Chombezo: Tipwatipwa tetema, Oooh tetema

Chombezo: Tipwatipwa tetema, Oooh tetema

SEHEMU YA 18



ILIPOISHIA:
“Basi usijali, nakupikia chakula kizuuuri, ukishakula kuna kazi inakusubiri,” alinibusu kisha akainuka, akawa anatoka huku akijitingisha, nikabaki nikimsindikiza kwa macho huku moyoni nikijiambia ‘za mwizi arobaini’.
SASA ENDELEA...
Basi niliendelea kujilaza pale kitandani huku nikiendelea kutafakari mambo mengi ndani ya kichwa changu, ama kwa hakika michezo ya haramu huwa inakuwa mitamu sana.
Mambo yalikuwa yamebadilika kwa kasi kubwa sana, kutoka kuwa muuza samaki mpaka kuja kuwa baba mwenye nyumba msaidizi, sasa nikifuliwa nguo na kupikiwa misosi ya nguvu! Jambo ambalo sikuwa nalijua ni kwamba mwisho wa yote hayo utakuwa nini?
Kutokana na kukolezwa na mama mdogo, nilijikuta nikimsahau kabisa mwanamke ambaye alikuwa na mapenzi ya dhati kwangu, tena akiwa hana mtu kama mwenyewe alivyoniambia isipokuwa mimi tu, Mimah! Lakini pia nilijikuta nikipoteza kabisa taiming ya kumpata mwanamke mwingine ‘chibonge’ lakini mrembo kwelikweli, Jack.
Yaani mama mdogo ni kama alikuwa amenipa limbwata ambalo sasa lilinifanya nizidi kuyakumbatia matatizo kwa mikono yangu miwili. Hivi kama mumewe ambaye kwangu mimi ni baba mdogo angeshtukia mchezo huo si ingekuwa hatari sana? Sasa nitafanyaje kujitoa kwenye mikono yake wakati nimeshazama?
Basi muda mfupi baadaye, mamdogo alileta msosi wa nguvu, mapochopocho kibao, wale samaki ambao huwa tunawauza kwa bei ya juu, aina ya changu, basi aliandaliwa mzima kwa ajili yangu. Kwa wataalamu wa samaki watakuwa wanajua kiwango cha samaki changu na bei yake.
Baada ya kumaliza kuandaa, hakutaka eti nianze kula mwenyewe, alianza kunilisha kama mtoto mdogo, tena akiwa ndani ya upande wa khanga nyepesi tu kwa sababu aliingia akiwa amevaa dela lakini akasema eti huwa hapendi mwili wake kubanwabanwa anapokuwa, kwa hiyo akalivua na kujifunga khanga.
Akaongeza kasi ya feni kisha ndiyo akaanza kunilisha sasa huku na yeye akila, yaani ilikuwa ni burudani isiyo na kifani, kidume nikawa nalishwa huku nikisindikizwa na mabusu motomoto.
Baada ya kumaliza kula, nilinyweshwa juisi moja matata sana ambayo mamdogo aliniambia eti ameiandaa kwa ajili yangu, ilikuwa na mchanganyiko wa tende, maziwa na vikorombwezo vingine kibao, wale wazee wa pwani wanajua shughuli yake ukinywa juisi ya aina hii.
Basi baada ya kumaliza glasi nzima, tena ile kubwa, nilijilaza huku nikipumua juujuu utafikiri chatu aliyemeza mbuzi, mamdogo akakusanya vyombo na kuviweka kwenye kona, nikamuona akilichomoa kufuli lake na kulitupa pembeni kisha akasogea pale kitandani na kujilaza, ‘maruhani’ yakaanza kunipanda.
“Ahsante kwa chakula kitamu.”
“Usijali mume wangu, huu ni mwanzo tu, mazuri zaidi yanakuja. Ila sitaki utoke kitambi kama baba’ako mdogo, uwe unafanya mazoezi sawa mume wangu,” aliniambia huku akinibusu, basi tukaendelea kupiga stori za kimahaba za hapa na pale wakati tukisubiri chakula kishuke.
