Chuki na husda dhidi ya wanaDiaspora

Mkuu Ulukolokwitanga huku ni kukosea watu heshima sidhani kama unajua umuhimu wa Dual citizenship otherwise Leave stone as they are. Thanx.

Diaspora wa Tanzania mchango wao ni JF MMU pekee, kwenye uchumi na ujasiriamali hutowaona kamwe. Sana Sana wakichoka kuosha vyombo huko utawaona Chit Chat. Usitegemee remittance kutoka kwa mijitu ya aina hii...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Spina Hili lina uhusiana vipi na kinachojadiliwa hapa jamani tusipende kuleta utani katika mambo ya Msingi. Just for love and peace. Thanx.

Yanga kama CDM hakuna haki lazima kuandamana kushinikiza kupata haki. Haki ni pamoja na kupewa ridhaa au kukataliwa
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lenu hamuwaelewi Watanzania au labda mmesahau kuhusu Watanzania.


Tumeshapata matatizo mengi sana hasa hasa na mahusiano na wageni, kuanzia wahindi, wakenya, warundi n.k, sasa nyie mnapoanza kudai uraia wa nchi mbili bila maelezo mazuri watanzania lazima wawe na mashaka. And remember if it aint broke, dont fix it. What kind of an animal you call "Dual citizenship"?.


Mnakaa kuongelea "Tunakosa opportunities huku tulipo", how does that affect my daily life in Tanzania? Mnaongelea kuhusu "Mabilioni", do you know the challenges we are facing due to a large influx of foreigners in this country, we cant be blind to this fact just for the sake on "Billions" you are "eagerly waiting to start sending" back to Tanzania.


As far as I know (You can correct me if am wrong), when you have legislation that allow dual citizenship, it means, every other person from another country[barring some restrictions], that allows dual citizenship can apply to be a citizen of your country. Tuna wakenya wengi tu hapa Tanzania ambao wameoa dada zetu so that they can buy land in this country. Kesho tukiruhusu waweze kuomba uraia, na uki-take into consideration how corrupt the country's officials are, we unadhani tutakuwa salama? Tuna jirani hapa Rwanda, ukubwa wa nchi yake is less than half the size of lake Victoria but has a population of almost 12 mil. We unadhani kesho ukiruhusu kiurahisi tu hawa nao waweze kuomba uraia kutatosha hapa.


Inawezekana mna mambo ya maana mnayotaka kufanya hapa Tanzania, lakini dont ignore our concern. Mnataka kuintroduce kitu kipya kwenye maisha yetu, lazima mtushawishi and iron out all the doubts. Tumekaa bila Dual citizenship all this time bila shida yoyote, dont force us to fit in your new found shoes.


Show us the numbers, show us the benefits. Jipangeni kama alivyosema Le Mutuz, semeni how much you have done to the country mpaka sasa hivi. Mmefanya investement kiasi gani?

If it ain't broke, dont fix it
 

lusungo mtu akiwa na dhana kuwa unamchukia maelewano huwa nadra!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:

Mkuu sijui tena tueleze nini !!!!?????
Ila wao wanaona ni chuki, husda, wivu, kutojiamini na mambo kama hayo!!!!!
 
Kaeni huko huko.Kama mnataka kutuchangia fanyeni harambee kusanyeni hela mtuletee tujenge mambweni na visima huku huku.Hivi mchina akiomba uraia,mhndi naye,mmexico halafu wakigombea uongozi hapa mchina akawa rais,mmexico PM NA KANJIBAH SPIKA ITAKUAJE
 
Ha ha ha

Hebu wafikirie watanzania wenzio mkuu..

Nawafikiria sana tu mkuu ndio maana mijadala hii nakaa muda mrefu kujifunza na kuchangia na nina amini kabisa tutafika muafaka!!!!!!!

Ila tofauti ya context na life experience inatuyumbisha sana!!!!!!!
 

Si kweli,
Nafikiri unajaribu kupotosha unaposema waTanzania wakirudishiwa nationality yao basi Wakenya by default wataomba uraia kwa sababu waTanzania by default wamerudishiwa nationality yao. Kwanza inabidi utambue tofauti ya nationality na citizenship ili kwayo upate kujenga hoja yako isiyo na mizizi.

