Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,646
Chombezo: MZEE WA DODO
Sehemu: 01
Mtunzi: Ally Mbetu
SIMU: 0713646500
Tumu aliingia chumbani kwake akiwa na hamu na mkewe baada ya kutoka kuoga pamoja na yeye kumwacha akijipaka mafuta na kutoka nje mara moja baada ya kuitwa na jirani yake. Akiwa katika mazungumzo akili yake yote ilikuwa kwa mkewe kwa kuamini siku ile hamu yake ya muda mrefu kupata penzi la ushirikiano
Alipoingia ndani alimkuta mkewe amelala bila kitu mwilini na macho yake kutua kwenye mahaba yake kwenye kilima kilichokuwa nyuma ya mkewe ambacho kwake kila alipomtazama mwili ulimsisimka. Alifunga mlango na kuondoa taulo iliyokuwa imenyanyuliwa chini kama mkonga wa gari la kubeba vitu vizito.
Alipanda kitandani na kumtikisa mkewe ili wafanya maandalizi kabla ya mchezo. Ajabu mkewe alionekana tayari kapitiwa usingizi mzito na kuanza kukoroma kuonesha amechoka sana na kazi za kutwa nzima. Yeye hamu zilikuwa juu lakini ndiyo hivyo mkewe ambaye kama kawaida alikuwa halali na nguo alikuwa ameisha pitiwa usingizi.
Kutokana na Mungu kumjalia maumbile ya utata hasa alipolalia tumbo Tumu alikuwa kwenye wakati mgumu kwani kila jicho lilipotua kwenye tuta alijikuta kwenye hali mbaya na alipomsogelea na kukutana na joto la asili hapo ndipo usingizi ulipokimbia kabisa na kuhitaji hata mguu wa jini ili alale bila hivyo mzee mzima aliteseka.
Kila alipomtikisa mkewe aliponekana yupo kwenye usingizi mzito, alimtikisa ili amsadie katika kulitafuta chozi moja kwani raha ya wimbo kuimba kwa kupokeza siyo kuimba peke yako. Alimtazama mkewe kwa jicho la uchu lakini tabia za kila siku kujipakulia na kula kisha aondoe vyombo aliiona kama inamnyima raha ya ndoa.
“Bebi..bebi..” Tumu alimtikisa mkewe aliyekuwa hakitambua japo kitanda kilikuwa sita kwa sita. Lakini kitanda chote alikimbaliza yeye miguu na mikono ilikuwa imetawanyika kuonesha amechoka sana kama alikuwa akifua vyuma. Aliendelea kumtikisa ili aamke alie chozi moja la ushirikiano alichoka kila siku kujifanyia self service.
“Mke wangu... Mama Maneno,” Tumu aliendelea kumwita mkewe aliyekuwa akikoroma.
“Mmh,” mkewe aliitika bila kuamka.
“Amka basi.”
“Mume wangu jamani nimechoka.”
“Sawa najua umechoka lakini nami nina haki kama mumeo.”
“Haki gani tena mume wangu?”
“Ya ndoa.”
“Mume wangu lini nimekunyima haki yako?” mkewe alimuuliza akiwa bado amelalia tumbo.
“Unanipatia lakini ya kunisusia.”
“Mume wangu si unajua kazi zangu nachoka sana?”
“Najua lakini na mimi mumeo nina haki ya kufurahia ndoa kwa kupata ushirikiano wako.”
“Mume wangu kila siku nakuachia ule utakavyo sijawahi kukubania kwa vile najua ni haki yako.”
“Unaniachia au unanisusia mpenzi gani nakuwa kama nafanya mapenzi na maiti.”
“Usiseme hivyo mume wangu maiti haina joto la kukufanya ufike safari yako.”
“Mke wangu raha ya mapenzi ni ushirikiano si kuniachia peke yangu,” Tumu alimlalamikia mkewe.
“Basi mume wangu nitajitahidi kukupa ushirikiano,” mkewe alisema huku akijigeuza mkao wa kula.