Mapenzi aliyokuwa ananionesha mama mdogo yalininifanya nijisahau mno, yaani nikawa najihisi kwamba mimi ndiyo mwenye mali sasa.
Haukupita muda mrefu alianza vimichezo vyake vya kuchezeana nywele, ukichanganya na ile juisi niliyokunywa, nilishtukia mkuu wa kaya akifurumuka kwa kasi ya kiberenge kutoka kwenye maficho yake, akawa amefyumu kwelikweli.
Kwa makusudi kabisa, aliamua kuja na ingizo jipya kwa kukamata kipaza sauti kisha akaanza kughani taratibu mashairi ambayo yalipenya mpaka kwenye mboni za macho yangu, basi nikawa naugulia tu nikiwa najihisi kama nataka kupaa bila kuwa na mabawa.
Wakati akiendelea kughani, alikuwa akijigeuzageuza na haukupita muda mrefu chungu cha asali kikawa kimegeuziwa upande wangu, nilishajua alichokuwa anakitaka basi kwa umahiri mkubwa nikaanza kulamba asali kama paka anavyolamba maziwa ya ng’ombe kwenye kibakuli.
Ni kama hakutegemea kilichotokea, basi akazidi kuking’ang’ania kipaza sauti huku kasi ya kushusha mashairi ikiongezeka, na mimi nikazidi kulamba asali ya nyuki wasiong’ata kutoka mkoani Tabora.
Ni kama alizidiwa kwani alichomoka kwa kasi ya mshale na kusimama huku akijinyonganyonga, sikutaka kumkaziwa kwa sababu kama ni maji ya mchele, yalishachemka vya kutosha na sasa kilichokuwa kinatakiwa ilikuwa ni kuweka mchele tu ili mapishi yaendelee.
Nilimrudisha eneo la tukio, bila kupoteza muda nikampeleka mkuu wa kaya kwenye eneo alilokuwa akistahili kuwepo kwa wakati huo kwa kazi maalum lakini kabla sijamruhusu achanje mbuga kuingia kwenye ‘mashimo ya Mfalme Suleimani’, nilimgongesha kwa makusudi kwenye kingo za juu za chungu cha asali, mamdogo akaruka kwa nguvu na kutoa ukelele fulani hivi uliozidisha burudani!
“Te...naaa!” alisema kwa sauti iliyoonesha kama alikuwa akifanyiwa uonevu mkubwa kinyume kabisa na haki za binadamu, nikatabasamu na kurudia tena kile kitendo, akaruka tena kwa nguvu, akanisihi niendelee tena na tena, na mimi bila hiyana nikafanya tena na tena, sasa ikawa ni kama mwalimu wa nidhamu anamuadhibu mwanafunzi mtukutu kwa kumchapa fimbo mfululizo bila huruma.
Kitendo hicho kilisababisha aangue dafu kubwa na kulipasua kwa nguvu! Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kushuhudia tukio la aina hiyo kwa sababu kichwani nilikuwa nimeshaamini kwamba ili mtu wa jinsia ya pili aangue madafu, ni lazima akwee mnazi taratibu mpaka juu kabisa, lakini kumbe kulikuwa na njia ya mkato!
Moyoni nikawa nachekelea kwani nilishagundua kamchezo kanakofurahisha sana. Nilimuacha apumue kidogo kisha nikamuweka sawa na kuendelea na kazi na safari hii ilikuwa ni zamu ya mkuu wa kaya kujinafasi. Mamdogo hakuchukua raundi, akakwea tena mpaka juu ya mnazi na safari hii aliangua madafu mawili kwa mpigo na alipoyapasua yote, alikuwa ni kama amepoteza fahamu.
Sikujali, niliendelea na kazikwa muda mrefu bila kuchoka, mpaka nakuja kuzifumania nyavu, mwili mzima ulikuwa umelowa kwa jasho chapachapa utafikiri nimemwagiwa maji. Cha ajabu kilichonishtua, mama mdogo bado alikuwa ametulia vilevile, nikajaribu kumtingisha lakini hakuzinduka, nikamshika mkono, kumuachia mkono nao ukaanguka pembeni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida nikijua lazima atakuwa amepatwa na jambo baya.
