Chuki na husda dhidi ya wanaDiaspora

Chuki na husda dhidi ya wanaDiaspora

Mimi nawatetea walo nje japo sina tatizo hilo. Wabongo tulio nyumbani hatuna sababu ya kuzuia uraia pacha kwa walio nje zaidi ya wivu tu. swala ni haki ya kuendelea kuwa watanzania baada ya kuchukua uraia wa nje. Uraia pacha utawa-protect kisheria kama wana kijisha au kibanda chake wasije wakatapeliwa na mnao jifanya mnatengeneza pesa ndefu kumbe mnafanya ufisadi. Watu bongo malizao wakati ni raia halali . Je itakuwaje kama mafisadi wakijua wewe sio rai kisheria. Watu wameondoka bongo kwenda kutafua elimu nje baada ya kukosa nafasi bongo mnataka wapoteze haki ya kuwa rai wa bongo. Wakati kilasiku munawauzia passport waindi, wakenya na wanaigeria. Pumba** zenu
Utazuia vipi? maana kinachotakiwa ni kuukana tu uraia wa nje, jambo ambalo mgeni anaweza kufanya lakini siku akirudi kwao anaomba tu passport.
Kumbuka wakati wa Nyerere wahindi walokimbilia UK na Canada walikuwa na uraia pacha na wakafanyiwa mipango ya usafiri na tukalaaniwa sisi, japo hao hao waliukana wa nje walipopata uraia wa Tanzania. wao watatushinda tu kwa kila hila, hizi chuki ni kwa wazawa tu hazitazami nje ya sanduku.

Hivyo hivyo leo Mkenya akija kwetu anaweza kuukana Uraia wa Kenya, mkampa passport kesho akapanda ndege kurudi kenya na kuchukua tena ganda la Kenya. Huyu mtu utamzuia vipi wakati passport yake inaonysha wiki moja tu kapata uraia wa Tanzania! na utajuaje?
 
Le Mutuz, sasa wewe ulikaa huko kwa miaka nenda rudi halafu hutaki kuelewa faida za dual citizenship sasa sijui tutegemee nini kwa akina Komba na Majimarefu!! The whole thing faida zake ni nyingi kuliko hasara (kama zipo) ila TZ kila siku lazima tuwe wa mwisho kwenye kila jambo!! Sioni sababu za hii kitu kusukumiziwa Membe as if is the only person anayeweza kujenga hoja au kuona faida zake. Unless tunat9aka kusema Membe yuko more exposed kwa vile amekaa nje sana kuliko hawa viongozi wengine??
wengine hawakuondoka kwa kupenda, ndo shida ilipo.
 
Nimeoma point yako mkuu. Ni Watanzania ndio wanapata hasara wasipo ruhusu dual citizenship. Kwa hiyo ni naona kama tz wanakataa mzawa kuwa na urai pacha basi wazuie mgeni yeyote ambae kwao kuna uraia pacha asipate uraia tz which is not possible.

Hii sheria ya kinyanyembe ni ya kijuha kupitiliza, huwezi sema unalinda masilahi ya nchi kwa kumuadhibu nduguyo mtanzania eti ukiogopa usalama wa nchi, wakati huo huo unawapa dual uraia wananchi wa nchi zingine. Katika sheria za kijuha hii imepitiliza viwango vyote vya ujuha.

Kwa sababu hii sheria haimuzuii mkenya kuwa na citizenship (passport) ya Tanzania na pia kuwa na citizenship (passport) ya Kenya. Ila inamzuia mtanzania tu mzawa kumiliki passport ya Tanzania na Kenya. Sheria hii mangumashi sana sipati picha wanaojinadi nayo wanalinda masilahi yepi? Upuuzi kweli unapoona sheria ya namna hii eti wanaipigia vipeuo inabidi kuanza kuhoji uwezo wa uelewa na sio anachopinga.
 
Mimi nawatetea walo nje japo sina tatizo hilo. Wabongo tulio nyumbani hatuna sababu ya kuzuia uraia pacha kwa walio nje zaidi ya wivu tu. swala ni haki ya kuendelea kuwa watanzania baada ya kuchukua uraia wa nje. Uraia pacha utawa-protect kisheria kama wana kijisha au kibanda chake wasije wakatapeliwa na mnao jifanya mnatengeneza pesa ndefu kumbe mnafanya ufisadi. Watu bongo malizao wakati ni raia halali . Je itakuwaje kama mafisadi wakijua wewe sio rai kisheria. Watu wameondoka bongo kwenda kutafua elimu nje baada ya kukosa nafasi bongo mnataka wapoteze haki ya kuwa rai wa bongo. Wakati kilasiku munawauzia passport waindi, wakenya na wanaigeria. Pumba** zenu
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!
 