Tumu aliyekuwa na uchu wa fisi hakuchelewa aliruka mchupo wa mkizi, mwanzo wa mchezo mkewe alijitahidi kuonesha ushirikiano ambao ulimfanya Tumu aufurahie usiku ule. Kila muda ulivyokwenda mkewe kupitia raha ya safari usingizi ulimpitia na kurudi hali ya siku zote ya Tumu kuimba bila ushirikiano.
Mpaka anafika safari mkewe alikuwa akikoroma, hali ile ilizidi kumuumiza sana Tumu na kuiona ndoa yake imekosa furaha. Kazi kwa mkewe imekuwa kila kitu kufikia hatua ya kuiona kazi kama ndiye mumewe. Raha ya ndoa aliipata mwanzo mpaka wapopata mtoto na kupata msichana wa kazi.
Basi kazi zote za ndani alimuachia msichana wa kazi mpaka kumlea mtoto, ikawa yeye na kazi, kazi na yeye. Kila aporudi usiku kutoka kazini aliulizia hali ya mtoto kama amelala hakuwa na shida ya kumuona alioga na kula kisha alipanda kitandani mpaka kesho yake kuwahi kazini.
Tumu alipotaka haki yake ya ndoa mkewe alimsusia afanye mambo yake bila ushirikiano mkewe akiuchapa usingizi wa kazi za kutwa. Tumu kila alipomaliza alimfunika mkewe na yeye kujilaza.
Siku ile nayo ilikuwa kama siku zilizopita, alinyanyuka baada ya shughuli ya upande mmoja, alimuangalia mkewe aliyekuwa kwenye usingizi mzito moyo ulimuuma na kupoteza hamu ya mapenzi na mkewe kutokana na kukosa ushirikiano. Alikwenda msalani aliporudi alimfunika mkewe na yeye kujilaza upande wa pili akiwa hana raha ya ndoa kabisa.
****
Snura mke wa Tumu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu alikuwa na ndoto za kupata mume mzuri chaguo la moyo wake, ombi lake lilitua kwa Tumu kijana mfanya biashara mwenye fedha za kubadili mboga. Ndoto yake ya pili kupata kazi kulingana na elimu yake, dua yake nayo ilipokelewa na kupata kazi katika benki kubwa nchini.
Mwanzo wa ndoa yake mapenzi yalikuwa motomoto kitu kilichomchanganya akili Tumu kwa kujiona sawa na kuokota dodo chini ya mkorosho. Snura pamoja na kuwa na umbile la kuvutia hakuwa mvivu mnapoamua kupimana kifua, kwake ilikuwa mpaka mkwezi useme bhaaaas ndipo akuruhusu uteremke kwenye mnazi wake.
Baada ya kujifungua mtoto mmoja na kuwa na msichana wa kazi aliyefanya kazi zote na yeye kuanza kuongezewa majukumu ya kazi taratibu
alijikuta akibadilika kutokana na kuzidiwa na kazi na kumfanya arudi nyumbani usiku amechoka sana kiasi cha kushindwa kukidhi haja za mumewe.
Kutokana na kurudi amechoka sana na uwezo wa kufanya mapenzi na mumewe wake akiwa macho hakuwa nao alimuomba mumewe kama ameshikika basi amtegeshee yeye ajilie tani yake kama nyani aliyelikuta shamba lisilo na mwenyewe.
Mwanzo mumewe alipokuwa akisusiwa kutokana na uchu na umbile la mkewe lisilo isha hamu. Aliona kawaida alijihudumia mwenyewe kisha alimwaga mzigo na humfunika mkewe na yeye kujilaza. Mwanzo alijua hali ile ni ya muda lakini kumbe iligeuka kuwa mazoea kwa mkewe kila siku kurudi amechoka na kumuachia ajilie, penzi lililokosa ushirikiano na kujiona kama anabaka au kufanya mapenzi na maiti.
NINI kitaendelea? Endelea kufuatilia katika ukurasa wa Hadithi za Ally Mbetu. Pia machombezo mikasa na riwaya utazipata katika Whatsapp kwa kulipia 4000 tu, wahi ili isipitwe na uhondo