Kwa kuwa kidogo nilikuwa nayajua mambo ya huduma ya kwanza, ilibidi nianze kumpa huduma ya kwanza, niliongeza kasi ya feni mpaka mwisho, nikachukua upande wake wa khanga na kuanza kumpepea kwa nguvu lakini haikusaidia chochote.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikitoka mbiombio na kwenda kuchukua ndoo ya maji, bahati nzuri ni kwamba hapakuwa na mtu yeyote pale uani, nikaingia nayo kule ndani na kuanza kummwagia mamdogo maji ya baridi lakini bado haikusaidia kitu.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 19





ILIPOISHIA:
Kwa kuwa kidogo nilikuwa nayajua mambo ya huduma ya kwanza, ilibidi nianze kumpa huduma ya kwanza, niliongeza kasi ya feni mpaka mwisho, nikachukua upande wake wa khanga na kuanza kumpepea kwa nguvu lakini haikusaidia chochote.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikitoka mbiombio na kwenda kuchukua ndoo ya maji, bahati nzuri ni kwamba hapakuwa na mtu yeyote pale uani, nikaingia nayo kule ndani na kuanza kummwagia mamdogo maji ya baridi lakini bado haikusaidia kitu.
SASA ENDELEA...
Alikuwa amelala kama aliyepoteza fahamu, nikaendelea kumtingisha kwa nguvu lakini bado hali ilikuwa ni ileile, nikawa nimechanganyikiwa kabisa, nikiwa sijui nini cha kufanya. Nikiwa nababaika mle ndani, ghafla alizinduka kama mtu aliyekuwa kwenye usingizi mzito.
“Eeeh! Enheee, unaniita,” alisema mam’dogo huku akiwa ametoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.
“Nenda ndani ukapumzike, nakuomba,” nilisema huku kijasho chembamba kikinitoka, akawa bado anashangaashangaa kuonesha kwamba akili zake bado hazikuwa zimekaa sawa.
“Naomba maji ya kunywa,” alisema kwa sauti kavu, harakaharaka nikampa chupa ya maji ambayo yeye ndiye aliyeniletea wakati wa msosi, wakati nahangaika kutafuta glasi, alikuwa tayari ameshaanza kuyagida yale maji kwenye chupa. Alipoishusha chini, tayari ilikuwa tupu, nikabaki namshangaa.
“Nisaidie kuinuka,” alisema huku akininyooshea mkono, akionesha ni kama anaugulia ndani kwa ndani, nilimsaidia, akasimama lakini nilipomuachia, alipepesuka na kutaka kuanguka, nikawahi kumdaka, ukichanganya na ubonge wake haikuwa kazi nyepesi.
“Vipi kwani, unajisikiaje?”
“Hata sijielewi! Nipe nguo zangu,” alisema, nikafanya kama alivyosema. Huwezi kuamini kwamba alishindwa hata kuzirudisha mahali pale, ikabidi nimsaidie. Nilipomaliza aliniambia:
“Nipeleke ndani,” alisema, nikamshika na kuanza kumkokota kuelekea kule kwake. Yaani kama ungetuona ungeweza kudhani labda ni mgonjwa mahututi ambaye anasaidiwa kutoka kitandani kupelekwa maliwatoni wodini.
Uzuri ni kwamba kwa muda huo hakukuwa na mtu pale nje, nikamkokota huku nikimvuta ili tufike ndani haraka. Nilipomuingiza tu ndani, nilimsaidia kujilaza kwenye kochi kisha harakaharaka nikatoka.
Nilienda chumbani kwangu na kuondoa ushahidi wowote wa kimazingira ambao hata likitkea la kutokea, hakuna anayeweza kunihisi kama nahusika. Nilienda kuoga kisha nikarudi na kutokana na mchecheto niliokuwa nao, sikutaka kuendelea kukaa pale nyumbani.
Nilienda kumuaga kule ndani kwake nikiwa ‘nimeshajipigilia’ kisawasawa, kilichozidi kunichanganya zaidi, alikuwa bado amelala akiwa katika hali kama ileile aliyokuwa nayo kule chumbani. Ni kama alikuwa amepoteza fahamu.