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!

Unawekeza kwenye masharti ahueni. Kwanini mtu aje kuwekeza bongo ambapo atakuwa na masharti magumu kuliko hata ya mzungu anayewekeza bongo? kwa nini asiwekeze hukohuko aliko?

Maana wazungu wakija kuwekeza bongo wanapewa holiday tax hata miaka 10, ikiisha miaka 10anabadirisha jina la kampuni anapewa tena mingine 10.
Akija mbongo hata hiyo holiday hapewi na on top, ndo anakuwa foreigner wa ukweli kweli, unapigwa tax from day one harafu sio ya uzawa. Kwi kwi kwi kwi kwanini aje kuwekeza??

Akija Mzungu tena bila pesa sababu ya ngozi yake anapewa hadi na mtaji kutoka bank za kibongo. Juzi juzi hapa mlikuwa mmeshapitisha kuwapa Wakenya Kenya airways fedha za bure kupitia Precious Air, naona mlisituka dakika ya mwisho. Najua mjanja hapo atakuwa Bernard Membe ndo aliwasitua dakika ya mwisho.
 
_42481604_africa_migration416x363.gif


Hivi chuki dhuidi ya wana diaspora na hasa toka kwa wanasiasa na watu wenye hali nzuri za kimaisha hapa nyumbani inatokana na nini?

Cha ajabu ni kuwa mawaziri na viongozi kadhaa wa serikali ya nchi hii watoto wao wana uraia wa nchi mbili mbili japo sheria hiyo haipo. Mfano Waziri wa mambo ya nchi za nje ambaye diaspora iko chini yake, Bw Bernard Membe, watoto wake ni raia wa Canada, Sisemi kuwa kuwa na uraia wa nje ni dhambi lakini ungetegemea kuwa alikuwa na uwezo wa kuwaandikisha wanae kuwa ni raia wa Tanzania lakini alikubali waandikishwe kuwa ni raiua wa Canada. Cha ajabu ni kuwa Mheshimiwa Membe amekjuwa kimya sana huku watanzania ambao wako Diaspora wakiendelea kusulubiwa na wanasiasa na vyombo vya habari hii inanipelekea kulizia kuwa hivi chuki na husda dhidi ya wana Disapora (ambao wengi wao ni watoto wa maskini) inatokana na nini hasa?

Hivi vyama vya siasa vina maoni gani kuhusu hili suala?



wao wanataka watoto wao tu ndio wawe na uraia wa nchi mbili si wewe wala mimi.
 
Kama ni hivyo basi watakuwa wamekosea sana kwa sababu uraia pacha utakuja kuwasaidia sana Wazanzibari huko mbeleni (baada ya uzinduzi wa Tanganyika) hasa hasa katika suala la umiliki wa ardhi.

Acha speculation tena kwenye suala la ardhi bora tushare na wabara walioko majuu lakini tukijitenga nanyi lazima sheria yetu kwa masuala ya ardhi iwape fursa “wazawa” na sio aina nyingine yeyote ya raia labda awe mwekezaji.
 
Unawekeza kwenye masharti ahueni. Kwanini mtu aje kuwekeza bongo ambapo atakuwa na masharti magumu kuliko hata ya mzungu anayewekeza bongo? kwa nini asiwekeze hukohuko aliko?

Maana wazungu wakija kuwekeza bongo wanapewa holiday tax hata miaka 10, ikiisha miaka 10anabadirisha jina la kampuni anapewa tena mingine 10.
Akija mbongo hata hiyo holiday hapewi na on top, ndo anakuwa foreigner wa ukweli kweli, unapigwa tax from day one harafu sio ya uzawa. Kwi kwi kwi kwi kwanini aje kuwekeza??

Akija Mzungu tena bila pesa sababu ya ngozi yake anapewa hadi na mtaji kutoka bank za kibongo. Juzi juzi hapa mlikuwa mmeshapitisha kuwapa Wakenya Kenya airways fedha za bure kupitia Precious Air, naona mlisituka dakika ya mwisho. Najua mjanja hapo atakuwa Bernard Membe ndo aliwasitua dakika ya mwisho.

Mkuu ni vizuri kujitafutia kwanza usahihi wa kitu halafu ndio uongee, kupotosha si jambo jema.
 
