Chunga sana rafiki yako akipata nafasi atatembea na shemeji yake

Chris wood

JF-Expert Member
Dec 21, 2020
1,667
5,008
Usishangae sana sii kwa ubaya huyo huyo best friend wako wa damu damu, ambae muda mwingi unapoteza nae, huyo huyo ambae shida zako nyingi anakusaidia kutatua kwa moyo wake wote.

Huyo huyo ambae ukibahatika kupata pisi kali au danga unakuwa wa kwanza kumpelekea umbea .Huyo huyo ambae ambae mkienda kula bata mnakaa meza moja unaondoka unaenda toilet unamuacha akulindie mzigo.

Moyo wa mtu unasiri asee hivi ulishawahi fikiria ile moment umeenda kumtambulisha mpenzi wako kwa rafiki yako that time wanasalimiana kwa kushikana mikono kwa mara ya kwanza huwa unahisi nini kinatokea kichwani mwao.??

Ebu tuwe wakweli hujawahi kwenda tambulishwa kwa mpenzi wa rafiki yako, ukajikuta umekufa umeoza kwa huyo shemeji yako...?? Ukiona rafiki yako kipenzi anakuuliza uliza hivi unampango gani na huyo jamaa/demu wako shituka mapema pengine anataka kupima kina cha maji.

Na kama ikitokea wamependana asee hakuna mchezo unaochezwa kwa siri kubwa kama huo ili kulinda urafikina fedhea ,yaani hata FBI na interpol wakija kupeleleza hawawezi pata ushahidi ,zaidi hata ya kuiba mkee wa mtu ,yaani error kutokea ni 0.0001perc

Ukiona wa dada ni marafiki saana wa muda mrefu ujue kunapossibility kubwa wameshagongwa na jamaa mmoja kwa nyakati tofauti na mmoja wao alimuiba kwa siri mpenzi wa rafiki yake. Hivyo hivyo kwa boys marafiki wawili kuchezea tundu moja sio jambo la kushangaza na hapo mmoja wao ni anamuibia mwezie.

Ushauri kama una mpenzi wako una ndoto za kufika nae mbali ukiwa unapiga story zake kwa marafiki zako usimu underrate ukasemaa aah yule napiga tu siku ziendee, au yule namchuna zikiisha nasepa aloo itakuja kula kwako utapigwa tukio huto amini.

Najua kuna wengi hawato amini sababu ya usiri mkubwa wa hilo jambo ila amini kwamba ndugu.
 
Demu wangu alifanya mistake kubwa sana. Alitumia simu ya rafiki yake kunipigia sababu yakwake ilikua imezima charge.

Nimeona status ya Rafik yake WhatsApp. Maana yake amesave namba yangu.

Namtafuna muda si mrefu, kabla hawajamaliza chuo July.
 
Asante kwa ushauri wako kwaiyo tufanye nini sasa

Umenena ukweli mkuu kuna boya mmoja nlimwona mwamba Kumbe fyatu kuna siku nimepiga tukio aka peleka umbea kwa wife bila kujua anacheza na black belt wa kufyeka hawa viumbe, hakuleta maana yoyote wife alinielewa ila nkammegea pisi yake kwa huo huo unafki alioleta kwangu nkaenda lia kwa mkewe kua Mbna mwamba anamwambia mambo ya uongo mke wangu anamtaka au kwenye kuelezana nkafyeka shemeji japo kwambinde ila baadae alileta ushirikiano nkajilia.
 
Usishangae sana sii kwa ubaya huyo huyo best friend wako wa damu damu, ambae muda mwingi unapoteza nae, huyo huyo ambae shida zako nyingi anakusaidia kutatua kwa moyo wake wote.

Huyo huyo ambae ukibahatika kupata pisi kali au danga unakuwa wa kwanza kumpelekea umbea .Huyo huyo....
Pole sana mkuu kwa yaliyokukuta ndo dunia ilivyo.
 
Huyu nilimuona kawa ndugu kwani tumekua mtaa mmoja, shule moja, tuition moja, darasa moja na mkondo mmoja ingawa darasani tulitofautiana madawati. Katika makuzi yetu ilifikia hatua hata mama zetu wakawa wanafahamiana, tukaachana tulipoingia sekondari.

Muda ukapita, bado tukiwa marafiki haswaa, tukishirikiana katika mambo mbali mbali. Madem zangu asilimia kubwa alikuwa anawajua either kwa stori au kwa kuwaona. Nasikitika kusema kuwa ni miaka 9 sasa imepita, ule urafiki, uthamani na undugu uliokuwa kati yetu haupo na wala hautakuja kuwepo kwa maisha yangu yaliyobaki duniani.

Kuna demu nilimpata nikawa nadate nae, ikafikia hatua nikamtambulisha kwa jamaa sababu alitaka kumsalimia siku moja sababu nilimwambia siku moja jamaa ni mgonjwa, wakasalimiana na mengine yakaendelea. Yule bibie penzi lilikufa, jamaa urafiki ukafa, sijuagi mpaka leo kama wanaendelea au waliachana ila huwa namuomba Mola tu awabariki.

2013 nilipitia kipindi kigumu na kizito sana. Hakuna siku nitakuja kusahau kipindi hiko.
 