Nilimuita mara kadhaa lakini hakuitika, wakati nageuka kutaka kuondoka, alikurupuka na kuanza kuitikia mfululizo huku akishangaashangaa.
“Natoka kidogo.”
“Haya! Haya,” alijibu harakaharaka kisha akalala tena. Nilibaki na maswali mengi ndani ya kichwa changu kuhusu hali iliyomtokea, nikawa natembea harakaharaka huku nikiwa na mawazo mengi ndani ya kichwa changu.
Nilikuwa natembea tu lakini hata sijui naelekea wapi, nikawa napuyanga mitaani na mwisho nilijikuta nikiwa nimefika nje ya geti la Mimah. Kwa siku kadhaa ni kama nilikuwa nimempotezea hivi, kila simu yake ilipokuwa inapigwa, nilikuwa bize na mambo mengine na kibaya zaidi hata sikuwa nikimtafuta tena.
Ni kama mwenyewe alikasirika ndani ya moyo wake kwani hakuwa akinitafuta tena, nikawa najiuliza nitamuanzaje nitakapoonana naye? Nitamueleza nini ili asijue kwamba nilikuwa nampotezea baada ya kuwa nimeshapata kile nilichokuwa nakitaka kwake?
Nilibonyeza kifute cha kengele pale mlangoni, nikawa nasikilizia kwa sababu kwa muda ule, na kwa siku yenyewe nilikuwa na uhakika wa asilimia mia moja kwamba lazima Mimah atakuwa nyumbani.
Baada ya muda, nilisikia mlango wa ndani ukifunguliwa, Mimah akatoka na kuja mpaka pale mlangoni huku nikiwa nimesimama sehemu ambayo haikuwa rahisi kwake kuniona.
Alipofungua mlango, macho yangu na yake yaligongana, katika hali ambayo sikuitegemea, alinipokea kwa tabasamu pana na bashasha ya hali ya juu, akaja kunikumbatia huku akianza kujibebisha kwamba eti alikuwa amenimiss sana, akawa ananibusu mfululizo.
Kwa muda huo wala hata hakuuliza chochote kuhusu kutopokea simu zake, alionesha kuwa na kiu kali na penzi langu. Japokuwa nilikuwa nimechoka kiasi lakini bado na mimi nilikuwa na ‘mzuka’ mkubwa wa kuingia msambweni, hasa baada ya mamdogo kushindwa kumudu kuitii kiu yangu.
Tuliingia mpaka ndani, kumbe Mimah alikuwa akiangalia tamythiliya pale sebuleni, akanikumbatia kwa nguvu na haukupita muda mrefu, tuligusanisha ndimi zetu, jambo lililoamsha bashasha kubwa kwa mkuu wangu wa kaya.
“Kwa nini unaniacha siku zote hizi, mi nakuwa mpweke mwenzio, nimeshakuzoea,” alisema Mimah kwa sauti ya kudeka huku akiingiza mkono kama anayetafuta kitu kwenye kapu, mara akamkamata mkuu wa kaya na kuanza kuhangaika kumtoa.
“Subiri kwanza, mbona pupa!” nilimwambia, nikalegeza mkanda wa suruali ya ‘jeans’ na kumrahisishia kufanya kile alichokuwa anakitaka, akapiga magoti huku akinitazama kwa macho yake ambayo sasa alikuwa akiyarembua kwelikweli, akakamata ‘mic’ kwa mkono mmoja huku ule mwingine akilitoa kufuli lililokuwa mwilini mwake, ukabidi nimsaidie.
Alinisukumia mpaka juu ya sofa, yeye akaendelea kupiga magoti sakafuni na kuendelea kughani kwa hisia za hali ya juu, ulikuwa ni mwendelezo wa burudani ya hali ya juu na kama kuna watu walikuwa na matumizi mabaya ya rasilimali watu, mimi nilikuwa miongoni mwao kwa siku hiyo.
