ya Private

Wao wenyewe wanakuwa wamiliki na walimu.Uganda shule nyingi za private zinamilikiwa na walimu sio watu wa mitaani

Mfumo huo Hapa kwetu unakuta shule inamilikiwa na darasa la saba kaajiri walimu

Sisi elimu ya kujiajiri hata hatujui maana yake.Mfano wahindi na waarabu kama ana biashara inategemea kama ni ya usafirishaji anapeleka watoto kwenda kusoma digrii kama za Transport management, Business administration, Mechanical Engineering nk related subjects.

Kama ana hospital anapeleka watoto kusoma course related na hospital kama medicine,pharmacy nk

Kama mkulima anapeka watoto.kusoma digrii za kilimo nk

Sisi ndio maana biashara za kiswahili hufa mwenyewe akifa.Mtu ana malori na mabadi anampeleka mtoto kusomea udaktari kisa ohh akimaliza apate ajira serikalini anasahau ana biashara yake inahitaji mtu wa ku take over

Ona kampuni kama ASAS mzee alikufa siku nyingi kampuni inakwenda vizuri watoto wame take over

Azam pia mzee wa watu darasa la pili aliishia ila watoto kawapigisha shule hasa za biadhara Azam inapaa

Mo Dewji baba yake alimsomesha mno mambo ya biashara ona kampuni inavyoenda

Matajiri waswahili hawajui hilo
Wanawaza cheap labor tu badala ya kuingiza kwenye kampuni mtoto wako mwenyewe aliyesoma vitu vipya aendeshe hiyo kampuni kisasa na aweza jituma mno sababu ni mmojawapo wa wamiliki wa kampuni

Waswahili hawatoi hisa kwa watoto
Mkuu uko vizuri sana, nimeokota mengi mazuri sana uliyoandika hapa. Ww ni mtambo, wewe ni mashine haswa...
 
Back
Top Bottom