Unawekeza kwenye masharti ahueni. Kwanini mtu aje kuwekeza bongo ambapo atakuwa na masharti magumu kuliko hata ya mzungu anayewekeza bongo? kwa nini asiwekeze hukohuko aliko?

Maana wazungu wakija kuwekeza bongo wanapewa holiday tax hata miaka 10, ikiisha miaka 10anabadirisha jina la kampuni anapewa tena mingine 10.
Akija mbongo hata hiyo holiday hapewi na on top, ndo anakuwa foreigner wa ukweli kweli, unapigwa tax from day one harafu sio ya uzawa. Kwi kwi kwi kwi kwanini aje kuwekeza??

Akija Mzungu tena bila pesa sababu ya ngozi yake anapewa hadi na mtaji kutoka bank za kibongo. Juzi juzi hapa mlikuwa mmeshapitisha kuwapa Wakenya Kenya airways fedha za bure kupitia Precious Air, naona mlisituka dakika ya mwisho. Najua mjanja hapo atakuwa Bernard Membe ndo aliwasitua dakika ya mwisho.
Inaelekea wewe ni mgeni katika nchi yako.
Nenda TIC(Tanzania Investment Centre) na uone waTanzania wenzako wanavyofaidika na hizo Tax Exemptions katika miradi yao.

Tatizo kubwa la Watanzania, kama MkamaP ni ujinga wa kutothubutu na kubaki kulalama tu!!
 
Last edited by a moderator:
Inaelekea wewe ni mgeni katika nchi yako.
Nenda TIC(Tanzania Investment Centre) na uone waTanzania wenzako wanavyofaidika na hizo Tax Exemptions katika miradi yao.

Tatizo kubwa la Watanzania, kama MkamaP ni ujinga wa kutothubutu na kubaki kulalama tu!!

Naomba ujishirikishe zaidi, ninaposema waTanzania ktk context hii naongelea wale waTanzania waliohujumiwa uzawa wao na sheria ya kinyanyembe ndo wanasota. Na ndio maana wanapigania haki yao ya msingi ili wakienda TIC wawe kama waTanzania wengine wanavyofaidika. Kituo kikubwa.

Sihitaji league ya Simba na Yanga ktk hili. Kituo. Na hivyo nashauri tuwe tuna digest context kabla yakuanzisha league isiyo natija.
 
Naomba ujishirikishe zaidi, ninaposema waTanzania ktk context hii naongelea wale waTanzania waliohujumiwa uzawa wao na sheria ya kinyanyembe ndo wanasota. Na ndio maana wanapigania haki yao ya msingi ili wakienda TIC wawe kama waTanzania wengine wanavyofaidika. Kituo kikubwa.

Sihitaji league ya Simba na Yanga ktk hili. Kituo. Na hivyo nashauri tuwe tuna digest context kabla yakuanzisha league isiyo natija.
Huwezi kujilipua na bado ukafaidi matunda yake!
In life you cannot eat your cake, and yet have it.
 
Mkuu ni vizuri kujitafutia kwanza usahihi wa kitu halafu ndio uongee, kupotosha si jambo jema.

Pamoja natoka nje ya maada kidogo, lakini nashauri muwe mnaji update hado hado.


[h=1]Fastjet resists Precision's $32m bailout[/h]



fastjet+px.jpg

Fastjet has termed the move as unfair, saying if the bailout is granted, it would adversely affect competition in the aviation industry in Tanzania.PHOTO|FILE
By Samuel Kamndaya,The Citizen Business Editor

Posted Thursday, December 19 2013 at 00:00

IN SUMMARY
But it is not clear why Fastjet sees the move as unfair while when the low-cost airline announced its lowest fare of $20 per one-way ticket, neither Precision Air nor Air Tanzania complained about the move.


Dar es Salaam.The battle to control Tanzania's skies has taken a new twist after Fastjet, a low-cost airline which entered the market with a bang, strongly opposed Precision Air's(PW) decision to seek a bailout amounting to $32 million (Sh51.2 billion) from the government.

Fastjet has termed the move as unfair, saying if the bailout is granted, it would adversely affect competition in the aviation industry in Tanzania.

But it is not clear why Fastjet sees the move as unfair while when the low-cost airline announced its lowest fare of $20 per one-way ticket, neither Precision Air nor Air Tanzania complained about the move.