Baada ya kuimba beti mbili kama siyo tatu, nilimuona akiinuka pale alipokuwa amepiga magoti, akakanyaga mguu mmoja upande wangu wa kushoto juu ya sofa, na mwingine akaupandisha na kukanyaga upande wa kulia, akamkamata mkuu wa kaya na kumuelekeza sehemu ya kuelekea kisha akawa ni kama anajaribu kuendesha baiskeli, nikajikuta miguno mfululizo ikinitoka.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 20





ILIPOISHIA:
Baada ya kuimba beti mbili kama siyo tatu, nilimuona akiinuka pale alipokuwa amepiga magoti, akakanyaga mguu mmoja upande wangu wa kushoto juu ya sofa, na mwingine akaupandisha na kukanyaga upande wa kulia, akamkamata mkuu wa kaya na kumuelekeza sehemu ya kuelekea kisha akawa ni kama anajaribu kuendesha baiskeli, nikajikuta miguno mfululizo ikinitoka.
SASA ENDELEA...
Tukiwa tunaendelea kulicheza ‘vanga’, mara tulishtuka baada ya kusikia mlango wa nje ukigongwa kwa nguvu.
Sijui kwa nini nilishtuka mno kuliko kawaida, nikawa natetemeka sana, Mimah na yeye alionesha kushtuka sana, harakaharaka akajitoa kwenye mikono yangu na kukimbilia kuchukua nguo zake, mapigo ya moyo wake yakawa yanamuenda mbio kuliko kawaida.
“Njoo huku,” alisema huku akinishika mkono, akawa ananivutia kule kwenye chumba cha wageni, akaniingiza mpaka ndani na kwenda kunifungia kwenye kabati la nguo.
“Kwani, we umeolewa?”
“Ha...pa...na!” alisema Mimah huku kijasho kikimtoka. Mlango uliendelea kugongwa, nikamuona akitoka mbio na kukimbilia bafuni, akawa anajimwagia maji harakaharaka.
“Karibuuu! Nakujaaa,” aliitikia kutokea bafuni, nadhani ilikuwa ni kwa lengo la kumzuga mgeni wake, nikawa najiuliza maswali mengi ndani ya kichwa changu kuhusu Mimah yaliyokosa majibu.
Kwa kipindi chote tangu nifahamiane naye, alikuwa amenihakikishia kwamba hana mtu lakini binafsi nilikuwa na mashaka kwa sababu aina ya maisha aliyokuwa anaishi, haikuwa kawaida kwa mwanamke peke yake kuwa na mafanikio makubwa kiasi hicho.
Alichokosa lilikuwa ni gari tu lakini alikuwa na nyumba nzuri ya kifahari yenye kila kitu ndani, kwa kifupi alikuwa anaishi maisha mazuri kwelikweli. Nikiwa kule kabatini, nilimsikia akimfungulia mgeni wake na kumpokea kwa bashasha za hapa na pale.
“Jamani mume wangu! Za safari baba, karibu sana,” nilimsikia Mimah akisema, nikajua kwamba kumbe alikuwa na mume ambaye alikuwa amesafiri na ndiyo maana alikuwa anajiachia sana na mimi.
Sio siri nilijisikia wivu mkali ndani ya moyo wangu, licha ya vituko nilivyokuwa namfanyia vya kutojali sana hisia zake, ukweli ni kwamba nilikuwa nampenda sana Mimah na kiukweli aina ya mapenzi aliyokuwa amenipa, yalikuwa ya kipekee sana.
Alionesha kunipenda na kunijali licha ya hali yangu duni niliyokuwa nayo, hakujali aina ya kazi niliyokuwa naifanya, alinipenda kwa moyo wake wote na hiyo ilikuwa ni zaidi ya heshima kwangu. Moyo uliniuma kwelikweli, kwa mara ya kwanza nilielewa jinsi mapenzi yanavyouma.
Basi nikiwa kule kabatini, machozi yalianza kunibubujika, nikawa napumua harakaharaka huku nikihisi maumivu makali sana ya moyo, nikawa naendelea kusikiliza mambo yote yaliyokuwa yakiendelea.