Pili, umejenga hoja ama kwa kutoelewa ama kutotaka kujielimisha mwenyewe na kujipa update muafaka hasa unapoongelea wakenya ama wanyarwanda kupewa citiznship na kununua ardhi. Kwa sababu:

- Hakuna sheria hadi leo inayomkataza mkenya kuomba citizenship ya Tanzania, na kama ameoa hadi leo hii mkenya anaruhusiwa kuomba uraia wa Tanzania, ila tu eti anatakiwa ku u kana ukanya. Hivyo, Mkenya akiitaka ardhi hadi leo anaoa mtanzania anaomba citizeship ana ukana uraia wa kenya, ananunua ardhi ya kutosha kesho yake anarudi kenya anaomba passport ya kenya bila kuukana uTanzania maana sheria ya kenya hamutaki hivyo. Kisha anakuwa na passport zote za Tanzania na Kenya, vivyo hivyo kwa mnyarwanda, mrundi mganda nk.
Hivyo katika sakata hili looser siku zote ni mTanzania ktk nchi zote, maana wengine wanakuja wanaoa wanapewa uraia wa Tanzania eti mkijifanya wameukana uraia wao, kumbe wanarudi kwao na kupewa tena.

Ungekuwa na hoja tu kama hadi leo, Tanzania sheria yake ya kijima hii, ingekuwa inakataza kabisa hakuna nationality mwingine kupata citizenship ya Tanzania. Lakini, kwa vile Tanzania inaruhusu kupata citizenship kwa kukana tu citizenship ulikotoka, basi hoja zote za wapinga dual citizenship ni WIVU, HUSDA, ama ualewa mdogo sana jinsi mambo yanavyofanya kazi hapa duniani.

Wapinga dual mngekuwa na hoja tu, kama duniani kote nchi zote zingekuwa zinalazimisha kuukana citizenship yako kabla ya kupata mwingine. Lakini kwa sheria leo ya Tanzania ilivyo, na kama unaelewa japo kidogo sana utaona ya kwamba, hii sheria ikiendelea itamzuia mTanzania tu wa kuzaliwa kuwa na dual. Lakini haimuzuii mkenya ama mwingine kutoka nchi yoyote kuwa na dual yani mTanzania na wakati huo huo mKenya.

Naomba muangalie hili swala kwa kutumia akili na sio kutumia mazoea ya kijima.
 

Le Mutuz, sasa wewe ulikaa huko kwa miaka nenda rudi halafu hutaki kuelewa faida za dual citizenship sasa sijui tutegemee nini kwa akina Komba na Majimarefu!! The whole thing faida zake ni nyingi kuliko hasara (kama zipo) ila TZ kila siku lazima tuwe wa mwisho kwenye kila jambo!! Sioni sababu za hii kitu kusukumiziwa Membe as if is the only person anayeweza kujenga hoja au kuona faida zake. Unless tunataka kusema Membe yuko more exposed kwa vile amekaa nje sana kuliko hawa viongozi wengine??
 

Duh...Unaua...!!
 

Jaman,
Nyie wenzetu mnaoishi nje inaonekana hamna uzalendo kabisa.
Na huu upuuzi wa kuomba kuwa na uraia wa nchi zaid ya Moja ni some sort ya Selfishness esepcially kwa Diaspora wa Ki Tanzania, Hebu tujiulize nyie mlioko huko Mpaka sasa mmesaidia nini hii nchi ? zaid ya kujificha Nyuma ya Keyboard zenu na kuishia kupiga Siasa tuuuu.
Mtu kama Chris Lukosi akiwa na Uraia either wa nchi moja ama mbili kutakuwa na tokea gani Chanya kwake na kwa Nchi yake Mama ?
 