In what points to a looming business war between the two airlines, Fastjet chief commercial officer Richard Bodin says that bailing out PW using taxpayers' money would create an unfair playing field among operators who are competing in the market. He says if Precision Air is bailed out, similar assistance should be extended to both Air Tanzania and Fastjet if the government wants to a create competitive and fair aviation industry.


http://www.thecitizen.co.tz/News/Fastjet-resists-Precision-s--32m-bailout/-/1840392/2117626/-/12by9ykz/-/index.html
 
Absolutely!
Hell is ones choice, think before you leap into the abyss!

Thank you, think tank. But however, Would you please depict the pros and cons for having dual citizenship. Again, please do it by the help of vivid example and use cases. Otherwise , I would much appreciate if you could mind your std.
 
Ati nini???-dual citzenship??-hakika mteteaji ajiandae vya kutosha,maana ,,,,,,duh.
 
Ati nini???-dual citzenship??-hakika mteteaji ajiandae vya kutosha,maana ,,,,,,duh.


Mteteaji ana kazi rahisi sana. Atawauliza, kwanini wanakataa dual citizenship(dual passport), najua watajibu wanalinda masilahi ya Taifa. Naye atawaambia ngoja niwapeni mfano.

Kwa sheria hii iliyopo inamruhusu Mkenya kupewa citizenship(passport) ya Tanzania kwa kuikana citizenship(passport) ya Kenya. Na hivyo basi,
Mkenya anakuja Tanzania anaoa/kuolewa anaomba citizenship(passport) ya Tanzania anapewa na anaikana yake ya kenya. Kisha huyu mkenya anarudi kwao kwa kutumia passport ya Tanzania akifika kwao anaomba passport nyingine ya Kenya, na kwa vile Kenya wanaruhusu kumiliki passport mbili, ile ya Tanzania wanamuachia na anakuwa na passport mbili (dual citizenship). Kisha anarudi Tanzania, na kwa vile nia ya mkenya ilikuwa kumiliki ardhi ya Tanzania basi ananunua maheka na maheka ya ardhi ya Tanzania na anayamiliki. Hapo masilahi ya Taifa watakuwa wameyalinda vipi?

Na unaendelea kuwahoji, kwa vile sheria hii inamzuia Mtanzania kumiliki passport mbili na wakati huo huo inaruhusu Mkenya na mnyarwanda kumiliki kwa pamoja passport ya Tanzania na Kenya ama Rwanda, je hayo ndio masilahi ya Taifa mnayolinda ktk hii sheria ya kinyanyembe? Ama masilahi ya Taifa ni pale tu inapomzuia mtanzania mzawa kumiliki passport nyingine?

Hii sheria inamwamini sana Mkenya, Mnyarwanda, mzungu, mchina na nk na kumpa passport na kwamba hawa jamaa hata wakimiliki passport mbili (dual citizenship) yani passport ya Tanzania na nchi yake hawahatarishi masilahi ya Taifa la Tanzania, ila tu masilahi ya Tanzania yatahatarishwa na mTanzania kumiliki passport ya Tanzania na ya nchi nyingine?

Hii ni sheria ya kinyanyembe ni ya kijuha kupita viwango vyote vya kijuha.
 
Si kweli,
Nafikiri unajaribu kupotosha unaposema waTanzania wakirudishiwa nationality yao basi Wakenya by default wataomba uraia kwa sababu waTanzania by default wamerudishiwa nationality yao. Kwanza inabidi utambue tofauti ya nationality na citizenship ili kwayo upate kujenga hoja yako isiyo na mizizi.

Pili, umejenga hoja ama kwa kutoelewa ama kutotaka kujielimisha mwenyewe na kujipa update muafaka hasa unapoongelea wakenya ama wanyarwanda kupewa citiznship na kununua ardhi. Kwa sababu:

- Hakuna sheria hadi leo inayomkataza mkenya kuomba citizenship ya Tanzania, na kama ameoa hadi leo hii mkenya anaruhusiwa kuomba uraia wa Tanzania, ila tu eti anatakiwa ku u kana ukanya. Hivyo, Mkenya akiitaka ardhi hadi leo anaoa mtanzania anaomba citizeship ana ukana uraia wa kenya, ananunua ardhi ya kutosha kesho yake anarudi kenya anaomba passport ya kenya bila kuukana uTanzania maana sheria ya kenya hamutaki hivyo. Kisha anakuwa na passport zote za Tanzania na Kenya, vivyo hivyo kwa mnyarwanda, mrundi mganda nk.
Hivyo katika sakata hili looser siku zote ni mTanzania ktk nchi zote, maana wengine wanakuja wanaoa wanapewa uraia wa Tanzania eti mkijifanya wameukana uraia wao, kumbe wanarudi kwao na kupewa tena.