Sema ivyoliwa na rafiki wa mpenzi wako.. Tupe story
Tulivyowa chuo kuna mkaka nilikuwa namzimikia, nikawa namwambia rafiki yangu nampenda yule Kaka so akawa anafahamu Hilo.

Na huyo mkaka alikuwa ananipenda sema hakuwahi nitamkia kwasababu tayari nilikuwa na mtu wangu. Ila tukienda club lazima anifate tucheze wote,dalili nyingi zilionyesha ananizimikia kiaina.

Basi baada ya muda nikaskia anatoka na rafiki yangu dah iliniuma lkn sikuwa na jinsi maana tayari nina mtu wangu anaye tambulika. Maisha yakaendelea.

Tulivyoenda likizo nikawa nachat na huyo mkaka shemeji yangu kipindi hiko Simu za mkonini ndo zimeingia, nilikuwa na simu yangu Siemens C25 (wahenga wenzangu watanielewa).

Halafu kutuma msg ilikuwa free huitaji salio Wala bando so kuchat 24/7.

Tumechat weee tukaanza kuflirt kiaina nikamwambia hapa home Kuna mizinga ya konyagi mingi na hakuna wanywaji so nitakuletea zawadi.

Tulivyo fungua chuo nikabeba zawadi. Bahati nzuri sie third year tuliwahi kufungua chuo sikumbuki sababu ni nini, rafiki yangu alirudia mwaka so alikuwa mwaka wa pili.

Nikampelekea shemeji zawadi room kwake...my friend kilichotokea sisemi sana ila tulikulana balaa na tukaendelea miaka na miaka.
Rafiki yangu alikuja kusikia baadae sana nimeshamaliza chuo akaniuliza nikaruka mita 200 akaniamini.

Huyo rafiki yangu ni best yangu hadi Leo tumekuwa watu wazima na huyo mkaka hata nikimtafuta leo tutakulana tu ni vile sina tena mzuka wa hayo mambo.

Siku nyingine nitakusimulia jinsi alivyoendelea kuwa mchepuko wangu hata baada ya kuolewa..akaonekana na Mr (ambae ndo yule wa chuo aliyekuwa anatambulika) ananishusha kwenye gari yake. Gari ikabondwabondwa na yeye kutolewa mangeu na kufikia kufikishana polisi. Na pesa ya hospitali nikatoa na bado tuliendelea hatukuachana 😀😀. Kiufupi ni bonge ya mshkaji .
 
Demu wangu alifanya mistake kubwa sana. Alitumia simu ya rafiki yake kunipigia sababu yakwake ilikua imezima charge.

Nimeona status ya Rafik yake WhatsApp. Maana yake amesave namba yangu.

Namtafuna muda si mrefu, kabla hawajamaliza chuo July.
Pengine demu wako alisave namba yako kwa rafiki yake ili kuangalia kama hua unammute kwenye dp na status
 
Tulivyowa chuo kuna mkaka nilikuwa namzimikia, nikawa namwambia rafiki yangu nampenda yule Kaka so akawa anafahamu Hilo.
Na huyo mkaka alikuwa ananipenda sema hakuwahi nitamkia kwasababu tayari nilikuwa na mtu wangu. Ila tukienda club lazima anifate tucheze wote,dalili nyingi zilionyesha ananizimikia kiaina.
Basi baada ya muda nikaskia anatoka na rafiki yangu dah iliniuma lkn sikuwa na jinsi maana tayari nina mtu wangu anaye tambulika. Maisha yakaendelea.
Tulivyoenda likizo nikawa nachat na huyo mkaka shemeji yangu kipindi hiko Simu za mkonini ndo zimeingia, nilikuwa na simu yangu Siemens C25 (wahenga wenzangu watanielewa).
Halafu kutuma msg ilikuwa free huitaji salio Wala bando so kuchat 24/7.

Tumechat weee tukaanza kuflirt kiaina nikamwambia hapa home Kuna mizinga ya konyagi mingi na hakuna wanywaji so nitakuletea zawadi.
Tulivyo fungua chuo nikabeba zawadi. Bahati nzuri sie third year tuliwahi kufungua chuo sikumbuki sababu ni nini, rafiki yangu alirudia mwaka so alikuwa mwaka wa pili.
Nikampelekea shemeji zawadi room kwake...my friend kilichotokea sisemi sana ila tulikulana balaa na tukaendelea miaka na miaka.
Rafiki yangu alikuja kusikia baadae sana nimeshamaliza chuo akaniuliza nikaruka mita 200 akaniamini.

Huyo rafiki yangu ni best yangu hadi Leo tumekuwa watu wazima na huyo mkaka hata nikimtafuta leo tutakulana tu ni vile sina tena mzuka wa hayo mambo.

Siku nyingine nitakusimulia jinsi alivyoendelea kuwa mchepuko wangu hata baada ya kuolewa..akaonekana na Mr (ambae ndo yule wa chuo aliyekuwa anatambulika) ananishusha kwenye gari yake. Gari ikabondwabondwa na yeye kutolewa mangeu na kufikia kufikishana polisi. Na pesa ya hospitali nikatoa na bado tuliendelea hatukuachana 😀😀. Kiufupi ni bonge ya mshkaji .
Cha mtu huliwa na mtu, chuma huliwa na kutu.
 
Back
Top Bottom