Hata hivyo, kuna wakati nilijitutumua na kuanza kujifariji kwamba sikuwa natakiwa kulia kwa sababu kama ni kumfaidi Mimah, nilikuwa nimemfaidi kwelikweli na utipwatipwa wake.
Swali la msingi ambalo nilikuwa najiuliza, ni kwamba kama kweli huyo aliyeingia ni mume wake, nitawezaje kutoka salama? Haya mambo ya kufumaniwa uyasikie tu, yakikutokea unaweza kutamani ardhi ipasuke uingie.
Basi niliendelea kumsikiliza Mimah akizungumza na huyo mwanaume, akaanza kumsimulia jinsi safari yao ilivyokuwa na ilionesha ni kama alikuwa amemmiss Mimah kwelikweli kwa sababu muda wote alikuwa akimbusubusu.
Baadaye nikawasikia wakikokotana kuelekea chumbani, Mimah alipohakikisha wameingia chumbani, sijui alitumia ujanja gani, akampeleka huyo mwanaume bafuni kisha yeye akatoka mbiombio na kuja kule nilikokuwa nimefichwa.
Akafungua mlango wa kabati na kunionesha ishara kwamba nisipige kelele hata kidogo, akanipa nguo zangu kwa sababu muda wote nilikuwa mtupu, akanipa ishara kwamba nitoke tutazungumza kwenye simu. Nilimtazama Mimah nikiwa ni kama siamini.
Hata hivyo, niliamua kumsaidia kwa sababu alikuwa amepoteza utulivu kabisa ndani ya nafsi yake, macho yake mazuri yalikuwa yamebadilika na kuwa makubwa, hofu ikawa inaonekana waziwazi kupitia macho yake.
Harakaharaka nilitoka jinsi nilivyo na sikutaka hata kugeuka nyuma, nilitoka nikiwa mtupu mpaka kibarazani, kwa kuwa nyumba yenyewe ilikuwa ni ndani ya geti, hakukuwa na mtyu yeyote aliyeniona, basi nikavaa nguo zangu harakaharaka na kuingia mtaani, huku nikijilaumu sana ndani ya kichwa changu.
Kilenilichokuwa nimekikimbia kule nyumbani kilikuw ana afadhali kuliko kile nilichoenda kukutana nacho, haya mambo ya kufumaniwa haya yasikie tu. Basi nililazimika kurudi nyumbani ambako nako nilikofika, mambo hayakuwa shwari.
Kumbe baba mdogoalikuwa amerudi pale nyumbani na kumkuta mkewe akiwa kwenye hali ile lakini kwa sababu ya ujanja wa mwanamke, ‘alimtengeneza’ mumewe kwamba alikuwa akiumwa sana tumbo na ndiyo lililosababisha awe na hali kama ile.
Bila kujua kwamba kumbe mimi ndiye niliyekuwa nimefanya uharibifu ule, baba mdogo alianza kumhangaingia mkewe, mara amchemshie maji ya moto, mara akimbie kwenda kufuata dawa za maumivu dukani, ilimradi pilikapilika za kuonesha nikwa kiasi gani alikuwa anamjali mkewe.
“Ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa nimeenda kwa rafiki yangu mmoja, kuna hela yangu nilikuwa namdai.”
“Sikuoni kama upo siriasi na kazi, una matatizo gani ndani ya kichwa chako?”
“Mimi sina tatizo lolote bamdogo, mbona nipo siriasi sana na kazi yangu?”
“Unaweza kuniambia kwa nini na leo hujaenda kuuza mzigo?”
“Mamdogo aliniambia kwamba yule mteja wa jana anataka samaki wengine, ikabidi niwaache wote hapa.”
“Yaani hela za jana bado hazijalipwa wala samaki hawajachukuliwa, na wewe leo unaambiwa hayo mambo unayakubali! Kwani wewe na mamaako mdogo mna njama gani? Mnataka kuniangusha mtaji si ndiyo?” alisema baba mdogo tukiwa tumesimama nje ya geti huku akionesha kuwa na jazba kubwa ndani yamoyo wake.
“Lakini bamdogo?”
