Afrika Furaha
JF-Expert Member
- Dec 16, 2010
- 329
- 9
Sikukuu za Christmas na Boxing day zilizopangwa kufanyika kesho na keshokutwa duniani kote zimesogezwa mbele hadi hapo zitakapopangwa tena.
Msemaji wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Mbingu za Mitaa (TAMIMBIMI), Mtakatifu Yohana Mbatizaji alisema kuwa tarehe ya sherehe na sikukuu hizo maarufu zaidi duniani zitapangwa hapo baadae wakati Baraza la Umungu litakapokaa kujadili vurugu zilizotokea jana ktk kikao cha kuchagua ma-Mayor wa kanda za Watakatifu na Malaika, na hadhi ya Mwana wa Mungu Yesu, baina ya chama cha upinzani, Chama cha Yesu na Maria Mtakatifu (CHAYEMA) na chama tawala, Chama cha Malaika wa Mbinguni (CMM).
CHAYEMA wanataka Yesu apewe hadhi ya Nabii, wakati CMM wanataka aitwe Mtume.
Katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwezi huu, CHAYEMA walizoa karibu viti vyote vya ubunge na udiwani kanda ya Watakatifu, ambako wanaishi watu wengi wa kabila la Manabii, wakati CMM waliteka kanda ya Malaika, ambako wanaishi watu wengi kabila la Mitume.
Kanda ya Watakatifu ina jumla ya viti 15 vya ubunge na 32 vya udiwani, ambapo CHAYEMA wana viti 12 vya ubunge na 28 vya udiwani, CMM ina viti 3 vya ubunge na viti 4 vya udiwani.
Kanda ya Malaika ina viti 17 vya ubunge na 35 vya udiwani, ambapo CMM ina viti 15 vya ubunge na 29 vya udiwani, wakati CHAYEMA wana viti 2 vya ubunge na viti 6 vya udiwani.
CHAYEMA wana msimamo mkali ktk kutubu dhambi, wakati CMM wana msimamo wa hiyari, ambapo hutaka wakosaji watubu dhambi bila kushinikizwa wala kuchaguliwa dhambi za kutubu.
Nchi ya Mbinguni imekumbwa na vurugu za mara kwa mara tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu ambapo chama tawala kimepoteza viti vingi vya ubunge na udiwani, ambapo Jeshi la Usalama Mbinguni limelazimika kutumia silaha nzito na za kisasa kama Maandiko Matakatifu na Ibada ktk kutawanya wafuasi wa CHAYEMA kila wanapotaka kufanya mkutano wa hadhara.
Msemaji wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Mbingu za Mitaa (TAMIMBIMI), Mtakatifu Yohana Mbatizaji alisema kuwa tarehe ya sherehe na sikukuu hizo maarufu zaidi duniani zitapangwa hapo baadae wakati Baraza la Umungu litakapokaa kujadili vurugu zilizotokea jana ktk kikao cha kuchagua ma-Mayor wa kanda za Watakatifu na Malaika, na hadhi ya Mwana wa Mungu Yesu, baina ya chama cha upinzani, Chama cha Yesu na Maria Mtakatifu (CHAYEMA) na chama tawala, Chama cha Malaika wa Mbinguni (CMM).
CHAYEMA wanataka Yesu apewe hadhi ya Nabii, wakati CMM wanataka aitwe Mtume.
Katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwezi huu, CHAYEMA walizoa karibu viti vyote vya ubunge na udiwani kanda ya Watakatifu, ambako wanaishi watu wengi wa kabila la Manabii, wakati CMM waliteka kanda ya Malaika, ambako wanaishi watu wengi kabila la Mitume.
Kanda ya Watakatifu ina jumla ya viti 15 vya ubunge na 32 vya udiwani, ambapo CHAYEMA wana viti 12 vya ubunge na 28 vya udiwani, CMM ina viti 3 vya ubunge na viti 4 vya udiwani.
Kanda ya Malaika ina viti 17 vya ubunge na 35 vya udiwani, ambapo CMM ina viti 15 vya ubunge na 29 vya udiwani, wakati CHAYEMA wana viti 2 vya ubunge na viti 6 vya udiwani.
CHAYEMA wana msimamo mkali ktk kutubu dhambi, wakati CMM wana msimamo wa hiyari, ambapo hutaka wakosaji watubu dhambi bila kushinikizwa wala kuchaguliwa dhambi za kutubu.
Nchi ya Mbinguni imekumbwa na vurugu za mara kwa mara tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu ambapo chama tawala kimepoteza viti vingi vya ubunge na udiwani, ambapo Jeshi la Usalama Mbinguni limelazimika kutumia silaha nzito na za kisasa kama Maandiko Matakatifu na Ibada ktk kutawanya wafuasi wa CHAYEMA kila wanapotaka kufanya mkutano wa hadhara.