Last edited by a moderator:
Watanzania wezangu mnaopinga dual
Naomba mtutumie akili na kuzishirikisha hizi akili. Hili si tusi, bali naomba mzishirikishe akili kwa tija yenu, yetu na kizazi chetu na kwa taifa kwa ujumla.
Kwasababu kupinga citizenship kwa Tanzania, hii inamnyima dual mzawa wa Tanzania tu na si mtu mwingine asiye mzawa. Hii inampa haki zaidi Mkenya kwa uzawa kuliko mTanzania kwa uzawa, kutokana na kwamba sheria hii tuliyonayo ya kijima bado inaruhusu kupewa mkenya uraia ama raia yeyote wa nje kuwa raia Tanzania kwa kuukana uraia wake wa awali. Nitakupa mfano kwanini hii sheria ni ya kinyanyembe kwa waTanzania wazawa tu.

Kwa sheria iliyopo
Mfano mie ni mkenya nakuja bongo naoa naomba citizenship(passport) napewa na Tanzania wanachukua passport yangu ya kenya. Poa, natumia passport ya Tanzania naingia kwetu Kenya, nikifika Kenya naomba passport nyingine ya Kenya na kwa sababu Kenya wanaruhusu kuwa na passport mbili hawaninyang'anyi ya Tanzania wananiachia. Narudi Tanzania nikiwa na passport mbili (Dual citizenship) na nunua ardhi ya Tanzania kubwaaaaaaa. Mmeona hapo???????

Hii sheria mnayotetea ya kijima na kinyanyembe , hailindi masilahi yoteyote ya Tanzania kwa njia zozote zile na kwa namna yoyote ile hata ya kubuni. Badala yake ina nyanyasa tu waTanzania wakuzaliwa na kupendelea wazawa wa nchi zingine, sijui sheria ya namna hii italinda vipi masilahi ya nchi???

Hii sheria ya kijima na kinyanyembe, wenda ilifanya kazi karne ile kwa sababu nchi nyingi wakati wa karne ile walikuwa hawaruhusu dual citizenship, hivyo ilikuwa ukichukua citizenship ya nchi husika na passport yako wanachukua na wanaituma nchi kwako hivyo ilikuwa kweli strictly unajulikana umekana uraia, lakini sasa sio hivyo. Kwa sababu mie mkenya niliechukua uraia wa Tanzania na kurudi kenya kuomba passport mpya Tanzania hawatajua kama nimeomba passport mpya ktk nchi yangu ya kuzaliwa, kwa sababu kenya haitaichukua passport yangu ya Tanzania na kuituma Tanzania ama kuwasiliana na Tanzania kabla ya kupewa passport nyingine ya Kenya.

Wanaotetea hii sheria ya kijima na kinyanyembe hawana hoja hata moja zaidi ya wivu wa kuwafunga watanzania wenzao wakati huohuo wakiwapa DUAL raia wa kigeni. Amkeni
 
Kwani wakiwa na uraia wa nchi mbili tunaathirika vipi?

Sijazungumzia swala la uraia pacha, nimezungumzia michango yao nchini pamoja na kutowasilisha hoja ya kuomba uraia pacha. Hata wao wakiwa na uraia wa nchi 4 hatuoni tija kwa taifa kama hawafanyi juhudi za kutuletea ujuzi waliopata pamoja na kutumia fursa ya kuwekeza. Sasa wao hoja yao kuu ni wivu na chuki, haya siyo mambo ya misingi ya kufanya katiba ikubaliane na uraia pacha.
 
Sijazungumzia swala la uraia pacha, nimezungumzia michango yao nchini pamoja na kutowasilisha hoja ya kuomba uraia pacha. Sasa wao hoja yao kuu ni wivu na chuki.

Hoja kama haijawasilishwa, imefika je kwenye rasimu ya katiba mpya? Hoja ipo tayari ama unataka hoja ipi kuwasilishwa?
 

kwani Le Mutuz ataweza kuloby pekeyake? Anahitaji team yenye kuonyesha commitment kwenye hili swala. Mbona wameweza kujiwakilisha vizuri kwenye vyama vya siasa vikubwa hapa nchini, wameshindwa nini kwenye hili? Wafanye hima kuwasilisha hoja zao za msingi katika mchakato huu wa upatikanaji wa KATIBA MPYA, nahisi halijachelewa na linajadilika with facts and figures.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…