“Lakini nini? Unafikiri sijui mnacjhokifanya si ndiyo?” alisema kauli iliyosababisha mapigo ya moyo wangu yalipuke nakuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 21



ILIPOISHIA:
“Yaani hela za jana bado hazijalipwa wala samaki hawajachukuliwa, na wewe leo unaambiwa hayo mambo unayakubali! Kwani wewe na mamaako mdogo mna njama gani? Mnataka kuniangusha mtaji si ndiyo?” alisema baba mdogo tukiwa tumesimama nje ya geti huku akionesha kuwa na jazba kubwa ndani yamoyo wake.
“Lakini bamdogo?”
“Lakini nini? Unafikiri sijui mnachokifanya si ndiyo?” alisema kauli iliyosababisha mapigo ya moyo wangu yalipuke na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
Akili ya haraka ilinituma kuamini kwamba kumbe baba mdogo anajua mchezo wote tunaoufanya na mkewe, nikawa natetemeka kwa sababu sasa nilijua za mwizi zimetimia, kama baba mdogo alikuwa anajua kwamba nilikuwa nikitia mkono kwenye kapu lake, unafikiria anaweza kuchagua adhabu gani inayonifaa? Nilijikuta nikitetemeka.
“Najua kila kitu Chande, huwezi kunizidi akili wala huyo mama mdogo wako hawezi kunizidi akili. Siku zote huwa nakwambia kwamba wanawake siyo rafiki zetu wa kudumu, umeshindwa kusimamia kazi iliyokuleta kutoka kijijini na sasa umeanza kushiriki kunihujumu.
“Jana samaki wote mmewaweka kwenye friji, leo pia unakubali kurudia makosa yaleyale, unafikiri mtaji ukianguka utabaki hapa mjini kufanya nini? Itabidi urudi kijijini, huwa sifugi mbwa asiyewinda mimi,” alisema baba mdogo kwa jazba, kidogo nikaanza kupata amani ndani ya moyo wangu kwamba kumbe alichokuwa anakijua ni kwamba tulikuwa tukishirikiana kumhujumu na siyo kwamba nafaidi kilicho halali yake.
“Mimi na wewe tunahitaji kuzungumza kwa kina baadaye, nitakuita,” alisema huku akigeuka na kuondoka, nikashusha pumzi ndefu na kujiinamia. Ilikuwa ni siku ya mkosi kwangu.
Niliingia chumbani kwangu na kujifungia mlango, nikavua nguo zote na kujilaza kitandani, nikawa naendelea kutafakari mambo yote yaliyotokea siku hiyo. Nilimtafakari Mimah, nikakosa majibu kabisa juu yake.
“Kumbe ni mke wa mtu? Kwa nini aliamua kunichuuza kiasi hicho? Au pengine ndiyo maana aliamua kukaa kimya kwa sababu alikuwa anajua mumewe anarudi?”
Nilimfikiria pia yule mpangaji, nikawa najiuliza kama nilichokuwa nakihisi awali ni kweli, kwamba baba mdogo anajua kwamba namlia mali zake, nani anaweza kuwa amemtonya kama siyo yeye?
Nilirudisha mawazo yangu na kuanza kumfikiria ma’mdogo! Nikakosa majibu. Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilijikuta nikipitiwa na usingizi mzito pale kitandani. Kisimu changu kilichokuwa kinaita mfululizo ndicho kilichokuja kunizindua, alikuwa ni mama mdogo.
“Uko wapi?”
“Nipo ndani nimelala.”
“Kimenuka mume wangu.”
“Usiniite hivyo mam’dogo, anaweza kusikia ikawa tatizo zaidi.”
“Ametoka! Vipi kwani amekwambia nini?”
“Ameniambia kwamba anajua kila kitu kinachoendelea kati yangu na yako, kwani amejua?”
“Hahaaaa,” mamdogo alicheka kwa sauti, nikawa sijaelewa kicheko chake kinamaanisha nini.
“Unacheka? Hujui anaweza hata kunichinja?”