Ungekuwa na hoja tu kama hadi leo, Tanzania sheria yake ya kijima hii, ingekuwa inakataza kabisa hakuna nationality mwingine kupata citizenship ya Tanzania. Lakini, kwa vile Tanzania inaruhusu kupata citizenship kwa kukana tu citizenship ulikotoka, basi hoja zote za wapinga dual citizenship ni WIVU, HUSDA, ama ualewa mdogo sana jinsi mambo yanavyofanya kazi hapa duniani.

Wapinga dual mngekuwa na hoja tu, kama duniani kote nchi zote zingekuwa zinalazimisha kuukana citizenship yako kabla ya kupata mwingine. Lakini kwa sheria leo ya Tanzania ilivyo, na kama unaelewa japo kidogo sana utaona ya kwamba, hii sheria ikiendelea itamzuia mTanzania tu wa kuzaliwa kuwa na dual. Lakini haimuzuii mkenya ama mwingine kutoka nchi yoyote kuwa na dual yani mTanzania na wakati huo huo mKenya.

Naomba muangalie hili swala kwa kutumia akili na sio kutumia mazoea ya kijima.

Naona hujanielewa au labda ni mi sijakuelewa. Me sitaki kuongelea swala la nationality, my concern hapa ni citizenship. Na niseme tu naona unajikanganya, Unaposema mtu akitaka uraia wa Tanzania, na kama yeye ni mkenya itabidi aukane uraia wa Kenya. Ndio hasa ambacho si tunakitaka. We know these guys, bado hatujafikia hatua ya kuwa comfortable nao.

Na unaposema sheria ya inayopinga dual citizenship haimzuii mkenya kuwa na uraia wa Tanzania, me sielewi. Una maana kwamba mtu anaweza akaja Tanzania na kupata uraia bila kuukana uraia wa nchi yake. Kama ndio maana yako, basi nadhani unapaswa ku-revisit the facts.
 
Naona hujanielewa au labda ni mi sijakuelewa. Me sitaki kuongelea swala la nationality, my concern hapa ni citizenship. Na niseme tu naona unajikanganya, Unaposema mtu akitaka uraia wa Tanzania, na kama yeye ni mkenya itabidi aukane uraia wa Kenya. Ndio hasa ambacho si tunakitaka. We know these guys, bado hatujafikia hatua ya kuwa comfortable nao.

Na unaposema sheria ya inayopinga dual citizenship haimzuii mkenya kuwa na uraia wa Tanzania, me sielewi. Una maana kwamba mtu anaweza akaja Tanzania na kupata uraia bila kuukana uraia wa nchi yake. Kama ndio maana yako, basi nadhani unapaswa ku-revisit the facts.

Article 16 of the Kenyan Constitution states, “A citizen by birth does not lose citizenship by acquiring the citizenship of another country”.

Habari ndo hiyo. Na huo ni mfano tu. Kwa maelezo zaidi hebu nenda hapa:
https://www.jamiiforums.com/katiba-...-uraia-pacha-na-wenzetu-afrika-mashariki.html
 
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!

Really? Mbona majibu yanatolewa kila siku lakini hamtaki kufungua masikio? Nikupe mfano mmoja tu. Kuna dada Mtanzania ambaye anafanya kazi NASA. Huwezi kupata kazi sehemu kama NASA kama hauna uraia wa Marekani. Huyu dada, ndugu zake WOTE wako Tanzania, lakini ilibidi apate kazi anayopenda na inayoendana na kisomo chake. Sasa, kama mtu huyu ambaye ana PhD ya aerospace engineering, Bongo arudi afanye kazi wapi? Je, na watoto wake ambao ni Watanzania-Wamarekani, nao ni "wasaliti" kama ambavyo mnajaribu kuwasulubu "waliojilipua"?

Sidhani kama Watanzania ni wajanja sana kuliko Wanyarwanda, Wakenya, Waganda, Waghana, na mataifa mengine sana ya Afrika ambao wanaruhusu uraia pacha. Kama kuna practical experience ya madhara ya uraia pacha, ningependa kusikia mfano. Vinginevyo hoja zinazotoka upande wa kupinga uraia pacha kama mada hii inayosema, zinaonekana kujaa uoga, chuki tu na husda, badala ya nondo za nguvu.
 
Back
Top Bottom