‘Siyo hivyo unavyofikiria. Ananilaumu kwamba eti mimi nakufundisha wewe usimtii, mimi na wewe tuna njama za kumuulia mtaji wake. Wala hajui kwamba wewe ni mume mwenzie.”
“Mbona ameniambia anajua kila kitu? Na amesema baadaye anataka tuzungumze?”
“Wala usiogope! Niachie mimi kila kitu.”
“Kwa hiyo akiniuliza nimwambieje? Mimi naona bora nikiri makosa tu na kumuomba msamaha!”
“Wee! Wee! Atatuchinja wote! Hajui chochote na hata hapa kabla hajaondoka nimemtuliza kidogo, anachojua ni kwamba njama zetu ni kumuangusha mtaji wake, basi!”
“Kwa hiyo tutafanyaje sasa?”
“Inabidi hawa samaki tuwakusanye kesho tukatoe msaada kwenye kituo chochote cha watoto yatima kwa sababu akiwaona hapa ndani ndiyo anachanganyikiwa. Nimemdanganya kwamba waliokuwa wametuagiza wamesogeza mbele sherehe yao lakini kesho watatulipa fedha zote.”
“Sasa tutapata wapi hela za kurudishia? Au unaonaje mimi nikiingia mtaani na kuanza kuwauza? Najua leo na kesho tu watakuwa wameisha.”
“Huna haja ya kuteseka mume wangu, kesho kuna hela ya vicoba nitaenda kuchukua halafu tutamdanganya kwamba wametulipa. Wewe tulia kabisa, kazi yote niachie mimi,” alisema mamdogo huku akiongea kwa kujiamini, akakata simu.
Kidogo roho yangu ilitulia, hata hivyo ndani ya moyo wangu nikajiambia kwamba mchezo niliokuwa naucheza ulikuwa wa hatari sana na unaweza kusababisha mtafaruku mkubwa sana siku akigundua kilichokuwa kinaendelea kati yangu na mkewe! Mke anauma bwana.
Nilichoamua ndani ya moyo wangu, ilikuwa ni kuanza kumkwepa mamdogo na kupunguza ukaribu kati yetu kwa sababu tulikuwa tunaelekea sehemu mbaya. Nikawa najiuliza kwamba hata nikisema nipunguze ukaribu na ma’mdogo, nitapata wapi tena pa kutulizia machungu yangu wakati Mimah tayari alikuwa ameshanichuuza?
Wakati nikiendelea kutafakari mambo mengi, ndipo nilipomkumbuka mtu muhimu sana ambaye alishaonesha kama ananielewa hivi, ambaye angeweza kuziba vizuri pengo la Mimah na ma’mdogo.
“Mambo!”
“Poa!”
“Mzima?”
“Mzima ndiyo, nani mwenzangu?”
“Mi Chande bwana, yule muuza samaki uliyekutana naye kwenye daladala.”
“Mh! Yaani wewe? Mpaka nikajilaumu kwa nini sikuchukua namba yako siku ile. Ndiyo nini unachukua namba halafu hata hunipigii?”
“Nisamehe bure mwaya, nilikuwa nimesahau jinsi nilivyokusevu kwenye simu yangu. Vipi naweza kukuona?”
“Umeanza hivyo muuza samaki! Unataka kuniona mimi ili iweje?”
“Tulia mrembo, mambo mazuri hayataki haraka,” nilimjibu kwenye meseji, huku moyoni nikianza kuchekelea kwa sababu ilishaonesha kwamba kazi inaweza kuwa nyepesi zaidi ya kumsukuma mlevi.
“Kwani kesho si unaenda Feri?”
“Mh! Sina uhakika sana, kwani kazini unatoka saa ngapi?”
“Kesho siendi kazini, nitapumzika nyumbani nifanyefanye usafi.”
“Nielekeze basi nikufuate unakoishi?”
“Akuu! Kwangu huwa hawaingii wanaume, unataka kuja kunifanya nini?” ilisomeka meseji yake, nikaona kama ananizingua, nikaamua kumpigia kabisa huku ‘mkuu wa kaya’ akiwa ameshaanza kusisimka kutokana na majibu yake ya kichokozi.
Je, nini kitafuatia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom